top of page
Vidokezo vya Afya

Acha mazoea ya kula chakula taka
Chakula taka, ni aina ya chakula kisicho na thamani kubwa mwilini mwako. Sifa yake kubwa ni kuwa na nishati kwa wingi zinazotokana na mafuta au sukari, huku kikikosa au kuwa na kiwango kidogo sana cha protini, vitamin, madini, nyuzinyuzi na virutubisho vingine muhimu kwa mwili wako. Acha uteja wa kula chakula taka, kula vyakula vinavyoshauriwa kiafya.

Acha mazoea ya kutumia dawa za maumivu jamii ya NSAIDS
Asilimia 15 ya watumiaji wa dawa za kupunguza maumivu jamii ya NSAIDS kama Ibuprofen, Indomethacin, aspirin, naproxen n.k, wana hatari ya kupata vidonda vya tumbo vinavyopelekea kutapika damu. Tumia njia mbadala au tumia dawa za maumivu inapolazimika.
bottom of page



