top of page

Mwandishi:

Dkt. Sospeter M, MD

Mhariri:

Dkt. Lugonda B, MD

29 Aprili 2020 09:00:45

Taspoglutide

Taspoglutide

Taspoglutide ni dawa mojawapo ya kutibu kisukari aina ya pili iliyo kwenye kundi la dawa linaloitwa Glucagon like peptide 1 Agonisti.


Majina ya kibiashara


Taspoglutide huwa maarufu kwa majina mengine ya kibiashara kama ipsen na roches.


Namna Taspoglutide inavyofanya kazi


Hufanya kazi kwa kuchochea kongosho kuzalisha homoni ya Insulin mara kiwango cha sukari kinapoongezeka kwenye damu.


Homoni ya Insulini husaidia seli za mwili kutumia na kuhifadhi sukari na hivyo kuiondoa kwenye dmau. Kufanya hivi kiwango cha sukari hupungua sana kwenye damu.


Dawa kundi moja na Taspoglutide


Dawa zingine zilizo kwenye kundi moja ni;


  • Exenatide

  • Lixisenatide

  • Semaglutide

  • Dulaglutide

  • Liraglutide


Taspoglutide hutibu nini?


Hutumika kudhibiti kiasi cha sukari kwa wagonjwa wa kisukari aina ya pili


Upekee wa Taspoglutide na dawa kundi GlP1 Agonisti


Sindano ya dawa hii huweza kuthibiti kiasi cha sukari mara mbili zaidi ya dawa zingine kwenye kundi hili

Dawa hii huleta maudhi mengi yasiyoelezeka katika mfumo wa chakula kama kichefuchefu na kutapika pamoja na mzio kwa watumiaji wengi


Mwingiliano wa Taspoglutide na dawa zingine


Dawa hii inapaswa kufuatiliwa kwa ukaribu inapotumika na dawa zifuatazo;


  • Acarbose

  • Aripiprazole

  • Asenapine

  • Atorvastatin

  • Cortisone

  • Darunavir

  • Desogestrel

  • Dexamethasone

  • Drospirenone

  • Enalapril

  • Eprosartan

  • Estradiol

  • Estropipate

  • Ethinylestradiol

  • Etonogestrel

  • Fludrocortisone

  • Fuphenazine

  • Fosamprenavir

  • Fosinopril

  • Glimepiridine

  • Glipizide

  • Glyburide


Wagonjwa wasiopaswa kutumia Taspoglutide


Dawa hii haipaswi kutumika kwa wagonjwa wafuatao:


  • Wagonjwa wenye aleji na dawa hiyo

  • Mwenye shida ya figo


Angalizo


Tahadhari ya Taspoglutide;


  • Sio mbadala wa Insulin

  • Haipaswi kutumika kwa mtu mwenye kisukari aina ya kwanza

  • Huweza kupelekea figo kushindwa kufanya kazi


Matumizi ya Taspoglutide kwa mama mjamzito na anayenyonyesha


Dawa hii haipaswi kutumika kwa mama mjamzito na mama anayenyonyesha


Maudhi ya Taspoglutide


Baadhi ya maudhi madogo ya taspoglutide


  • Kichefuchefu

  • Kuhara

  • Kutapika

  • Choo kuwa kigumu

  • Kuvimba sehemu iliyochomwa sindano

  • Maumivu ya kichwa

  • Kupunguza hamu ya kula

  • Kuchoka

  • Kizunguzungu

  • Maumivu ya tumbo


Je endapo utasahau dozi yako ufanyaje?


Kama umesahau kutumia dozi ya Taspoglutide, tumia mara pale utakapokumbuka. Kama muda wa dozi nyingine umekaribia sana usinywe mpaka muda utakapofika kasha endelea kwa muda uliopangiwa na daktari wako. Usinywe dozi mbili kwa wakati mmoja.

ONYO: Usitumie dawa yoyote bila ushauri wa daktari. Dawa zinaweza kuleta madhara mwilini na pia matumizi ya baadhi ya dawa pasipo ushauri na vipimo husababisha  vimelea kuwa sugu dhidi ya dawa hiyo.
ULY clinic inakushauri kuwasiliana na daktari wako unapotaka kuchukua maamuzi yoyote yanayohusu afya yako.
Wasiliana na daktari/Mfamasia wa ULY clinic kwa ushauri na Tiba au kuandikiwa dawa kwa kupiga simu au Kubonyeza Pata tiba chini ya tovuti hii.

Imeboreshwa,

3 Novemba 2021 11:22:44

Rejea za mada hii:-

bottom of page