top of page

Mwandishi:

Mhariri:

Dkt. Benjamin S, MD

Dkt. Lugonda, MD

3 Novemba 2021 12:31:24

Kitanzi

ULY CLINIC inakushauri siku zote uwasiliane na daktari wako kabla ya kuchukua hatua yoyote ile ya kiafya baada ya kusoma makala hii

Wasiliana na daktari wa ULY CLINIC kwa ushauri na tiba kupitia namba za simu au kwa kubonyeza 'Pata tiba' chini ya tovuti hii

Imeboreshwa,

Tarehe mwezi na mwaka na saa

ULY clinic inakushauri siku zote ufuate ushauri wa daktari wako kabla ya kuchukua hatua yoyote ile baada ya kusoma makala hii.

Wasiliana na daktari wa ULY CLINIC kwa ushauri na tiba kupitia mawasiliano yetu.

Rejea za mada:

Vipandikizi vinavyowekwa chini ya ngozi kwa ajili ya kuzuia mimba vinaweza kuwa vya aina tofauti, aina hizi hutegemea homoni zilizowekwa kwenye vipandikizi hivyo, kuna aina mbili za homoni zinazowekwa kwenye vipandikiza ikiwemo homoni ya estrogen na progesterone

​

Kitanzi chini ya ngozi kinaweza kuwa kilicho tengenezwa na estrogeni tu, kilicho tengenezwa na progesterone tu au cha mchanganyiko wa progesterone na estrogen. Kila aina ya kitanzi kina kazi faida na madhara yake kwenye mwili wa binadamu

​

Sehemu hii tuzazungumzia aina hizi tofauti, kwanini unatumia aina Fulani, maudhi yanayoweza kutokea na namna ya kukabiliana nayo

​

Kitanzi cha progesterone tu

​

Kitanzi hiki huwekwa chini ya ngozi, sehemu ya ndani ya mkono chini kidogo ya kwapa kwa ajili ya kuzuia mimba kwa mda mrefu. Kitanzi hiki kinaweza kuwa na majina aina tofauti ya kibiashara kama implanon na nexplanon lakini vyote huwa na uwezo mzuri wa kuzuia mimba

​

Nani anatakiwa kutumia kitanzi hiki?

​

Kitanzi cha progesterone tu huweza kutumiwa na wanawake wengi, kuna baadhi ya magonjwa au hali huweza kumzuia mwanamke kutumia vipandikizi hiki mfano mwanamke mwenye saratani ya titi/chuchu, na mwanamke mwenye ugonjwa wa ini. Shirika la afya ulimwenguni limeweka utaratibu wa mwanamke yupi atumie vipandikizi vya progesterone tu.

​

Wanawake ambao wana hatari ya kupata mimba zisizotarajiwa, ikiwa pamoja na wasichana wadogo, wanawake waliotokwa na mimba, ni wanachama wa kutumia aina hii ya kitanzi kwa sababu wanahatari ya kuacha matumizi ya njia zingine za uzazi wa mpango. Kwa tafiti zilizofanyika imeonyesha kwamba wanawake chini ya umri wa miaka 20 wanapenda njia hii za uzazi wa mpango zinazoweza kuzuia mimba kwa mda mrefu.

​

Nani hatakiwi tumia njia hii?


  • Mwanamke mwenye mimba au au anayeshukiwa kuwa anamimba

  • Hitoria iliyopita au ya sasa ya kuganda kwa damu

  • Kuwa na Saratani ya ini au ugonjwa wa ini

  • Kutokwa na damu kwenye via vya uzazi

  • Kujulikana au kuhisiwa kuwa na saratani ya matiti

  • Mzio/aleji kwenye homoni hii

​

Kwa wanawake waliopata au walio na tatizo la damu kuganda wanatakiwa kutumia kitanzi chenye homon imchanganyiko wa estrogen na progesterone.

​

Faida ya kitanzi cha progesterone dhidi ya njia zingine zinazotumia progesterone tu

​

Njia zingine za uzazi wa mpango zinazotumia progesterone tu ni kama njia ya kitanzi cha kuwekwa ndani kuta za uzazi, vidonge vya uzazi wa mpango (levonorgestrel), na sindano ya depo.

​

Faida za kutumia dawa ni kwamba, haziitaji upasuaji wakati wa kuanza au kuacha njia hizo, huwa pia hazina estrogen, hasara zake ni hatari ya kutokwa na damu katikati ya mwezi, ambapo hutokea pia kwenye kitanzi cha ngozi, lakini haitokei kwenye kitanzicha kuwekwa ndani ya kuta za uzazi.

Faida zingine ni kwamba Kitanzi cha kuwekwa ndani ya kuta za uzazi na chini ya ngozi huwa havionekani, lakini uzi wa kitanzi ndani ya kuta za uzazi unaweza kuchomoza maeneo ya siri. Sindano ya uzazi wa mpango huwa inaficha siri sana kwa sababu hamna mtu anayeweza kujua kiurahisi kwamba unatumia njia ya uzazi wa mpango lakini hasara yake, huweza kusabaisha kupata damu kidogo sana ya hedhi.

​

Hufanyaje kazi kuzuia mimba?

​

Homoni ya progesterone hubadili mazingira ya kwenye uke, kwa kubadilisha ute usiwe rafiki kwa mbegu za kiume kupita, pia huweza kuzuia mayai kuzalishwa kutoka kwenye ovary endapo dozi kubwa itatumika. Ingawa homoni ya progesterone huzuia ukuta wa mimba kutokuwa rafiki kwa ajili ya kujipandikiza kwa mimba endapo mimba imetungishwa, kazi kubwa inayofanya ni kuzuia kutungishwa kwa mimba.

​

Muda wa kufanya kazi?

​

Kitanzi kinafanya kazi kulingana na mda ambao dawa hiyo itaisha, kuna vinavyofanya kazi kwa miaka mi tatu. Vipandikizi vya ndani ya kuta za uzazi huweza kuzuia mimba kwa miaka 5 hadi 10.

​

Maudhi au madhara yanayoweza kutokea ni

​

Mzio. Kwa baadhi ya wanawake wenye aleji/mzio na homoni hii kwenye ngozi, wakiwekewa kitanzichini ya ngozi, ngozi zao huwa nyekundu, kufanyika kwa uvimbe kutokana na kuvilia damu, kuvilia kwa damu chini ya ngozi, na maumivu

​

Maudhi mengine ni kama kuwashwa, kupata makovu wakati wa kuweka au kutoa kitanzi kwenye mfumo wa uzazi maudhi yanayoweza kutokea ni kama

​

Kubadilika kwa hedhi;

​

Wanawake wanaotumia vipandikizi wanaweza kuwa na kipindi kirefu au kifupi cha hedhi au kutotokwa na damu kabisa(amenolea). Maudhi makuu yanayotokea, kutokana na matumizi ya kitanzi cha progesterone tu huwa ni pamoja na, kutokwa na damu kwa kushitukiza, kutokwa na damu katikati ya mwezi ambapo hali hii inaweza isiishe au kupungua endapo mwanamke ataendelea kutumia kitanzi hicho. Dalili hizi zimelipotiiwa na asilimia 11 ya watumiaji wa njia hii.

​

Kushitukizwa kwa hedhi hutokea sana mwanzoni wa matumizi haswa katika miezi mitatu ya mwaka wa kwanza tangu kuwekewa kitanzi, kisha kutoweka na kuamka tena mwaka wa pili na watatu wa matumizi. Wanawake waliopata kutokwa na damu mara kwa mara wengi walisimama/acha kuendelea kutumia njia hii.

​

Matibabu ya kutokwa na damu bila ratiba si lazima, lakini kwa sababu kutokwa na damu husababisha mtumiaji kuona aache kutumia njia hiyo basi kuna njia za kuchukua ili kukabili tatizo hili. Njia hizo ni matumizi ya dawa za mda mfupi jamii ya NSAIDs,, matumizi ya dawa za kunywa zenye mchanganyiko wa homoni zote mbili, au kupewa homoni nyongeza ya estrogen.

Kujua Matibabu ya kutokwa na damu nyingi kusikotkubalika ongea na daktari wako.

​

Madhara katika Mifupa

​

Kitanzi cha progesterone tu haipelekei mifupa kupoteza uimara wake kwa kasi sana ukilinganisha na njia ya sindano ya depo

​​

Kitanzi chenye homoni ya estrogeni hupunguza kiwango cha homoni ya insulin kwenye damu inayochakatua sukari mwilini, pia hupunguza kiwango cha lehemu aina ya HDL na LDL. Madhara ya upungufu huu yameonekana kwa wanawake waliotumia kitanzi cha progesterone tu chini ya ngozi kwa mda wa miaka mitatu.

​

Maudhi mengineyo

​

Maudhi mengineyo ni kama Maumivu ya kichwa, kuongezeka kwa uzito, maumivu ya matiti, kutoeleweka kwa hali ya mtu, maumivu ya tumbo. Wanawake wanaotumia kitanzi hiki huongezeka uzito wa kilo tatu katika miezi 36 ya matumizi ya homoni ya progesterone tu haijalishi ni kitanzi cha ndani ya kuta za uzazi, dawa za kumeza au kitanzi chini ya ngozi

​

bottom of page