top of page

Dalili na viashiria bonyeza herufi ya kwanza kusoma zaidi

[A] [B] [C] [D] [E] [F] [G] [H] [I] [J] [K] [L] [M] [N] [O] [P] [Q] [R] [S] [T] [U] [V] [W] [X] [Y] [Z] [#]

Mwandishi:

Dkt. Benjamin M, MD

Mhariri:

Dkt. Adolf S, MD

22 Machi 2020 13:22:27

Matibabu ya mikraruzo na majeraha madogo mwilini

Matibabu ya mikraruzo na majeraha madogo mwilini

Kila mtu ana Kihatarishi cha kupata majeraha madogo kwenye Ngozi kwa kujikata au kukwaruzwa na kitu au kuanguka. Wakati mwingine unapopatwa na tatizo hili unaweza kuwa na hofu ya nini kitakachotokea baada ya majeraha hayo. Sehemu hii imezungumzia kuhusu matibabu ya nyumbani ya majeraha madogo.


Majeraha madogo kwenye Ngozi ni nini?


Aina za majeraha kwenye Ngozi yanaweza kuwa ni majeraha madogo ambayo hayajazama ndani ya Ngozi au majeraha yaliyozama ndani.


Majeraha ambayo hayajazama ndani ni kama vile;

Mikraruzo kwenye Ngozi, abrasheni, kuungua kwa Ngozi ya juu. Mikraruzo hutokea sana kwenye magoti kiwiko cha mkono na viganja vya mikono. Huweza kutokana na kuanguka wakati mtu anatembea au kukimbia.


Majeraha ambayo yamezama ndani Zaidi


Mareraha ya kukatwa na kitu chenye ncha kali, lasalesheni, na kusagika kwa Ngozi

Jeraha la bruizi


Wakati gani unahitaji matibabu ya kushonywa na nyuzi unapokuwa na majeraha kwenye ngozi?


  • Jeraha lolote lile ambalo limepasua Ngozi na kuzama Zaidi ya milimita 12 kwenye Ngozi linahitaji kushonwa ili lisipone kwa kuleta kovu kubwa

  • Michaniko kwenye uso Zaidi ya milimita 6 inahitaji kushonwa pia

  • Kidonda chochote kinachohitaji matibabu ya kushonywa kinatakiwa kionwe mapema iwezekanavyo na daktari ikiwezekana ndani ya masaa sita toka jeraha limetokea. Malengo ni kuzuia maambukizi yasitokee kwenye kidonda maana yanaweza kubadili matibabu


Je unajuaje hili ni jeraha la mkraruzo au la kukatwa?


Ni muhimu ukiwa unaamua kutibu majeraha madogo ukatathmini mambo yafuatayo.


  • Ngozi ya binadamu ina upana wa milimita 3

  • Majeraha ya kujikata na lasaresheni hukata upana huu wote

  • Mikraruzo huwa mara nyingi haimalizi upana wote wa ngozi

  • Majeraha ya kujikata ambayo yanaweka uwazi wakati wa mjongeo yanahitaji kushonwa ili kuzuia kupona kunakoambatana na makovu

  • Mikraruzo na majeraha yanayofanana nayo mara nyingi huwa hayahitaji kushonwa hata yakiwa yamedhuru eneo kubwa kiasi gani



Wakati gani wa kuwasiliana na daktari?


Ukiwa na majeraha ya ngozi, mpigie daktari wako haraka kwa huduma ya kwanza endapo;


  • Ngozi imekatwa na ina hitaji kushonwa

  • Maumivu makali kuendelea masaa mawili baada ya kutumia dawa za maumivu

  • Kuwa na umri chini ya mwaka mmoja

  • Kuna uchafu kwenye kidonda hata baada ya kujisafisha na maji safi

  • Ngozi imeraruka

  • Mikraruzo iliyo athiri sehemu kubwa ya mwili

  • Mikraruzo au majeraha ya kujikata yanayoonekana kuwa yana maambukizi (kuwa mekundu, kutoa

  • usaha)

  • Kama umejikata na hujapata chanjo ya tetenasi au chanjo imeisha muda wake

  • Kama unafikiria una jeraha kubwa

  • Kuwa na bruizi kubwa licha ya kuwa na jeraha dogo sana

  • Bruizi kutokea bila jeraha lolote

  • Kidonda hakiponi licha ya siku 10 kupita

  • Una maswali mengine au unahitaji ushauri


Matibabu ya nyumbani ya mikwaruzo kwenye ngozi

Matibabu ya majeraha ambayo hayajazama chini ya Ngozi


Tumia nguvu kiasi kugandamiza maeneo hayo ili yasiendelee kuvuja damu, fanya hivi kwa dakika 10 mpaka damu itakapoacha kutoka

Osha eneo lililoathirika kwa kutumia maji yanayotiririka kwa muda wa dakika 5

Tahadhari- usiloweke eneo ambalo litahitaji kushonwa maana litavimba na kusababisha lisiweze kushonwa kirahisi

Tumia tauro safi isiyoacha nyuzunyuzi ili kuondoa uchafu kwenye kidonda endapo hautoki kwa kuosha tu

Tumia dawa ya antibayotiki ya kupaka kama vile polysporin kutoka kwenye maduka ya dawa baridi. Au mpigie daktari wako akuandikie. Baada ya kupaka hakikisha unafunika eneo na bandeji mpya. Na fanya ivi kila siku


Matibabu ya Majeraha madogo ya kujikata

Tumia dandeji tepe kufunika kidonda. Hii inaweza kufunika kidonda kwa muda wa wiki moja tu

ukilinganisha na badeji zingine ambazo zinatakiwa kubadilishwa kila siku, pia huchochea kupona kwa kidonda haraka na kuzuia maambukizi.


Matibabu ya bruizi

Matibabu ya bruizi hayajaongelewa hapa ila yameongelewa sehemu nyingine kwenye tovuti hii


Dawa za maumivu mtu mwenye majeraha kwenye ngozi

Ili kuondoa maumivu unahitaji kutumia dawa za kupunguza maumivu kama vile parasetamo au ibrupofen.


Ingia kwenye mada ya dawa za maumivu kusoma Zaidi kuhusu dawa za kupunguza maumivu.


Chanjo ya tetenasi kwa mgonjwa mwenye majeraha kwenye ngozi


  • Unatakiwa kupata chanjo endapo chanjo ya tetenasi uliyopewa tayari imeisha muda wake

  • Soma zaidi kwenye Makala zetu muda gani chanjo ya tetenasi hudumu mwili na wakati gani unatakiwa kupata chanjo nyingine.

  • Kwa vidonda ambavyo vimesababishwa na vitu vichafu au kupatwa na uchafu wakati wa kupata jeraha unatakiwa kupigwa chanjo ya tetenasi ili kubusti endapo miaka mitano imeshapita toka upate chanjo ya mwisho.

  • Kwa kidonda kisafi au ambacho kimesababishwa na kitu kisafi kisicho na kutu au mchanga, utatakiwa kupata chanjo ya kubusti ya tetenasi endapo muda umeshapita miaka kumi tokea upate chanjo ya mwisho.


Lini kidonda kitapona?


Kwa vidonda vidogo vya kujikata au kukwaruza kidonda kitapona ndani ya muda wa wiki moja

ULY CLINIC inakushauri siku zote uwasilianane na daktari wako kwa ushauri zaidi na tiba kabla ya kuchukua hatua yoyote baada ya kusoma makala hii

Wasiliana na daktari wa ULY clinic kwa kupiga namba za simu  au kubonyeza sehemu imeandikwa "Pata tiba" chini ya tovuti hii.

Imeboreshwa,

21 Julai 2023 16:20:09

Rejea za mada hii;

1. Bailey & Love's Short Practice of Surgery, chapisho la 27
2. American College of Emergency Physicians Foundation: "Cuts and abrasions."

bottom of page