top of page

Mwandishi:

Dkt. Sospeter M, MD

Mhariri:

Dkt. Lugonda B, MD

19 Aprili 2020 11:15:06

Phenformin

Phenformin

Ni dawa ya kumeza iliyokuwa ukitumika katika matibabu kisukari aina ya pili ila kwa sasa imeondolewa sokoni kutokan ana madhara yake. Phenformin ipo kundi la dawa la Biguanide.


Majina ya kibiashara


  • Phenformin ilikuwa ikiuzwa kwa majina ya kibiashara kama

  • Bidiabe [+ Chlorpropamide]

  • Sanofi-Aventis, Italy

  • Gliben F [+ Glibenclamide]

  • Abiogen Pharma, Italy

  • Glinorboral [+ Glibenclamide]

  • Silanes, Mexico

  • Glinorboral Compuesto [+ Glibenclamide]

  • Silanes, Mexico; Silanes, El Salvador


Kwanini imeondolewa sokoni?


Phenformin imeondolewa sokoni toka mwana 1977 kutokana na madhara yake ya kusabababisha kifo kutokana na laktiki asidosisi. Laktiki asidosis ni hali inayotokea kama uzalishaji wa kemikali laktiki asidi ni mkubwa. Baadhi ya nchi bado zinatumia dawa hii.


Dawa kundi moja na Phenformin


Dawa zingine ambazo zipo kwenye kundi moja na Metformin ni zifuatazo;


  • Proguanil

  • Buformin

  • Chlorhexidine

  • Metformin

  • Chlorproguanil

  • Cycloguanil


Buformin kama ilivyo Phenformin ilizuiliwa kutumika pia miaka ya 1970.


Phenformin inavyofanya kazi


  • Hufanya kazi ya kupunguza kiasi cha sukari kinachotolewa na Ini kwenda kwenye damu.

  • Hupunguza ufyozwaji wa glukosi kwenye utumbo mdogo

  • Hufanya seli Beta za kongosho kuzalisha homoni ya insulin


Phenformin hutibu nini?


Phenformin ilikuwa ikitumika kwenye matibabu ya kisukari aina ya pili ambacho mara nyingi husababishw ana uzalishwaji wa mdogo wa insulin. Lakini kwa sasa haitumiki kutokana na athari zake za kusabababisha Laktiki Asidosisi.


Hutumika kutibu baadhi ya saratani kwa uwezo wake wa kuzuia ukuaji wa seli na ukuaji wa uvimbe kama saratani ya matiti, utumbo mpana na tezi dume.


Wagonjwa wasiopaswa kutumia Phenformin


Dawa hii haipaswi tumika kwa wagonjwa wenye;


  • Mzio na dawa hii

  • Moyo ulioferi

  • Dayabeetiki ketoasidosisi

  • Maambukizi makali kwenye fogo

  • Kulewa

  • Upumuaji wa shida


Angalizo


Tahadhari ya Phenformin


  • Utumiaji wa pombe na Phenformin huweza kupelekea hali mbaya ya laktiki asidosisi

  • Husababisha tezi ya adreno kushindwa kufanya kazi vizuri

  • Husababisha tezi pituitari kushindwa kufanya kazi zaidi

  • Huweza kuathiri ufyozwaji wa Vitamin B12


Phenformin kwa anayenyonyesha


Haipaswi kutumika kwa mama wajawazito na wamama wanaonyonyesha


Baadhi ya maudhi madogo ya Phenformin


  • Maumivu ya tumbo

  • Kichefuchefu

  • Kutapika

  • Kukosa hamu ya kula

  • Kuharisha kidogo

  • kuchoka

  • Kuongezeka kwenye damu kiwango cha laktiki asidi

ONYO: Usitumie dawa yoyote bila ushauri wa daktari. Dawa zinaweza kuleta madhara mwilini na pia matumizi ya baadhi ya dawa pasipo ushauri na vipimo husababisha  vimelea kuwa sugu dhidi ya dawa hiyo.
ULY clinic inakushauri kuwasiliana na daktari wako unapotaka kuchukua maamuzi yoyote yanayohusu afya yako.
Wasiliana na daktari/Mfamasia wa ULY clinic kwa ushauri na Tiba au kuandikiwa dawa kwa kupiga simu au Kubonyeza Pata tiba chini ya tovuti hii.

Imeboreshwa,

3 Novemba 2021 11:26:20

Rejea za mada hii:-

1.DrugBank.Phenformin.https://www.drugbank.ca/drugs/DB00914. Imechukuliwa 18/4/2020

2.ScienceDirect.Phenformin.https://www.sciencedirect.com/topics/neuroscience/phenformin. Imechukuliwa 18/4/2020

3.EBI.Phenformin.https://www.ebi.ac.uk/chebi/searchId.do?chebiId=8064. Imechukuliwa 18/4/2020

4.CayMan.Phenformin.https://www.caymanchem.com/product/14997/phenformin-(hydrochloride). Imechukuliwa 18/4/2020

5. Science direct. Biguanide Derivative. https://www.sciencedirect.com/topics/medicine-and-dentistry/biguanide-derivative. Imechukuliwa 18/4/2020
bottom of page