top of page

Mwandishi:

Dkt. Sospeter M, MD

Mhariri:

Dkt. Lugonda B, MD

13 Aprili 2020, 13:06:16

Dapsone

Dapsone

Ni dawa iliyo kwenye kundi la dawa za kutibu ukoma- (antileprosi), dawa hii hutumika kwa pamoja na rifampicin na clofazimine ili kutibu ukoma. Dawa hii inayojulikana kwa jina jingine la diaminodiphenyl sulfone, hupatikana katika mfumo wa kidonge na jeli ya kupaka, kidonge huwa na uzito wa 25mg au 100mg.


Jinsi Dapsone inavyofanya kazi


  • Humzuia bakteria kuzalisha foliki asidi. Foliki asidi ni muhimu sana kwenye seli ya bakteria kwani inahusika katika utengenezajiwa wa protini mbalimbali na Jinomu ya bakteria, inapozuia bakteria hushindwa kujizalia na wengine hufa.


  • Dawa hii hutumika kumlenga bakteria wa ukoma mwenye jina la mycobacterium leprae, lakini pia inaweza kutumika pamja na pyrimethamine kutibu malaria.


Kazi za dawa ya Dapsone


  • Hutumika kutibu ugonjwa wa Ngozi wa Demataitizi Hepatiformizi

  • Hutumiwa na dawa zingine kutibu ugonjwa wa ukoma

  • Hutumika kama kinga ya kuepusha kupata nimonia inayosababishwa na pneumocystis (karinii) Jiroveci

  • Hutumika kwa wagonjwa wenye kinga ya chini kuwalinda kutopata ugonjwa wa toksoplasmosisi.

  • Huweza kutumika kutibu malaria ikitumiwa Pamoja na pyrimethamine


Dawa usizopaswa kutumia pamoja na Dapsone


Dawa hii haipaswi kutumika pamoja na dawa zifuatazo :

  • Aluminum hydroxide

  • Apalutamide

  • Chanjo hai ya BCG

  • Calcium carbonate

  • Famotidine

  • Ibuprofen

  • Idelalisib

  • Ivosidenib

  • Lansoprazole

  • Mefloquine

  • Nefazodone

  • Sodium bicarbonate

  • Sodium citrate

  • Chanjo hai ya typhoid

  • Voxelotor


Tahadhari ya Dapsone kwa wagonjwa wafuatao;


  • Tahadhari ya dawa hii

  • Hupelekea kupungua kwa kiasi cha chembechembe nyeupe za damu

  • Chukua tahadhari unapomtibu mgonjwa mwenye mzio na kemikali ya sulphonamide.

  • Haipaswi kutumika kwa mgonjwa mwenye mzio na dawa hii


Matumizi ya Dapsone Kwa mama mjamzito na anayenyonyesha


Kwa mama mjamzito na anayenyonyesha

  • Inapaswa kutumika kwa tahadhari kwa mama mjamzito

  • Kwa mama anayenyonyesha haipaswi kutumika


Maudhi ya Dapsone


Baadhi ya maudhi madogo ya dawa hi ni pamoja na;

  • Agranyulosaitosisi

  • Upungua hamu ya kula

  • Kuvunjwa kwa chembe nyekundu za damu

  • Anemia ya hemolitiki

  • Maumivu ya kichwa

  • Madhaifu ya Ini

  • Haipoalbuminemia

  • Kukosa usingizi

  • Mzio wa lepra

  • Methaemoglobinemia

  • Kupoteza kazi mota

  • Kichefuchefu

  • Nyuropathi ya mfumo wa fahamu wa pembeni

  • Mzio mkali wa ngozi

  • Mapigo ya moyo kwenda haraka

  • Kutapika


Je endapo umesahau dozi ya Dapsone ufanyeje?


Endapo mgonjwa atasahau kutumia hii dozi anapaswa kuitumia pale atakapokumbuka

ONYO: Usitumie dawa yoyote bila ushauri wa daktari. Dawa zinaweza kuleta madhara mwilini na pia matumizi ya baadhi ya dawa pasipo ushauri na vipimo husababisha  vimelea kuwa sugu dhidi ya dawa hiyo.
ULY clinic inakushauri kuwasiliana na daktari wako unapotaka kuchukua maamuzi yoyote yanayohusu afya yako.
Wasiliana na daktari/Mfamasia wa ULY clinic kwa ushauri na Tiba au kuandikiwa dawa kwa kupiga simu au Kubonyeza Pata tiba chini ya tovuti hii.

Imeboreshwa,

3 Novemba 2021, 11:46:40

Rejea za mada hii:-

1.BNF 76,march September 2018 march 2019, ukurasa wa 566-567.dnf.org.

2.Web Md.Dapsone https://www.webmd.com/drugs/2/drug-6744/dapsone-oral/details. Imechukuliwa 13/4/2020


3.Medscape.Dapsone. https://reference.medscape.com/drug/aczone-dapsone-342559. Iimechukuliwa 13/4/2020

4.Drug Bank.Dapsone. https://www.drugbank.ca/drugs/DB00250. Imechukuliwa 13/4/2020

5.Ncbi.Dapsone. https://www.ncbi.nlm.nih.gov/pmc/articles/PMC3927068/. Imechukuliwa 13/4/2020
bottom of page