top of page
Mwandishi:
ULY CLINIC
Mhariri:
Dkt. Adolf S, MD

Dawa za kusafisha ulimi

5 Novemba 2021 09:50:51
Image-empty-state.png

Kusafisha ulimi kila baada ya kula kunaweza kukusaidia kuondoa uchavu pamoja na hatari ya magonjwa ya kinywa na harufu mbaya. Watu wengi wamekuwa wakisafisha ulimi kwa kutumia dawa za meno, lakini kuna dawa zingine ambazo zinaweza kutumika kusafisha kinywa chako na kukiweka katika hali nzuri ya kiafya.

​

Baadhi ya tafiti zinasema kwamba kusafisha ulimi kwa kutumia kifaa cha kukwangua ulimi au mswaki ni njia nzuri Zaidi ya kusafisha ulimi. Hata hivyo matumizi ya mswaki na dawa za kuosha kinywa pia husaidia mara nyingi kuweka kinywa chako safi;

​

Baadhi ya dawa za kusafisha ulimi ni pamoja na;

​

  • Unga wa baking soda- husafisha ulimi kwa kuondoa na kuua fangasi aina ya candida pamoja na bakteria streptococci

  • Chlorhexidine gluconate

ONYO: Usitumie dawa yoyote bila ushauri wa daktari. Dawa zinaweza kuleta madhara mwilini na pia matumizi ya baadhi ya dawa pasipo ushauri na vipimo husababisha  vimelea kuwa sugu dhidi ya dawa hiyo.
ULY clinic inakushauri kuwasiliana na daktari wako unapotaka kuchukua maamuzi yoyote yanayohusu afya yako.
Wasiliana na daktari/Mfamasia wa ULY clinic kwa ushauri na Tiba au kuandikiwa dawa kwa kupiga simu au Kubonyeza Pata tiba chini ya tovuti hii.
Imeboreshwa,
10 Julai 2023 10:16:39
bottom of page