Swali:
Je, inawezekana kutokwa na damu nyingi na ya mabonge bila maumivu yoyote na mimba kuendelea kuwepo?
Jibu:
Ndio
Njia ya kufahamu mimba imetoka kwa dalili
Kutokwa damu ya mabonge baada ya kutumia dawa ya kutoa mimba inaweza maanisha mimba imetoka au la. Mara nyingi mimba ikitoka damu yake huwa nyingi na kuambatana na maumivu ya tumbo yanayoweza kuwa ya kawaida au makali. Damu inayotoka huambatana na tishu za ujauzito au viungo vya mwili wa mtoto na hivi hutegemea mimba ilikuwa na umri gani.
Kwa mimba ya chini ya mwezi mmoja, kiasi cha damu kinachotoka huzidi kidogo damu ya hedhi na wakati mwigine huwa kama ya hedhi.
Je, unafahamu vipi mimba imetoka?
Njia pekee ya kufahamu mimba imetoka ni kwa kufanya kipimo cha ujauzito ambacho majibu yake huwa sahihi ukipima angalau wiki la pili toka umetoa mimba. Hii ni kwa sababu katika kipindi hiki, kiwango cha homoni ya jauzito(HCG) kwenye mkojo huwa kidogo kuweza kutambuliwa na kipimo na hivyo ukipima wakati huu mimba haitaonekana endapo imetoka. Inashauriwa kutumia mkono wa asubuhi unapoamka kwa kuwa huwa na kiwango kikunwa cha homoni hii endapo mimba ipo.
Njia zingine mbali na kipimo cha mkojo ya kufahamu kuwa mimba imetoka
Njia nyingine ya haraka inayoweza kutumika ni kwa kutumia kipimo cha picha mionzi sauti(ultrasound) ya kizazi. Kipimo hiki hutambua kama tishu za mimba zimeshatoka kwenye kuta za mji wa mimba au la. Licha ya kuwa kipimo kizuri kutambua mapema kuwa mimba imetoka au la, majibu ya kipimo hutegemea uwezo na uzoefu wa mpigaji picha kupiga na kutafsiri.
Wapi unaweza kupata maelezo zaidi?
Soma zaidi kwenye makala nyingine kuhusu kutoa mimba kwa dawa katika tovuti hii.