top of page

Tafiti  'Matumizi ya dawa pasipo ushauri wa daktari'

 

Habari ndugu mtumiaji wa tovuti ya ULY CLINIC

​

​

Matumizi yasiyo sahihi ya dawa jamii ya ‘antibiotic’ na ‘antifungal’ zinazotibu magonjwa mbalimbali kama kisonono, TB, UTI, tonses, nimonia, homa ya matumbo, fangasi ukeni n.k, husababisha vimelea kuwa sugu na kutotibika na dawa hizo. 

 

Tafiti nyingi zimefanyika kuangalia ukubwa wa tatizo la usugu wa vimelea vya maradhi kwenye dawa na zinaonyesha kuwepo na ongezeko la wimbi kubwa la usugu wa vimelea vya maradhi kwenye dawa za kutibu maambukizi ya bakteria na fangasi. Tatizo hili linaweza kudhuru watu wa umri wowote na taifa lolote lile na huongeza gharama kwa wagonjwa na kukaa hospitali kwa muda mrefu.

​

Lengo la tafiti hii ni kuangalia 'matumizi ya dawa mtandaoni bila ushauri wa daktari' tatizo linaloweza kupelekea kutokea kwa  'Usugu wa vimelea kwenye dawa'. Tafiti hii ni mahususi katika kukusanya taarifa zinazohusu 'Usugu wa vimelea kwenye dawa' na vitu vinavyochangia kusababisha matumizi ya dawa pasipo ushauri wa daktari. Kwa kujaza taarifa hizi utasaidia kuboresha utoaji wa huduma za afya na matumizi sahihi ya dawa. ULY clinic inazingatia sera yake ya usiri wa taarifa zako, pia haikusanyi taarifa kuhusu emaili wala jina lako.

​

​

Ombi: Tafadhari jaza taarifa sahihi na kwa uaminifu katika vyumba 11 vilivyo hapa chini. Asante kwa kushiriki.

1. Umri wako

2. Elimu yako

3. Nchi na Mkoa ulipo

4. Wilaya ulipo

5. Mara ngapi umetumia huduma za mtandaoni  kutafuta dawa kisha kujitibu mwenyewe katika kipindi cha miezi 12 iliyopita

6. Umeshapata madhara yoyote ya kutumia dawa bila ushauri wa daktari kutoka mtandaoni? Elezea tafadhari

7. Ni dawa aina gani umeshawahi tumia baada ya kuona mtandaoni bila kupata maelezo kutoka kwa daktari? Orodhesha dawa zote tafadhari

8. Ni mara ngapi katika kipindi cha miezi 12 iliyopita umetumia dawa kwa kuona imeandikwa tu mtandaoni bila ushauri wa daktari?

9. Orodhesha ugonjwa na dawa uliyotumia kutibu kutoka mtandaoni. mfano, tonses- amoxclav

10. Unafahamu madhara ya kutumia dawa bila ushauri wadaktari? Elezea tafadhari

11. Ni nini sababu ya kutowasiliana na daktari kabla ya kutumia dawa? Elezea tafadhari

Taarifa zako zimetumwa kikamilifu. Asante kwa kuchangia taarifa muhimu za afya

Kuna makosa yametokea katika ujazaji wa fomu yako. Tafadhari jaza upya

bottom of page