top of page

Magonjwa

Public·783 members

Sumu ya kunywa maji mengi kupita kiasi

Kunywa maji mengi kupitiliza

Haishauriwi kiafya kunywa maji mengi zaidi ya mahitaji ya mwili wako kwa kuwa kiwango kinachozidi huweza geuka kuwa sumu. Kwa bahati mbaya dalili za sumu ya maji kutokana na kunywa maji mengi huwa ngumu kutambuliwa kirahisi na wataalamu wa afya kwa kuwa dalili zake hufanana na magonjwa ya akili, endapo tatizo lisipofahamika mapema na kupata tiba huleta madhara makubwa pamoja na kifo.

 

Tatizo la sumu ya maji linalotokea kutokana kuwa na maji mengi mwilini kuliko kiwango cha chumvi hutokea kwa nadra na huweza pelekea kifo.

 

Dalili za mtu aliyekunywa maji mengi kupitiliza


9 Views

Tetekuwanga

Tetekuwanga ni ugonjwa unaosababshwa na kirusi Varicella zoster AU kirusi tetekuwanga. Ugonjwa huu husababisha harara ndogo na malenge kwenye ngozi yanayoambatana na muwasho.


Dalili za tetekuwanga

Tetekuwanga huonekana siku 10 hadi 21 baada ya kupata maambukizi. Dalili kuu ya ugonjwa huu huwa ni malengelenge madogo yanayowasha na hudumu kwa muda wa siku 5 hadi 10. Dalili zingine zinazoonekana siku 1 hadi 2 kabla ya kuona vipele ni;

  • Homa

  • Kukosa hamu ya kula

  • Maumivu ya kichwa


15 Views

Homa baada ya chanjo

Kwanini homa hutokea baada ya chanjo?


Chanjo hutayarisha mfumo wa kinga ya mwili kuulinda mwili dhidi ya virusi au bakteria wanaoweza kuleta ugonjwa. Homa hii hutokea kwa sababu chanjo huwa na viunda vya vijidudu hivyo ambavyo vinajulikana kuamsha mwitikio wa kinga ya mwili. Hata hivyo, chanjo huwa hazisababishi mwitikio wa unaoweza kumfanya mtu kuugua ugonjwa kama wanavyosababisha vimelea asili. Kwa baadhi ya watu, mwitikio wa kinga ya mwili huwa na nguvu ya kutosha kusababisha dalili zinazoweza kuonekana kama vile homa kali.


Nini unapaswa kufanya unapopata homa?


Mara nyingi si lazima kutumia dawa za kushusha homa kama vile paracetamol unapopatwa na homa baada ya kuchoma chanjo. Inashauriwa kunywa maji ya kutosha tu wakati huu. Kama unafikiria homa ni kali au inakupelekea kukulaza, wasiliana na daktari wako kwa ushauri na tiba.


Rejea za mada hii:


  1. Ahn SH, Zhiang J, Kim H, Chang S, Shin J, Kim M, Lee Y, Lee JH, Park…


7 Views

Magonjwa ya ngono

Magonjwa ya ngono hufahamika pia kama magonjwa ya zinaa, ni magonjwa yanayoenezwa kwa njia ya kujamiana. Kuna njia mbalimbali za kujamiana ambazo zinafahamika. Njia zote hizi zinaweza kuwa chanzo cha kueneza magonjwa hayo.


Makundi ya maonjwa ya ngono


Magonjwa ya ngono yamegawanywa kwenye makundi mawili makuu, magonjwa ya ngono yanayotibika na yale yasiyotibika. Mifano ya magonjwa hayo imeelezewa hapa chini, kusoma zaidi bofya ugonjwa husika.


Magonjwa ya ngono yanayotibika


Baadhi ya magonjwa ya ngono yanayotibika ni:


  • Klamidia (Chlamydia)


68 Views

Kuhusu kundi

Sehemu ambayo imeandikwa magonjwa mbalimbali yanayowapata bi...

bottom of page