top of page

Mwandishi:

Mhariri:

ULY CLINIC

Dkt. Mangwella S, MD

Jumatano, 6 Mei 2020

Sumu kwenye chakula
Sumu kwenye chakula

Kudhuliwa na sumu ya chakula ni dalili zinazoonekana kutokana na kula chakula kilichochangamana na sumu ya bakteria, virusi, fangasi au kemikali za kiwandani au zinazozalishwa na vimelea.


Chakula kinaweza pata sumu wakati wa kuandaa kama mazingira ni machafu mfano mikono ya muadaaji, sehemu ya kuhifadhia chakula, chakula kimekaa muda gani, maji yanayotumika, vyombo vinavyotumika na hali ya kiafya ya muandaaji.


Dalili za mtu aliyedhuriwa na sumu ya chakula huanza kuonekana baada ya saa moja la kula.


Dalili ya kudhuriwa na sumu ya chakula


Dalili mara nyingi hutegemea na aina ya sumu iliyoliwa, baadhidi zinaweza kuwa;


  • Kichefuchefu

  • Kutapika

  • Kuhara maji au damu

  • Tumbo kuuma

  • Tumbo kuvuta

  • Homa


Dalili za hatari


Mara nyingi mtu akila sumu kwenye chakula, dalili huweza isha bila matibabu. Kama utapata dalili zifuatazo, onana na daktari mara moja;


  • Kutapika sana na mara kwa mara kiasi kwamba kitu hakibaki tumboni

  • Kutapika damu

  • Kuharisha kwa zaidi ya siku tatu

  • Maumivu makali ya tumbo au kubana kwa tumbo mara kwa mara

  • Joto la mwili kupanda

  • Dalili za kuishiwa maji mwilini kama kuwa na kiu sana, Kukauka midomo, kuishiwa nguvu, kukojoa kidogo au kutokujoa kabisa na kuhisi kizunguzungu

  • Kutokuona vizuri


Bakteria wanaotengeneza sumu kwenye chakula


  • Campylobacter

  • Clostridium botulinum

  • Clostridium perfringens

  • Escherichia coli (E. coli)

  • Giardia lamblia

  • Listeria

  • Noroviruses (Norwalk-like viruses)

  • Rotavirus

  • Salmonella

  • Shigella

  • Staphylococcus aureus


Makundi ya hatari zaidi kuathiriwa na sumu ya chakula


  • Wajawazito

  • Watu wazima

  • Watoto wadogo

  • Watu wenye magonjwa sugu


Kinga


Ili kujikinga na sumu ya chakula, fanya mambo yafuatayo;


  • Nawa mikono yako, osha vyombo vya chakula na safisha sehemu ambayo chakula knaandaliwa au kuhifadhiwa

  • Tenganisha vyakula ambavyo tayari vimeandaliwa na vile ambavyo havijaandaliwa

  • Pika chakula katika joto ambalo ni sahihi

  • Tunza vyakula kwenye jokofu katika hali ya ubaridi kuepuka kisiharibike

  • Usile vyakula vilivyoharibika au kukaa muda mrefu baada ya kupika endapo havijatunzwa sehemu sahihi

Imeboreshwa,
10 Novemba 2021 11:11:31
Bofya hapa kusoma zaidi kuhusu namna ya kuandaa vyakula mbalimbali vinavyoweza kukukinga dhidi ya magonjwa ya shinikizo la damu la juu na Kisukari, pia kuupa mwili wako uwezo wa kudhibiti magonjwa ya kisukari na shinikizo la juu la damu(presha).

 

ULY CLINIC inakushauri siku zote uwasiliane na daktari wako kwa ushauri na tiba zaidi kabla ya kuchukua hatua yoyote ile ya kiafya baada ya kusoma makala hii.
 

Wasiliana na daktari wa ulyclinic kwa ushauri zaidi na tiba kwa kutumia namba za simu au kubonyeza link ya Pata Tiba chini ya tovuti hii

Rejea za mada hii

  1. MayoClinic.FoodPoisoning.https://www.mayoclinic.org/diseases-conditions/food-poisoning/symptoms-causes/syc-20356230. Imechukuliwa 16/4/2020

  2. HealthLine.FoodPoisoning.https://www.healthline.com/health/food-poisoning. Imechukuliwa 16/4/2020

  3. MedicineNet.FoodPoisoning.https://www.medicinenet.com/food_poisoning/article.htm. Imechukuliwa 16/4/2020

  4. Harrison Principles of Internal Medicine ISBN NI 9781259644030 Written by Tinsley R Harrison ukurasa wa 754

bottom of page