Ushauri na Dawa mara moja kwa wasio VIP
Kama umeletwa kwenye ukurasa huu baada ya kujaza fomu (dodoso) ya kutoa taarifa za ugonjwa wako ili daktari aweze kuelewa hali yako, basi umefika hapa makusudi ili kuendelea na hatua inayofuata ya kupata huduma kutoka kwetu.
Tafadhali kamilisha hatua hii ili uweze kuendelea na mchakato wa kuwasiliana na daktari, kupata ushauri wa kitaalamu, pamoja na mapendekezo ya dawa au matibabu yanayofaa kwa hali yako.
Huduma hizi zinakupa ushauri wa kitabibu na kuandikiwa dawa mtandaoni mara moja, kwa kuzingatia viwango vya kimatibabu na maadili ya kitaaluma.
Neno “mara moja” katika maelezo haya linamaanisha kuwa utapatiwa huduma wakati huu uliofika tu. Ikiwa utahitaji huduma tena wakati mwingine, utahitajika kujiunga upya ili kupata ushauri na huduma nyingine.
1️⃣ HUDUMA KWA WASIO VIP – Tsh 20,000/=
Madaktari wanaopatikana
Unaweza kupata huduma kutoka kwa madaktari wa:
-
Ngozi
-
Mifupa
-
Mionzi
-
Watoto
-
Magonjwa ya wanawake
-
Magonjwa ya wazee
-
Magonjwa ya akili
-
Meno
-
Masikio, pua na koo
-
Upasuaji
-
Magonjwa ya kawaida
-
Lishe
-
Macho
Huduma unazopata mara moja kwa tatizo:
-
Ushauri wa moja kwa moja kutoka kwa daktari
-
Maelezo ya tatizo lako kulingana na historia na dalili
-
Kupendekezewa vipimo vinavyohitajika
-
Usomaji wa vipimo na kuandikiwa dawa kwa walioandikiwa vipimo wakati wa huduma ya kwanza
-
Kuandikiwa cheti cha dawa (prescription)
-
Maelekezo sahihi ya matumizi ya dawa
-
Ufafanuzi wa majibu ya vipimo (maabara/mionzi)
-
Ushauri wa dawa sahihi kwa tatizo lako
-
Vidokezo muhimu vya kiafya kulingana na hali yako
Mambo yasiyojumuishwa kwa Huduma hii:
-
Kupewa dawa
-
Kufanyiwa vipimo
-
Kufanyiwa upasuaji
-
Kupigiwa simu
-
Kutembelewa na daktari/mhudumu
Malipo
Lipa Tsh 20,000 kupitia MPESA namba
📞 +255 752 954 281
Baada ya malipo:
➡️ Jaza fomu iliyo chini ya ukurasa → Tuma → Kisha wasiliana na whatsapp namba +255 621 122 578 kwa matibabu.
Muda wa Huduma (Sio VIP)
🕒 Saa 9:30 mchana – 5:00 usiku (15:00–23:00)
📅 Kila siku isipokuwa Jumapili (mapumziko)
Iwapo Huna uwezo wa kulipa
Wasiliana nasi kupitia namba zetu. Utaulizwa maswali ya uthibitisho na ukithibitika kuwa unahitaji msaada, utapewa utaratibu maalumu wa huduma. Pia unaweza kusoma kupitia kurasa ya utaratibu wa huduma zetu kwa maelezo zaidi ya namna ya kupta huduma hii
2️⃣ HUDUMA ZA VIP – Tsh 50,000/=
Huduma za VIP hukupa upendeleo wa muda, majibu ya haraka, na muda mrefu zaidi wa kuwa na mtaalamu wa Afya.
Madaktari Wanaopatikana
(Orodha ni ile ile kama ya wasio VIP)
Huduma unazopata mara moja kwa tatizo:
-
Ushauri wa moja kwa moja na daktari
-
Utambuzi wa tatizo kulingana na dalili na historia
-
Ushauri wa vipimo vinavyohitajika
-
Usomaji wa vipimo na kuandikiwa dawa kwa walioandikiwa vipimo wakati wa huduma ya kwanza
-
Kuandikiwa cheti cha dawa (prescription)
-
Ufafanuzi wa vipimo (maabara/mionzi)
-
Maelekezo ya matumizi ya dawa
-
Vidokezo vya kiafya kulingana na hali yako
Huduma zisizojumuishwa kwenye kifurushi hiki:
-
Kupewa dawa
-
Kufanyiwa vipimo
-
Kufanyiwa upasuaji
-
Kupigiwa simu
-
Kutembelewa na mhudumu
Malipo
Lipa Tsh 50,000 kupitia MPESA namba:
📞 +255 752 954 281
Baada ya malipo: ➡️ Jaza fomu iliyo chini ya ukurasa → Tuma → Kisha wasiliana na whatsapp namba +255 621 122 578 kwa matibabu.
Muda wa Huduma za VIP
-
Jumatatu – Ijumaa: 2:00 asubuhi – 5:00 usiku (08:00–23:00)
-
Jumamosi: 3:00 asubuhi – 5:00 usiku (09:00–23:00)
-
Jumapili: Mapumziko
Usiri na Ubora wa Huduma
ULY Clinic inafuata miiko, maadili, na viwango vya kitabibu.
Taarifa zako zote ni siri kati yako na daktari. Kwa kujaza fomu hii unathibitisha kukubaliana na Vigezo na Masharti ya huduma.
