top of page

RIDHAA YA USHIRIKI WA UTAFITI MTANDAONI

Namba ya Idhini ya IRB: KUIRB-2026-0025-01

TAARIFA ZA JUMLA ZA UTAFITI

Mada ya Utafiti:Uundaji, Utekelezaji na Tathmini ya athari ya jukwaa la afya la Kidijitali linalotumia Akili Unde (AI) kwa Kiswahili ili kuongeza uelewa wa Afya miongoni mwa Wagonjwa na Wahudumu wa afya wa kada ya kati nchini Tanzania.


Utafiti huu unahusisha binadamu na unafanyika mtandaoni. Ushiriki ni wa hiari kabisa na ni kwa watu wanaokubali kushiriki baada ya kusoma na kuelewa maelezo haya.

1. HATI YA MAELEZO YA USHIRIKI WA UTAFITI

Maelezo haya yametolewa kueleza kwa nini utafiti huu unafanyika, jinsi taarifa zako zitakavyotumika, pamoja na faida, hatari au usumbufu wowote unaoweza kutokea kutokana na ushiriki wako. Ikiwa una swali au kuna jambo lolote halieleweki, una haki ya kuuliza kabla ya kuendelea.


1.1 Madhumuni ya Utafiti na Faida Zinazotarajiwa

Watu wengi nchini Tanzania hupata changamoto ya kupata taarifa za afya zilizo wazi na za kuaminika katika lugha wanayoielewa kikamilifu. Utafiti huu unalenga kuunda na kupima jukwaa la afya ya kidijitali linalotumia Akili Unde (AI) kwa Kiswahili ili kusaidia wagonjwa na wahudumu wa afya wa kada ya kati kupata taarifa sahihi na rahisi kueleweka.

Madhumuni ya utafiti huu ni:

  1. Kuunda jukwaa la kidijitali linalotumia lugha rahisi ya Kiswahili na linalotumika kirahisi.

  2. Kupima jinsi jukwaa linavyosaidia kuboresha uelewa wa Afya.

  3. Kulinganisha jinsi wagonjwa na wahudumu wa afya wa kada ya kati wanavyotumia na kunufaika na jukwaa.

Huenda usipate faida ya moja kwa moja binafsi, lakini ushiriki wako utasaidia kuboresha elimu ya afya kwa Kiswahili kwa manufaa ya jamii kwa ujumla.


1.2 Washiriki, Muda na Taratibu za Utafiti

Utafiti huu unahusisha takribani washiriki 380: wagonjwa watu wazima 190 na wahudumu wa afya wa kada ya kati 190. Muda wa ushiriki kwa kila mshiriki ni takribani dakika 15–20 na unahusisha matumizi ya jukwaa la afya la kidijitali na ujazaji wa dodoso mara moja.


Utafiti unafanyika mtandaoni kikamilifu na hakuna haja ya kufika kituoni.


1.3 Hatari, Faida, na Haki ya Kujiondoa

Utafiti huu una hatari ndogo sana. Hakuna hatari za kimwili. Usumbufu mdogo unaweza kutokea wakati wa kujibu maswali ya dodoso. Taarifa zote zitahifadhiwa bila majina na kwa usalama.


Ushiriki ni wa hiari kabisa. Unaweza kukataa kushiriki au kujiondoa wakati wowote bila madhara yoyote, na taarifa zako zitafutwa endapo utaamua kujiondoa.


Hakuna malipo, fidia, au zawadi zitakazotolewa kwa kushiriki katika utafiti huu.

2. RIDHAA YA UCHAKATAJI WA TAARIFA BINAFSI (LAZIMA)

2.1 Aina ya Taarifa Zitakazokusanywa

Taarifa zitakazokusanywa ni pamoja na: Jinsia, Umri, Elimu, Kazi, Mkoa/Wilaya, aina ya mshiriki (mgonjwa au mhudumu wa afya), na majibu ya dodoso.


2.2 Madhumuni ya Matumizi ya Taarifa

Taarifa zitakazotolewa zitatumika kwa madhumuni ya utekelezaji wa utafiti, tathmini ya ufanisi wa jukwaa la afya la kidijitali linalotumia AI kwa Kiswahili, na uandishi wa machapisho ya kisayansi. Hakuna taarifa binafsi zitakazotumika kumtambua mshiriki.


Taarifa zitahifadhiwa kwa muda wa miaka 3 kuanzia kukamilika kwa utafiti.

Swali la Ridhaa ya Uchakataji wa Taarifa Binafsi
Ninakubali uchakataji wa taarifa binafsi kama ilivyoelezwa hapo juu
Sikubali

3. RIDHAA YA UTOAJI WA TAARIFA KWA MTU WA TATU (LAZIMA)

Taarifa zisizo na utambulisho zinaweza kutolewa kwa Chuo Kikuu cha Korea na Bodi ya Mapitio ya Taasisi (IRB) kwa madhumuni ya mapitio ya kimaadili ya utafiti. Muda wa kuhifadhi ni nusu ya kudumu kulingana na kanuni za IRB.

Swali la ridhaa ya Utoaji wa Taarifa kwa Mtu wa Tatu
Ninakubali utoaji wa taarifa kama ilivyoelezwa
Sikubali

4. RIDHAA YA MATUMIZI YA TAARIFA KWA UTAFITI WA BAADAYE (HIARI)

Taarifa za dodoso zisizo na utambulisho zinaweza kutumika kwa tafiti za baadaye kuhusu uelewa wa masuala ya Afya. Kukataa hakutaathiri ushiriki wako katika utafiti huu.

Swali la Ridhaa ya Matumizi ya Taarifa kwa Utafiti wa Baadaye
Ninakubali matumizi ya taarifa kwa utafiti wa baadaye
Sikubali

5. RIDHAA YA USHIRIKI WA UTAFITI MTANDAONI

Kwa kuthibitisha hapa chini, unathibitisha kwamba:

  1. Umesoma na kuelewa Hati ya Maelezo ya Ushiriki wa Utafiti.

  2. Unashiriki kwa hiari kwa madhumuni ya utafiti.

  3. Unaelewa haki yako ya kujiondoa wakati wowote bila madhara.

  4. Unaelewa mawasiliano ya mtafiti endapo una maswali ya kimaadili au haki zako.

Uamuzi wako:
Nakubali kushiriki katika utafiti
Sikubali kushiriki katika utafiti

6. TAARIFA MUHIMU

Mtafiti Mkuu: 김도환 (Dohwan Kim) – Korea University

Namba ya Simu: +82 10-8628-3233

Barua pepe: ulyclinic.research@gmail.com

Mtafiti: Sospeter Benjamin Mangwella

Namba ya simu: +82 10-9703-2057

bottom of page