top of page

Mwandishi;

Dkt. Mercy M, CO

Mhariri;

Dkt. Mangwella S, MD

16 Septemba 2021, 11:27:01

Kirusi zika

Kirusi zika

nyingi huwa hasababishi ugonjwa mkali na dalili zake kuu ni homa, maumivu ya kichwa, misuli, maungio ya mwili na macho mekundu.


Kirusi husababisha nini?


Kirusi zika husababisha homa ya wastani na wakati mwingine homa kali inayoambatana na upele mwilini hasa maeneo ya kifua uso, viganja na miguu.


Msambazaji wa kirusi


Kirusi cha ziko husambazwa na mbu jike aina ya Aedes hasa Anopheles Aegyptindiye.


Kirusi cha zika kilianza mwaka gani


Tafiti zinaonesha kuwa kirusi cha zika kilianza kuonekana kwa mara ya kwanza kwa nyani mwaka1947 huko Uganda na mwaka 1948 virusi hawa walionekana kwa mbu aina ya Aedes na ripoti ya kwanza kwa binadamu ilionekana mwaka 1952 uganda na Tanzania. Milipuko mingine ya kirusi zika imewahi ripotiwa baada ya miaka hiyo kwenye nchi zingine za Afrika, Americas, Asia na bahari ya pasifiki.


Familia ya kirusi


Kirusi cha zika ni kimoja wapo kwenye familia ya Flaviviridae, Virusi katika familia hii hufahamika kwa kusababisha Homa kali.


Sifa za kirusi


Kirusi Zika ni ni aina ya kirusi chenye RNA moja katika familia ya virusi vya Flaviviridae yenye sifa zifuatazo;


  • Hupatikana kwenye wadudu jamii ya arthropodi

  • Huwa na umbile la uzi

  • Ukuta wake umefungwa

  • Huwa warefu

  • Wana RNA moja


Virusi vya familia flaviviridae


Baadhi ya virusi vingine kwenye familia ya Flaviviridae ni;


  • Kirusi cha homa ya njano

  • Kirusi Tick-borne encephalitis

  • Kirusi West Nile

  • Kirusi dengue

  • Kirusi chikungunya


Mtunzaji wa kirusi


Kirusi cha Zika hutunzwa na binadamu, m'bu jike aina ya Aedes na nyani.


Uenezaji w akirusi


Kirusi cha Zika kinaenezwa kwa njia zifuatazo;


Kung’atwa na mbu jike aliyebeba virusi kutoka kwa mgonjwa wa zika

Kujamiana bila kinga (virusi hawa wameonekana kwenye shahawa za mwanaume)

Kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto

Kwa kuongezewa damu


Dalili za ugonjwa wa Zika


Kipindi cha kuatema cha kirusi zika ni kati ya siku 3 hadi 14. Mtu hawezi kusambaza ugonjwa mpaka pale dalili zitakapoonekana. Dalili za ugonjwa zake huwa pamoja na;


  • Homa kali

  • Uchovu

  • Maumivu ya kichwa

  • Kukosa hamu ya kula

  • Upele mwilini hasa kifuani, usoni, viganja na miguu


Dalili zingine ni;


  • Hisia za maumivu nyuma ya macho

  • Kuvimba mitoki

  • Kuharisha

  • Kuvimba miguu na mikono

  • Kuumizwa na mwanga

  • Kikohozi

  • Uchovu

  • Maumivu ya mgongo

  • Vidonda vya aphthous

  • Kutokwa na jasho


Magonjwa linganifu


Magonjwa yanayofanana dalili na ugonjwa wa zika ni pamoja na;


  • Malaria

  • Ebola

  • Homa ya njano

  • Homa ya chikungunya

  • Influenza

  • Measles

  • Rubella

  • Ugonjwa wa Corona virus diseases

  • Maambukizi ya Streptococcal kundi A


Vipimo tambuzi


  • Picha nzima ya damu

  • Kipimo cha PCR ya kirusi Zika

  • Kipimo cha Immunoglobulin M (1gM)

  • Kipimo cha Immunoglobulin G (1gM)

  • Kipimo cha Nucleic Acid Amplification (NAATs)

  • Kuotesha kirusi


Matibabu


Hakuna dawa maalumu inayotumika kutibu maambukizi ya kirusi Zika na hivyo tiba hulenga kupunguza au kuondoa dalili zinazojitokeza na huhusisaha;


  • Kupata muda mwingi wa kupumzika

  • Kunywa maji ya kutosha

  • Kutumia dawa za maumivu kama Acetaminophen(paracetamol) kwa kuzuia homa na maumivu

  • Matumizi ya dawa jamii ya antihistamine kwa ajiri ya vipele na muwasho


Kinga na chanjo


Ili kujikinga na maambukizi ya kirusi zika, fanya yafuatayo;


  • Dhibiti vimelea wanaoeneza kirusi zika kama vile mbu kwa;

  • Kupuliza ndai au kupaka dawa ya kuua mbu wakati wa jioni

  • Punguza au acha safari zisizo za lazima katika maeneo yenye hali ya juu ya maambukizi

  • Vaa nguo ndefu zinazofunika sehemu zote za mwili, tumia pia kofia na soksi ndefu

  • Usiache milango na madirisha wazi isipokuwa kama kuna wavu katika dilisha ambapo unaweza acha madirisha wazi

  • Tumia kinga wakati wa kujamiana.


Je kuna chanjo ya kirusi cha zika?


Hapana! mpaka sasa bado hakuna chanjo iliyogunduliwa kwa kwa ajili ya kirusi zika.


ULY clinic inakushauri uwasiliane na daktari wako siku zote kabla ya kuchukua hatua yoyote inayohusu afya yako


Wasiliana na daktari wa ULY clinin kwa ushauri na Tiba kwa kupiga nambza za simu au kubonyeza "Pata Tiba"chini ya tovuti hii

​

Orodha kuu


Rejea zamada hii;

  1. WHO. Zika virus. https://www.who.int/news-room/fact-sheets/detail/zika-virus. Imechukuliwa 13/09/2021 

  2. MEDSCAPE. Zika virus. https://emedicine.medscape.com/article/2500035-guidelines. Imechukuliwa 13/09/2021 

  3. CDC. Zika. https://www.cdc.gov/zika/about/index.html. Imechukuliwa 13/09/2021 A.D.T. Barrett, S.C. Arboviruses: alphaviruses, flaviviruses and bunyaviruses .https://www.sciencedirect.com/topics/neuroscience/zika-virus. Imechukuliwa 13/09/2021 

  4. CDC. About Zika. https://www.cdc.gov/zika/about/index.html. Imechukuliwa 13/09/2021 

  5. K Gorshkov, et al. Zika Virus: Origins, Pathological Action, and Treatment. https://www.ncbi.nlm.nih.gov/pmc/articles/PMC6330993/. Imechukuliwa 13/09/2021 

  6. Syeda Sidra Kazmi, et al. A review on Zika virus outbreak, epidemiology, transmission and infection dynamics. https://jbiolres.biomedcentral.com/articles/10.1186/s40709-020-00115-4. Imechukuliwa 13/09/2021

Imeboreshwa;

27 Septemba 2021, 12:11:46

bottom of page