top of page

Mwandishi:

Dkt. Sospeter M, MD

Mhariri:

Dkt. Lugonda B, MD

3 Aprili 2020 18:30:55

Aspirini

Aspirini

Dawa hii kwa jina lingine hujulikana kama acetylsalicylic asidi.

Hutumika sana kupunguza homa na maumivu kiasi na wastani yanayotokana na maumivu ya misuli, maumivu ya jino na homa baridi. Dawa hii pia inaweza kupunguza maumivu ya athraitizi.

Sifa za dawa


  • Ipo kwenye kundi la dawa zijulikanazo kwa jina la NSAIDs

  • Hutumika kutibu homa pamoja na maumivu

  • Hupatikana katika mfumo wa kidonge

  • Mara nyingi rangi ya dawa hii ni nyeupe

  • Dawa hii inapaswa kutumika pamoja na chakula ili kuepusha maudhi kwenye mfumo wa chakula

Dawa zingine ambazo zipo kwenye kundi moja pamoja na acetaminophen ni:


  • Paracetamol

  • Diclofenac

  • Ibuprofen

  • Naproxen

Jinsi inavyofanya kazi mwilini?


Dawa hii hufanya kazi kwa kuzuia utengenezwaji wa kemikali ya prostaglandin mwilini. Kemikali hii hufahamika kusababisha maumivu ,homa na infamesheni.

Kazi za Aspirin Mwilini ni kama zifuatazo:


  • Hutumika kuondoa na kutibu maumivu

  • Hutumika kuondoa homa

  • Hutumika kupunguza sindromu ya akyuti koronari, huu ni moja ya ugonjwa wa moyo unaotokana na kuziba kwa mishipa ya damu ya koronari.

  • Hutumika kupunguza kasi ya kupata magonjwa ya moyo kwa wagonjwa waliopo katika kundi hatarishi kupata hasa miaka 40-70

  • Hutumika kwa wagonjwa wa kiharusi cha iskemia na iskemia ya mpito

  • Hutumika kwa wagonjwa wa osteoarthraitisi, arthraitisi ya rheumatoid haya ni magonjwa ambayo hupelekea kupata maumivu na kuvimba kwenye maungio ya mwili dawa hii hutumika kuzuia maumivu na uvimbe.

  • Hutumika kuzuia saratani ya kolorekto

  • Hutumika kutibu maumivu ya kipanda uso

Aspirini haipaswi kutumika pamoja na dawa zifuatazo:


  • Dichlorphenamide

  • Ketorolac

  • Captopril

  • Ibuprofen

  • Methotrexate

  • Fosinopril

  • Enalapril

  • Macimorelin

Dawa hii haipaswi kutumika kwa wagonjwa wafuatao:


  • Vidonda vya tumbo vinavyotoa damu

  • Anemia ya Hemolitiki

  • Ugonjwa wa hemophilia

  • Wenye polipu (nyama) puani zilizosababishwa na pumu

  • Wagonjwa wenye kidole tumbo (appendisaitizi)

  • Pumu

  • Kuhara kwa muda mrefu

Dawa hii inapaswa kutumika kwa tahadhari kwa wagonjwa wafuatao:


  • Wenye upungufu wa damu

  • Wenye historia ya vidonda vya tumbo

  • Wagonjwa wa Ini

  • Wenye Figo iliyoferi kutokufanya kazi

  • Wenye upungufu wa vitamin K

  • Watumiaji wa pombe

Kwa mama mjamzito na anayenyonyesha.


  • Kwa mama mjamzito: Endapo kuna ulazima wa kutumia dawa hii, dozi ndogo itumike ili kumuepusha mama pamoja na mtoto kwenye magonjwa ya kuvuja damu.

  • Kwa mama anayenyonyesha: Haipaswi kutumika kwa mama anayenyonyesha sababu ina madhara kwa mtoto. Huweza kuleta shida ya kutokwana damu pasipo kuganda kwa mtoto.


Baadhi ya maudhi madogo ya dawa hi ni pamoja na :


  • Maumivu ya tumbo

  • Kichefuchefu

  • Masikio kupunguza usikivu

  • Kuharibu ini

  • Kuharibu figo

  • Kutapika

  • Kubana kwa njia za hewa na kuleta shida katika upumuaji

  • Kuvimba kwa ngozi ndani bila maumivu

  • Matatizo ya damu kutoganda kirahisi

Je endapo utasahau dozi yako ufanyaje?


Endapo ukisahau kunywa dozi yako, unaweza kunywa mara pale utakapokumbuka ,Isipokuwa endapo muda wa dozi nyingine umeshafika unatakiwa kuruka hiyo dozi uliyosahau na kuendelea na dozi yako kama muda uliopangiwa

ONYO: Usitumie dawa yoyote bila ushauri wa daktari. Dawa zinaweza kuleta madhara mwilini na pia matumizi ya baadhi ya dawa pasipo ushauri na vipimo husababisha  vimelea kuwa sugu dhidi ya dawa hiyo.
ULY clinic inakushauri kuwasiliana na daktari wako unapotaka kuchukua maamuzi yoyote yanayohusu afya yako.
Wasiliana na daktari/Mfamasia wa ULY clinic kwa ushauri na Tiba au kuandikiwa dawa kwa kupiga simu au Kubonyeza Pata tiba chini ya tovuti hii.

Imeboreshwa,

3 Novemba 2021 11:49:33

Rejea za mada hii:-

1.Goodman and Gilman’s The pharmacological Basis of therapeutic ISBN 978-0-07-1624428 ukurasa wa ,75 na 764.

2.Modern pharmacology with Clinical applications written by Charles R. Craig and Robert E. Stitizel Ukurasa wa 256.

3.Clinical pharmacology and Therapeutics Written by James M Ritter ISBN 978-0-340-90046-8 ukurasa wa 48,143 na 157.

4.Medicinenet. Aspirin. https://www.webmd.com/drugs/2/drug-1082-3/aspirin-oral/aspirin-oral/details Imechukuliwa 2/4/2020.

5.Medscape. Aspirin dosage. https://www.webmd.com/drugs/2/drug-1082-3/aspirin-oral/aspirin-oral/details. Imechukuliwa 2/4/2020
bottom of page