top of page

Kamusi Tiba ya ULY CLINIC

AIDS ni nini?

AIDS

Ni hatua ya mwisho ya maambukizi ya virusi vya UKIMWI (VVU), ambapo kinga ya mwili huwa dhaifu sana. Hali hii humfanya mtu kuwa rahisi kushambuliwa na magonjwa mbalimbali nyemelezi.

Aaron’s sign

Aaron’s sign

Ni maumivu ya upande wa kulia wa tumbo yanayotokea unaposhinikiza sehemu ya chini ya kifua. Ni dalili inayoweza kusaidia kubaini uvimbe wa kidole tumbo (appendicitis), hasa kwa watoto.

Abadie’s sign

Abadie’s sign

Huonekana kwa wagonjwa wenye kisonono cha neva, ambapo mishipa ya fahamu imeathiriwa na hivyo hupoteza uwezo wa kuhisi maumivu.

Abdominal mass ni nini?

Abdominal mass

Ni uvimbe au mkusanyiko wa tishu usio wa kawaida unaopatikana ndani au juu ya sehemu ya tumbo. Uvimbe huu unaweza kuwa mgumu au laini, na mara nyingine unaweza kuambatana na dalili kama maumivu, kujaa, au mabadiliko ya haja kubwa na ndogo, na huhitaji uchunguzi wa kitaalamu kubaini chanzo chake.

Abortion ni nini?

Abortion

Ni kitendo cha mimba kuharibika au kukatizwa kabla ya kijusi kufikia uwezo wa kuishi nje ya mfuko wa uzazi, kawaida kabla ya wiki ya 20 ya ujauzito. Inaweza kutokea kwa njia ya asili (mimba kutoka yenyewe) au kwa makusudi (kutoa mimba kwa njia ya matibabu au upasuaji).

bottom of page