top of page

Mwandishi:

Mhariri:

ULY CLINIC

Dkt. Mangwella S, MD

4 Septemba 2021, 14:33:29

Maumivu wakati wa kupitisha haja kubwa
shahawa-zenye-damu-ulyclinic-compressor.

Maumivu wakati wa kupitisha haja kubwa

Visababishi vya maumivu wakati wa kutoa hajakubwa ni;


  • Mpasuko kwenye njia ya haja kubwa

  • Bawasiri

  • Haja ngumu

  • Kuchomoza kwa puru

  • Kuhara

  • Michomo kinga kwenye matumbo (IBD)

  • Endometriosis

  • Kaswende au klamidia

  • Saratani ya puru

  • maambukizi ya kirusi cha HPV


Wakati gani wa kuonana na daktari kama una maumivu wakati wa haja kubwa?


Onana na daktari mara moja kwa uchunguzi wa kisababishi cha tatizo lako endapo unapata dalili zifuatazo;


  • Maumivu wakati wa kutoa haja kubwa yanayodumu zaidi ya wiki moja

  • Kutokwa na damu njia ya haja kubwa kunakodumu zaidi ya wiki moja

  • Kupatwa na homa au uchovu usio wa kawaida

  • Kutokwa na uchafu usio wa kawaida wakati unatoa haja kubwa

  • Maumivu wakati wa kushiriki ngono haswa endapo umepata mpenzi mpya au una wapenzi wengi

  • Maumivu makali ya kubana ya mgongo au tumbo

  • Kuonekana kwa uvimbe mpya kwenye njia ya haja kubwa


Mpasuko kwenye njia ya haja kubwa

Mpasuko huu unaweza kutokana na kupitisha kinyesi kigumu na mara nyingi huambatana na damu kidogo kwenye kinyesi.


Dalili

  • Kuonekana kwa mpasuko kwenye tundu la haja kubwa

  • Kuota kwa ngozi eneo lenye mpasuko

  • Maumivu makali kwenye njia ya haja kubwa wakati wa kupitisha kinyesi

  • Kupata damu kwenye kishu utakayotumia kufuta njia ya haja kubwa baada ya kumaliza haja

  • Muwasho njia ya haja kubwa

  • Hisia za kungua kwenye maeneo yanayozunguka njia ya haja kubwa


Mara nyingi mpasuko njia ya haja kubwa huwa hauhitaji matibabu na unaweza isha bila kupata matibabu.


Matibabu

Unaweza kufanya mambo kadhaa ili kupona haraka,


  • Kwanza kutumia dawa za kulainisha haja kubwa au kula chakula chenye nyuzinyuzi kwa wingi pamoja na maji ya kutosha

  • Pili, kalia maji ya uvuguvugu yenye detol kwa muda wa dakika 20 mara mbili kila siku kwa muda wa siku 5

  • Tatu, kama muwasho unaendelea unaweza kupaka dawa jamii ya hydrocortisone ili kuondoa muwasho na muchomo kutokana na maambukizi kwenye njia ya haja kubwa

  • Nne, kama maumivu yanaendelea, tumia dawa za kupaka kwa ajili ya kupunguza maumivu


Bawasili

Bawasili kwa jina jingine hutokana na kuvimba kwa mishipa ya damu ndani ya puruna njia ya haja kubwa, mara nyingi hutokana na kuongezeka kwa shinikizo kwenye mishipa ya maeneo haya.


Dalili

Dalili kuu ni ni maumivu wakati wa kutoa haja kubwa pamoja na;


  • Muwasho mkali na maumivu njia ya haja kubwa

  • Uvimbe kwenye njia ya haja kubwa unaouma na kuwasha

  • Kutokwa na majimaji njia ya haja kubwa

  • Kuona damu kwenye tishu unapojisafisha njia ya haja kubwa baada ya kumaliza haja kubwa


Matibabu ya nyumbani

Unaweza kujitibu bawasiri mwenyewe nyumbani kwa njia zifuatazo;


  • Kuoga maji ya uvuguvugu kwa muda wa dakika 10 kila siku ili kupuguza maumivu

  • Paka dawa za kuzuia muwasho na hisia za kuungua njia ya haja kubwa

  • Kula mlo wenye nyuzinyuzi kwa wingi kama mboga za majani, nafaka zisizokobolewa na vyakula vyenye majimaji kwa wingi.

  • Tumia dawa nyongeza za kuongeza nyuzinyuzi kwenye tumbo

  • Kalia maji ya uvuguvugu yaliyotiwa deto kwa muda wa dakika 20 mara mbili kwa siku

  • Safisha vema njia ya haja kubwa mara baada ya kujisaidia na wakati unaoga, tumia sabuni zisizo na marashi na safisha taratibu( soma zaidi njia za kiafya ya kusafisha njia ya haja kubwa)

  • Tumia tishu laini kama unapendelea kutumia tishu kujifuta njia ya haja kubwa baada ya haja

  • Kanda njia ya haja kubwa kwa barafu kama kuna uvimbe kwenye njia hiyo

  • Tumia dawa za kupaka kuzuia maumivu, muwasho kama ibuprofen, naproxen n.k


Kama hali bado inaendelea zaidi ya wiki mbili licha ya kufanya mambo yaliyoainishwa hapo juu, utapaswa kuonana na daktari kwa ushauri na tiba zaidi


Haja ngumu

Haja ngumu hufahamika pia kama konstipesheni hutokea endapo unapata shida kupitisha kinyesi kutokana na kinyesi kigumu au kutopata kinyesi chini ya mara tatu kwa wiki.


Dalili

Dalili kuu ni kupata maumivu wakati wa kupitisha kinyesi na zingine ambazo ni;


  • Kupata haja kubwa ngumu, iliyokauka na inayotoka kama golori au vipande vidogodogo vilivyoungana

  • Maumimu ya tumbo wakati wa kujisaidia

  • Hisia za kutaka kujisaidia mara baada ya kumaliza haja kubwa

  • Tumbo kujaa gesi kuuma

  • Maumivu nyumba ya mgongo wa chini

  • Hisia za kitu kimeziba utumbo


Matibabu ya nyumbani

Unaweza kujitibu nyumbani kwa kufanya mambo yafuatayo


  • Kunywa maji ya kutosha angalau glasinane kwa siku

  • Punguza kutumia kahawa na pombe

  • Kula vyakula vyenye nyuzinyuzi kwa wingi au kunywa vidonge vya nyuzinyuzi ili kulanisha haja kubwa

  • Kunywa maziwa mtindi

  • Punguza kula vyakula vinavyokausha haja kubwa kama vile kula nyama kila siku

  • Kufanya mazoezi angalau dakika 30 kwa siku kama kutembea, kuogelea kukimbia, kucheza mziki n.k

  • Jisaidia mara unapopata hamu ya kutoa haja kubwa

  • Tumia dawa za kulainisha njia utumbo baada ya kuongea na daktari wako


Kuchomoza kwa puru

Hutokea pale endapo kuta za ndnai ya njia ya hajakubwa zimechomoza nje kisha kupata michomo ya kingaya mwili. Ni dalili inayotokea sana kwa watu wenye maambukizi ya magonjwa ya zinaa, wanaopata matibabu ya saratani kwa mionzi, magonjwa ya michomo kwenye utumbo mfano vidonda vya kolaitiz n.k


Dalili

  • Dalili kuu ni maumivu wakati wa kupitisha haja kubwa pamoja na;

  • Kuharisha

  • Kutokwa damu wakati wa kujisaidia

  • Kutokwa na uteute kama kamasi njia ya haja kubwa

  • Hisia za kutaka kujisaidia haja kubwa mara baada ya kumaliza haja kubwa


Matibabu na kinga

  • Tumia kondomu wakati wa kufanya ngono ili kujikinga na magonjwa ya zinaa

  • Usifanye ngono ya njia ya haja kubwa

  • Usishiriki ngono na mtu mwenye vidonda au uvimbe maeneo ya siri

  • Kunywa antbayotiki au dawa za kupambana na virusi kutibu maambukizi ya bakteria na virusi kama unafikiria una magonjwa ya zinaa baada ya kuwasiliana na daktari wako

  • Kunywa dawa za kuzuia madhara ya matibabu ya mionzi kama mesalamine (Canasa) au metronidazole (Flagyl).

  • Tumia dawa za kulainisha utumbo zinazopatikana kwenye maduka ya dawa muhimu

  • Tumia dawa za kuzuia michomo ya kinga za mwili kwenye puru kama vile mesalamine (Canasa), prednisone (Rayos), infliximab (Remicade)

  • Pata matibabu ya upasuaji ili kuondoa sehemu ya haja kubwa iliyo na shida


Kuhara

Kuharisha hutokea pale endapo unapata choo kilani kama maji zaidi ya mara tatu kwa siku.


Dalili

Mara nyingi kuhara hakusabaishi upate hisia za maumivu njia ya haja kubwa hata hivyo unapopitisha haja kubwa na kujifuta mara nyingi zaidi hupelekea kuanza kupata maumivu wakati w akupitisha haja kubwa.


Unaweza kupata dalili za kuvimba kwa njia ya haja kubwa na michubuko


Dalili zingine ni

  • Kichefuchefu

  • Maumivu ya tumbo

  • Kuishiwa maji

  • Hisia za tumbo kujaa

  • Kupata damu kwenye kinyesi

  • Homa

  • Kupata kinyesi kikubwa


Matibabu na kinga

Matibabu kuhara huhusisha kurejesha kiwango cha maji kilichopotea kwa kunywa au kuwekewa kwenye mishipa. Kama kisababishi ni maambukizi, dawa za antibayotiki hutumika. Unaweza kufanya mambo yafuatayo kujikinga;


Nawa mikono kwa kutumia sabuni na maji safi kabla na baada ya kula

Safisha matunda na pika chakula kiive vema na kukila. Epuka kula masalia ya chakula kabla ya kupashwa.

Usitumie maji ya bomba ambayo hayajatiwa dawa ya kuua vimelea kunywa au kuosha matunda badala yake tumia maji ya kununua kwenye chupa


Michomo kinga kwenye matumbo (IBD)

Michomo kinga kwneye matumbo ni ugonjwa unaosababishwa na mwitikio wa kinga za mwili dhidi ya chembe hai za kuta za mfumo wa mmeng’enyo wa chakula. Magonjwa yaliyo kwenye kundi hili ni ugonjwa wa Crohn’s, asaletivu colaitiz, na ugonjwa wa sindromu kuchokozwa tumbo (IBD)


Dalili

  • Dalili kuu ya michomo kwenye matumbo ni maumivu wakati wa kujisaidia haja kubwa pamoja na;

  • Kuharisha

  • Hisia za kuishiwa nguvu

  • Maumivu au kutojihisi cema ndani ya tumbo

  • Kupoteza uzito bila sababu

  • Kupata kinyesi chenye damu

  • Kutojihisi njaa hata kama hujala muda mrefu


Matibabu

Mambo unayoweza kufanya ili kupunguza dalili za muchomo kinga kwenye matumbo


  • Tumia dawa za kuzuia michomo kama, mesalamine (Delzicol), olsalazine (Dipentum)

  • Dawa za kushusha kinga ya mwili kama azathioprine au methotrexate (Trexall)

  • Dawa za kudhibiti mwitikio wa mfumo wa kinga mwilini kama adalimumab (Humira) au natalizumab (Tysabri)

  • Dawa za kuzuia maambukizi kama vile metronidazole (Flagyl)

  • Dawa za kuzuia kuharisha kama vile methylcellulose (Citrucel) au loperamide (Imodium A-D)

  • Dawa za maumivu kama vile acetaminophen (Tylenol)

  • Dawa za kurejesha madini chuma mwilini

  • Vidonge vya calcium au vitamin D kuzuia hatari ya kuwa na mifupa dhaifu

  • Kufanyiwa upasuaji w akuondoa sehemu ya utumbo yenye shida

  • Kula vyakula vyenye maziwa kidogo, nyama kidogo, vyenye nyuzinyuzi kwa wastani na kuwa na kahawa au pombe kwa kiasi kidogo sana


Ugonjwa wa klamidia au kaswende

Magonjwa ya zinaa yanayosababishwa na chlamydia au kisonono huambukizwa kwa njia ya kujamiana. Mtu anaweza kupata magonjwa haya kwa kufanya ngono inayohusisha njia ya haja kubwa. Maambukizi ya kisonono na chlamydia husababisha puru kuvimba na kuwa na maumivu wakati wote au wakati wa kujisaidia


Dalili

Mbali na dalili ya kuvimba puru na maumivu wakati wa kupitisha haja kubwa dalili zingine ni pamoja na;


  • Hisia za kuungua njia ya haja kubwa

  • Maumivu ya kuungua wakati wa kukojoa

  • Kutokwa na uchafu sehemu za siri

  • Maumivu wakati wa kujamiana


Matibabu

  • Matumizi ya dawa za kutibu kaswende na chlamydia wewe na wote unaoshiriki nao ngono

  • Kuacha kushiriki ngono wakati unatumia dawa za kutibu magonjwa ya zinaa

  • Tumia kondomu wakati unashiriki ngono yoyote ile iwe ya mdomo, uume, uke na puru


Endometriosis

Endometriosis hutokea pale tishu zilizo ndani ya kizazi zimeota sehemu nyingine ya nje ya kizazi. Tishu hizo hufahamika kama endometriamu na huweza kujipandikiza kwenye utumbo mpana na hivyi kupelekea uchokozi wa utumbo huo na kutengeneza makovu kutokana na michomo. Uchokozi wa utumbo na michomo hupelekea dalili ya maumivu wakati wa kutoa haja kubwa.


Dalili

  • Mbali na maumivu wakati wa kutoa haja kubwa, dalili zingine zinazoweza kuonekana kwa mtu mwenye endometriosis ya utumbo mpana ni;

  • Maumivu ya tumbo kipindi cha hedhi

  • Maumivu ya kubana ya tumbo la chini na mgongo kipindi kifupi kabla ya kuanza kwa hedhi

  • Kuwa na hedhi nzito

  • Maumivu wakati wa kushiriki ngono au baada ya ngono

  • Ugumba


Matibabu

  • Matumizi ya dawa za maumivu kama ibuprofen

  • Matumizi ya gonadotropin-releasing hormone (GRNH) kudhibiti ukuaji wa tishu kwa kuzuia uzalishaji wa estrogen

  • Matumizi ya dawa za uzazi wa mpango jamii ya medroxyprogesterone

  • Tiba ya upasuaji wa mionzi kupunguza tishu zilizokua

  • Upasuaji wa kuondoa kizazi na mirija yake pamoja na ovari. Hufanyika kama tiba ya mwisho


Saratani ya puru

Ni nadra sana kwa saratani ya puru kuwa miongoni mwa sababu ya maumivu ya njia ya haja kubwa wakati wa kupitisha kinyesi licha ya kuweza kusababisha dalili hii.


Dalili

  • Mbali na dalili ya maumivu wakati wa kupitisha haja kubwa, dalili zingine ni

  • Kubadilika ghafla kwa umbile la kinyesi na rangi yake

  • Kupitisha kinyesi kidogo na chembemba

  • Damu kwenye kinyesi au tishu unayojifutia baada ya kumaliza haja kubwa

  • Kuota uvimbe mpya au usio wa kawaida unaouma unapoukandamiza

  • Muwasho maeneo ya kuzunguka njia ya haja kubwa

  • Kutokwa uchafu usio wa kawaida kwenye njia ya haja kubwa

  • Kuharisha mara kwa mara au kupata hajangumu

  • Kuishiwa nguvu

  • Tumbo kujaa gesi na kubeua

  • Kupungua uzito

  • Maumivu ya tumbo ya kudumu


Matibabu


Unapaswa kuonana na daktari kwa uchugnuzi na tiba endapo unapata dalili zilizoorodheshwa hapo juu kwa uchunguzi na tiba. Matibabu yanaweza kuhusisha;


Dawa za kuua chembe za saratani

Upasuaji wa kuondoa saratani na kuzuia kusambaa kwa saratani sehemu zingine za mwili

Matibabu ya mionzi


Maambukizi ya kirusi cha human papilloma (HPV)

Kirusi cha Human papilloma (HPV) huweza kusababisha sunzua kubwa maeneo karibu na njia ya haja kubwa, kwenye maeneo ya siri, mdomoni na kwenye koo. Sunzua kwenye njia ya haja kubwa zinaweza kuchokozwa na kinyesi hivyo kuleta dalili ya maumivu wakati wa kutoa haja kubwa.


Baadhi ya virusi vya HPV huweza kusababisha saratani kama usipopata matibabu. Unaweza kujikinga na maambukizi haya kwa;


  • Kupata chanjo ya kirusi

  • Kutumia kondomu wakati wa kushiriki ngono

  • Kufanya kipimo cha Pap smear kama unashiriki ngono mara kwa mara

ULY CLINIC inakushauri siku zote uwasiliane na daktari wako kwa ushauri na tiba zaidi kabla ya kuchukua hatua yoyote ile ya kiafya baada ya kusoma makala hii.

Wasiliana na daktari wa ulyclinic kwa ushauri zaidi na tiba kwa kutumia namba za simu au kubonyeza link ya Pata Tiba chini ya tovuti hii

Imeboreshwa, 

8 Oktoba 2021, 04:53:14

Soma dalili zingine Zaidi kwa kubonyeza herufi ya mwanzo hapa chini

​

[A] [B] [C] [D] [E] [F] [G] [H] [I] [J] [K] [L] [M] [N] [O] [P] [Q] [R] [S] [T] [U] [V] [W] [X] [Y] [Z] [Z] [#]

Rejea za mada

FDA approves expanded use of Gardasil 9 to include individuals 27 through 45 years old. fda.gov/NewsEvents/Newsroom/PressAnnouncements/ucm622715.htm. Imechukuliwa 04.09.2021

Cleveland clinic. Hemorrhoids. my.clevelandclinic.org/health/diseases/15120-hemorrhoids. Imechukuliwa 04.09.2021

CDC. Human papillomavirus (HPV) treatment and care. cdc.gov/std/hpv/treatment.htm. Imechukuliwa 04.09.2021

Mayo Clinic Staff. Anal fissure. mayoclinic.org/diseases-conditions/anal-fissure/symptoms-causes/syc-20351424. Imechukuliwa 04.09.2021

Mayo Clinic Staff. Constipation. mayoclinic.org/diseases-conditions/constipation/symptoms-causes/syc-20354253. Imechukuliwa 04.09.2021

NIH. Proctitis. niddk.nih.gov/health-information/digestive-diseases/proctitis. Imechukuliwa 04.09.2021

Cleveland clinic. Rectal bleeding. my.clevelandclinic.org/health/symptoms/14612-rectal-bleeding. Imechukuliwa 04.09.2021

Cancer gov. Regorafenib. cancer.gov/about-cancer/treatment/drugs/regorafenib?redirect=true. Imechukuliwa 04.09.2021

Mayo Clinic Q and A: Painful bowel movements may be due to anal fissure. newsnetwork.mayoclinic.org/discussion/mayo-clinic-q-and-a-painful-bowel-movements-may-be-due-to-anal-fissure/%0A/. Imechukuliwa 04.09.2021

CDC. What is inflammatory bowel disease (IBD)?. cdc.gov/ibd/what-is-IBD.htm. Imechukuliwa 04.09.2021

bottom of page