top of page

Huduma ya kwanza

Katika sehemu hii utajifunza kuhusu huduma ya kwanza kwenye matukio mbalimbali ili uweze kuwa msaada pale itakapohitajika kabla wataalamu wa afya hawajafika kwenye tukio

Kifua kubana kwa mtoto: Huduma ya kwanza

Kifua kubana kwa mtoto: Huduma ya kwanza

Kifua kubana kwa mtoto kinaweza kusababishwa na kubana kwa njia za hewa kama kwenye pumu au bronkiolaitisi, au kutokana na matatizo ya moyo yanayosababisha upumuaji mgumu. Wazazi wanapaswa kutoa huduma ya kwanza kama kumketisha wima na kuhakikisha anapata hewa ya kutosha huku wakimkimbiza hospitali mara moja ili kubaini chanzo sahihi na kuanza matibabu haraka.

Huduma ya kwanza- Mtu mwenye maumivu ya chembe ya moyo

Huduma ya kwanza- Mtu mwenye maumivu ya chembe ya moyo

Huduma ya kwanza kwa maumivu ya chembe ya moyo ni kumpumzisha mgonjwa, kumpa maji kidogo, na kuepuka kumpa chakula kizito au dawa za maumivu. Ikiwa maumivu ni makali au yanaambatana na dalili hatarishi, mpeleke hospitali mara moja.

Maumivu ya koo huduma ya kwanza

Maumivu ya koo huduma ya kwanza

Kusukutua kwa maji yenye chumvu au magadi, kupumzisha koo, kulala muda wa kutosha na kuongeza unyevu kwenye koo ni baadhi ya mbinu za kupunguza maumivu ya koo.

Kutapika safarini: Huduma ya kwanza

Kutapika safarini: Huduma ya kwanza

Kutapika wakati wa kusafiri ni sindromu inayotokea mtu anapokuwa kwenye mwendo aina Fulani na mara nyingi huisha mara mwendo unaisha na hutokea sana wakati wa kusafiri.

Kumwagikiwa na kemikali machoni- Huduma ya kwanza

Kumwagikiwa na kemikali machoni- Huduma ya kwanza

Kumwagikiwa na kemikali kwenye macho inapaswa kuchukuliwa kama tukio la kupata matibabu ya dharura na endapo hatua zisipochukuliwa mapema, inaweza pelekea kuharibika kwa umbo la jicho/macho, matatizo ya uono, ukavu, presha na hata upofu wa macho. Ukubwa wa jeraha na athari zinazoweza kujitokeza hutegemea aina ya kemikali, kiwango kilichomwagikia na muda wa kemikali kuwa katika jicho/macho.

bottom of page