top of page

Mwandishi:

Mhhariri

ULY CLINIC

Dkt. Mangwella S, MD

Jumanne, 6 Aprili 2021

Saratani ya damu (leukemia)

Saratani ya damu (leukemia)

Leukemia ni saratani ya damu inayoshambulia tishu zinazohusika kutengeneza damu ikiwa pamoja na urojo wa mifupa na mfumo wa limfatiki.


Leukemia mara nyingi huathiri chembe nyeupe za damu ambazo hupambana na maradhi mbalimbali. Kuathiriwa kwa chembe hizi hufanya mwili kushindwa kupambana na maradhi kutokana na kinga ya mwili kushuka baada ya shambulio hilo.


Vihatarishi


Vihatarishi vya saratani hii havijulikani lakini zipo sababu hatarishi zinazoweza kupelekea mtu kupata saratani hii ikiwa pamoja na:


  • Kupigwa na mionzi mikali: Mfano baada ya kupigwa bomu la nyuklia kule Japan,Ongezeko la wagonjwa wa saratani ya leukemia iliongezeka zaidi

  • Kemikali za sumu: Mfano kemikali inayoitwa Benzene ya inayotumiwa viwandani huweza kusababisha saratani hii Leukemia, uvutaji wa sigara na tumbaku humweka mtu hatarini kupata saratani ya AML

  • Virusi: Mfano kirusi cha Human T- Cell Lymphotropic Virus type 1-( HTLV-1) Epstein Bar Virus,pia kirusi cha UKIMWI huweza kusababisha saratani ya leukemia

  • Sababu za jini (vinasaba): Wanaume huathiriwa zaidi kuliko wanawake, pia watu wenye tatizo la sindromu ya Down?s huathiriwa Zaidi


Makundi ya saratani ya leukemia


  • Leukemia ya muda mfupi

  • Leukemia sugu

  • Leukemia ya muda mfupi


Leukemia hii inaambatana na kuongezeka zaidi kwa chembechembe za damu ambazo hazijakomaa katika damu. Chembe hizi huitwa blast. Blast hujizalisha kwa wiki sanga ana pia huwa hazina uwezo wa kufnaya majukumu yake ya kinga mwilini. Ugonjwa huhitaji kutibiwa hima ili kupambana nao


Saratani ya Leukemia ya muda mfupi pia imegawanyika kwenye makundi makuu mawili ambayo ni :


  • Leukemia ya muda mfupi ya Mayeloblastiki (AML)

  • Leukemia ya muda mfupi ya limphoblastiki (ALL)

  • Leukemia ya muda mfupi ya Mayeloblastiki (AML)


Leukemia ya muda mfupi ya Mayeloblastiki (AML): Hii ni aina ya saratani ambayo pana kuwepo seli nyingi za blasts kwenye damu. Seli hizi changa huwa hazina uwezo wa kufnaya kazi za kinga ya mwili. Kuwepo kwa seli hizi chanha husababisha matatizo mwilini na kuleta dalili mbalimbali.


Dalili za mgonjwa mwenye leukemia ya muda mfupi ya Mayeloblastik ni;


  • Kuvimba kwa ini

  • Kuvimba kwa Bandama

  • Kuvimba kwa fizi

  • Mwili kuchoka

  • Kupungua uzito

  • Kupata maambukizi ya magonjwa kurahisi

  • Matatizo ya damu kuganda

  • Kuishiwa damu mwilini


Leukemia ya muda mfupi ya limphoblastiki (ALL)

Leukemia ya muda mfupi ya Mayeloblastiki (AML): Hii ni aina ya saratani ambayo pana kuwepo seli nyingi za blasts kwenye damu. Seli hizi changa huwa hazina uwezo wa kufnaya kazi za kinga ya mwili. Kuwepo kwa seli hizi chanha husababisha matatizo mwilini na kuleta dalili mbalimbali.


Dalili za mgonjwa mwenye leukemia ya muda mfupi ya Mayeloblastik


  • Kuvimba kwa ini

  • Kuvimba kwa Bandama

  • Kuvimba kwa fizi

  • Mwili kuchoka

  • Kupungua uzito

  • Kupata maambukizi ya magonjwa kurahisi

  • Matatizo ya damu kuganda

  • Kuishiwa damu mwilini


Leukemia ya muda mfupi ya limfoblastiki (ALL)

Hii ni aina ya saratani ya damu ambayo damu inakuwa seli za limfoblasti kwa wingi kwenye damu kulinganisha na aina zingine za saratani.


Kuwepo kwa seli nyingi za limfoblasti hupunguza nafasi ya seli zingine za damu, hivyo mtu anakuwa na upungufu wa seli zingine za damu.


Dalili za mgonjwa mwenye leukemia ya muda mfupi ya limfoblastiki Leukemia


  • Maumivu ya misuli

  • Maumivu ya mifupa

  • Maumivu ya kichwa

  • Kuvimbwa kwa tezi za limfu

  • Kuvimba kwa korodani

  • Uvimbe kwenye mediastina

  • Kuvimba kwa ini

  • Kuvimba kwa bandama


Leukemia sugu

Sifa ya saratani hii ni kwamba chembe nyeupe za damu zinazozalishwa, nyingi huwa zimekomaa na zinaweza kufanya baadhi ya majukumu yake ya kinga mwilini. TSaratani hili hutokea taratibu sana na dalili zinaweza zisitambulike kwa haraka mpaka baada ya miaka kadhaa.


Leukemia sugu imegawanyika kwenye makundi makuu mawili:


  • Leukemia sugu ya myeloid (CML)

  • Leukemia sugu ya limfositiki (CLL)


Leukemia sugu ya myeloid (CML)

Hii ni aina ya saratani yenye sifa za utengenezwaji na uzalishwaji kwa wingi wa seli za myeloid, hali hii hupelekea kuvimba kwa bandama na kuwa na kiasi kikubwa cha chembe nyeupe za damu.


Asilimia 95 ya wagonjwa wa CML huwa na vinasaba visivyo vya kawaida na asilimia 25 ya wagonjwa huwa hawaonyeshi dalili zozote zile


Dalili za mgonjwa mwenye Leukemia sugu ya myeloid (CML)


  • Kuchoka sana kwa mwili kusiko na sababu

  • Kupungua uzito bila sababu

  • Kupata shida kupumua

  • Maumivu ya tumbo

  • Kukosa hamu ya kula

  • Kutokwa na jasho kwa wingi

  • Tumbo kujaa

  • Kupata michubuko kirahisi ya ngozi

  • Ini kuvimba

  • Bandama kuvimba


Saratani sugu ya limphositiki leukemia (CLL)

Saratani hii hutokea hasa kwa wagonjwa kati ya umri wa miaka 65 hadi 70 . Aina hii saratani hutokea kwa mwili kushindwa kukuthibiti ukuaji wa seli za B Limphosaiti hivyo hupelekea kinga ya mwili kushuka na utengenezwaji wa seli yeupe za damu kuwa mdogo.


Dalili


Dalili ya mgonjwa mwenye leukemia sugu ya limphositiki ni kama zifuatavyo:


  • Kupata maambukizi mara kwa mara na kwa urahisi kama vile homa ya mapafu- nimonia

  • Kushiba mapema kutokana na bandama kuwa kubwa

  • Kutokwa na damu kirahisi au kuumia kirahisi

  • Kuvilia kwa damu chini ya ngozi na hivyo kuleta madoa mekundu ya patekio

  • Mwili kuchoka sana

  • Homa za mara kwa mara

  • Jasho nyakati za usiku

  • Kupungua uzito


Matibabu


Kuna aina mbalimbali za matibabu ya saratani ya leukemia ambayo ni pamoja na;


Tiba ya dawa za Kemotherapi- kemotherapi ni msingi mkubwa wa matibabu ya saratani ya leukemia. Dawa hizi ni kemikali zinazotumika kuua chembe za saratani. Mfano wa dawa ni Vincristine, Methotrexate na Cyclophosphamide.


Kwa kutegemea aina ya saratani unaweza kutumia dozi moja au dozi yenye mchanganyiko wa dawa. Dawa hizi zinaweza kuwa kwenye mfumo wa tembe au dawa za maji kwa ajili ya kuchomwa kwenye mishipa ya damu.


Tiba baiologia

Tiba hii huamuru chembe za ulinzi wa mwili kupambana na chembe za saratani.


Tiba elekezi

Tiba hii hutumia dawa zinazoenda kuvamia hatua Fulani ya uzalishaji wa chembe za saratani. Mfano wa dawa ni imatinib.


Tiba mionzi

Mionzi ya Xray hutumika kuharibu chembe ambazo ni saratani na kusimamisha kuzaliana.


Kupandikizwa tishu za stem

Tishu za stem ni tishu za urojo wa mifupa, daktari atakufanyia atakuweka tishu mpya kwenye mifupa yako ili zizalishe chembechembe nyeupe za damu zisizo na saratani.


Kabla ya kuwekewa tishu za stem, utakuwa kwenye dozi kali ya kemotherapi au mionzi ili kuua chembe zinazozalisha saratani. Utawekewa kwenye mifupa yako tishu za stem kutoka kwako mwenyewe au kwa mtu mwingine.

ULY CLINIC inakushauri siku zote uwasiliane na daktari wako kwa ushauri na tiba kabla ya kuchukua hatua yoyote ya kitiba baada ya kusoma makala hii.

Wasiliana na daktari wa ulyclinic kwa ushauri zaidi na tiba kwa kubofya 'Pata Tiba,  au ''mawasiliano yetu' chini ya tovuti hii

Imeboreshwa,

26 Oktoba 2021 21:04:44

Rejea za mada hii:

1.Leukemia. Leukemia & Lymphoma Society. http://www.lls.org/resourcecenter/freeeducationmaterials/leukemia/understandingleukemia. Imechukuliwa 26.03.2020

2.Taking time: Support for people with cancer. National Cancer Institute. http://www.cancer.gov/publications/patient-education/taking-time. Imechukuliwa 26.03.2020

3.Davidson's Essentials of Medicine edited by J.Alaslair Innes Ukurasa wa 547-552

4.Long Cases in Clinical Medicine kimeandikwa na ABM Abdullah kurasa wa 633-638

5.What you need to know about leukemia. National Cancer Institute. http://www.cancer.gov/publications/patient-education/wyntk-leukemia. Imechukuliwa 26.03.2020

bottom of page