top of page

Mwandishi;

Mhariri:

Jaza jina na cheo cha mwandishi

Jumanne, 12 Januari 2021

Degedege kwa mtoto-Huduma ya kwanza
Degedege kwa mtoto-Huduma ya kwanza
Degedege kwa mtoto-Huduma ya kwanza
Degedege kwa mtoto-Huduma ya kwanza

Degedege kwa mtoto-Huduma ya kwanza

Malengo ya kutoa huduma ya kwanza kwa mgonjwa mwenye degedege ni kumlinda asipate madhara wakati degedege limetokea. Watu wengi hawafahamu mambo sahihi na yasiyo sahihi kuwafanyia waliopatwa na degedege kwenye eneo la tukio, kusoma makala hii itakusaidia kufahamu mambo hayo ya muhimu.


Degedege ni dalili inayoashiria mvurugiko katika mawasiliano ya umeme katika seli za ubongo

Hali hii huwapata watu wengi, inakadiriwa kuwa mtu mmoja kati ya kumi anaweza kupata degedege wakati wa maisha yake.


Mara nyingi degedege inapotokea kwa mtu hudumu kwa dakika chache bila kuleta madhara, na mara chache huweza kuwa dharura na kuhitaji msaada wa kitabibu wa haraka.


Kutokana na tatizo hili kujitokeza mara nyingi unashauriwa kujifunza namna ya kutoa huduma ya kwanza.


Namna ya kutoa huduma ya kwanza kwa mtu mzima mwenye degedege


Zifuatao ni njia za kumsaidia mtu mwenye aina yoyote ya degedege

  • Kaa nae, na kuwa mtulivu mpaka pale degedege litakapoisha, rekodi muda degedege lilipoanza na litakapoishia ili ufahamu limedumu kwa muda gani.

  • Muweke sehemu salama kwa kumtoa sehemu yenye hatari kama karibu na maji, moto n.k

  • Fahamu zitakaporejea, mueleze nini kilichotokea kwa ufupi na kumliwaza asijisikie vibaya

  • Mgeuze mwathirika wa degedege alalie ubavu mmoja (pozi la kupona kama ilivyo kwenye picha) kisha weka mto au kitu laini kichwani

  • Piga namba ya simu ya dharura kwa msaada zaidi kutoka kwa watoa huduma za dharura karibu nawe endapo degedege limedumu zaidi ya muda wa dakika 5


Huduma ya kwanza kwa mtu mwenye degedege linalohusisha mwili mzima


  • Kaa nae, na kuwa mtulivu mpaka pale degedege litakapoisha, rekodi muda degedege lilipoanza na litakapoishia ili ufahamu limedumu kwa muda gani.

  • Mgeuze alalie ubavu wa kushoto (pozi la kupona)

  • Weka kitu laini chini ya kichwa chake mfano nguo, mto nk

  • Legeza mavazi yanayobana shingo au ondoa kitu chochote katika shingo ili aweze kupumua vizuri

  • Piga namba ya simu ya dharura kwa msaada zaidi kutoka kwa watoa huduma za dharura karibu nawe endapo degedege limedumu zaidi ya muda wa dakika 5


Mambo yaliyo marufuku kumfanyia mwathirika wa degedege


Usifanye mambo yafuatayo ili kutomwatarisha au kujihatarishi usalama wako;


  • Kuzuia mijongeo ya misuli ya mwili kwa kumshikilia miguu au mikono

  • Kuweka kitu chochote katika mdomo wake, kufanya hivyo kutapelekea kuumiza meno au taya

  • Kumpa pumzi mdomo kwa mdomo

  • Kumpa chakula au kinywaji wakati wa degedege


Mambo unaweza mfanyia mtu anayepata degedege


Kumpatia dawa zake endapo ameandikiwa na daktari. Fanya hivi baada ya degedege kuisha na fahamu kurejea


Ni wakati gani degedege huwa dharura?


  • Degedege linalotokea kwa mara ya kwanza bila kuwa na historia ya degedege hapo awali

  • Mwathiriwa kushindwa kupumua

  • Kushindwa kuamka au kurejea kwa fahamu

  • Degedege linalodumu kwa zaidi ya dakika 5

  • Degedege kujirudia rudia

  • Degedege linatokea kwa watu wenye magonjwa mengine kama kisukari, magonjwa ya moyo

  • Dehedege linalotokea kwa mjamzito, mtu anayeumwa au mwenye jeraha

  • Degedege likitokea mgonjwa akiwa kwenye maji

ULY CLINIC inakukumbusha siku zote uwasiliane na daktari wako kwa elimu na ushauri zaidi kabla ya kuchukua thatua yoyote baada ya kusoma makala hii

Wasiliana na daktari wa ULY CLINIC kwa suhauri zaidi kupitia namba za simu au kwa kubonyeza 'Pata tiba'  chini ya tovuti hii

Imeboreshwa,

1 Oktoba 2021 08:12:19

Rejea za mada:

  1. First aid manual 10 chapisho la 10 kurasa namba 219, imeandikwa na kupitiwa na UK;S leading first aid providers

  2. Epilepsy foundation.Epilepsy. https://www.epilepsy.com/living-epilepsy/epilepsy-and/parents-and-caregivers/about-kids/seizure-first-aid. Imechukuliwa 11.01.2021

  3. Seizures – first aidhttps://www.childrens.health.qld.gov.au/fact-sheet-first-aid-for-seizures/. Imechukuliwa 11.01.2021

  4. Epilepsy - first aid and safety. https://www.betterhealth.vic.gov.au/health/ConditionsAndTreatments/epilepsy-first-aid-and-safety. Imechukuliwa 11.01.2021

  5. AJ Noble etal. ‘Seizure First Aid Training’ for people with epilepsy who attend emergency departments, and their family and friends: study protocol for intervention development and a pilot randomised controlled trial. https://www.ncbi.nlm.nih.gov/pmc/articles/PMC4521519/. Imechukuliwa 11.01.2021

  6. Pediatric in review. Seizure in children. https://pedsinreview.aappublications.org/content/41/7/321. Imechukuliwa 11.01.2021

bottom of page