top of page
Bei ya Furosemide

Bei ya Furosemide

Furosemide ni dawa ya kundi la loop diuretics inayotumika kuongeza utolewaji wa mkojo ili kupunguza maji mengi mwilini. Hutumika sana kutibu shinikizo la damu, uvimbe (edema) unaosababishwa na magonjwa ya moyo, figo, au ini, na wakati mwingine kwenye dharura kama mapafu kujaa maji (pulmonari edema).


Fomu za kawaida za Furosemide


Furosemide vidonge (20 mg / 40 mg). Hutumika kwa wagonjwa wa nje na waliolazwa.Dozi hutegemea tatizo, mara nyingi 20–40 mg mara 1–2 kwa siku.


Bei:

  • MSD / Bohari ya dawa: takriban TZS 100–300 kwa kidonge

  • Famasi binafsi: takriban TZS 300–800 kwa kidonge


Furosemide ya sindano (Injection 20 mg / 40 mg)

Hutumika hospitalini, hasa kwenye dharura au kwa wagonjwa wasioweza kumeza dawa.


Bei:

  • MSD / Bohari ya dawa: takriban TZS 800–1,500 kwa ampoule

  • Hospitali binafsi: takriban TZS 2,000–4,000 kwa dozi (bila gharama ya huduma)


Kumbuka muhimu

  • Furosemide husababisha kukojoa mara kwa mara

  • Inaweza kupunguza kiwango cha potassium (potasium) mwilini

  • Haitakiwi kutumiwa bila ufuatiliaji wa mtaalamu wa afya

  • Wagonjwa wenye matatizo ya figo wanahitaji uangalizi maalum

  • Matumizi mabaya yanaweza kusababisha upungufu wa maji mwilini

Imeboreshwa:

15 Januari 2026, 08:32:08

bottom of page