top of page

Vikokotoo vya Afya

Vikokotoo vya Afya vya ULY Clinic vimeundwa kukusaidia kufanya maamuzi sahihi ya kiafya kwa kutumia taarifa sahihi, rahisi na za kitaalamu. Zana hizi hazichukui nafasi ya ushauri wa daktari, bali hukusaidia kuelewa hali yako kabla au baada ya kupata ushauri wa kitaalamu. Ili kutumia kikokotoo, bofya kichwa cha habari cha kikokotoo unachohitaji kisha kitafunguka na kukuelekeza namna ya kukitumia.

A. Vikokotoo vya Uzazi & Ujauzito

Vikokotoo hivi vinahusiana na mzunguko wa hedhi, rutuba, ujauzito na maendeleo ya mtoto tumboni.

Mzunguko wa Hedhi

Husaidia kufuatilia siku za hedhi, siku za rutuba na ovulesheni.

Siku ya Ovulesheni(Siku za hatari)

Hukokotoa siku ya ovulesheni na siku hatarishi za kushika mimba.

Umri wa Mimba

Hukokotoa wiki za ujauzito, kipindi cha sasa cha ujauzito na makadirio ya muda uliobakia.

Tarehe ya Kujifungua

Hukadiria tarehe ya kujifungua (EDD) kulingana na tarehe ya mwisho ya hedhi.

Ukuaji wa Mtoto Tumboni

Hutoa makadirio ya uzito, urefu na hatua ya maendeleo ya mtoto kwa wiki za ujauzito.

Siku salama na Hatari kwa ujauzito

Huhesabu siku za hatari (Dirisha la rutuba), siku za kati, na siku salama za mzunguko wa hedhi ili kusaidia kupanga mimba au kuepuka ujauzito.

Idadi ya siku za mzunguko wa hedhi

Kukokotoa urefu wa mzunguko wa hedhi

Umri wa Ujauzito: Wiki, Uzito wa Mtoto na Ushauri wa Lishe

programu ya inayosaidia mjamzito au mtoa huduma ya afya kukokotoa umri wa ujauzito  kwa kuzingatia tarehe ya kwanza ya kuanza kuona hedhi ya mwisho. Pia hutoa:

  • Makadirio ya tarehe ya kujifungua (EDD) kulingana na kanuni ya Naegele.

  • Makadirio ya uzito wa mtoto tumboni kulingana na wiki za ujauzito.

  • Ushauri wa lishe bora kwa mama mjamzito kulingana na hatua ya ujauzito.

  • Vitu vya kuepuka wakati wa ujauzito (pombe, sigara, dawa zisizo na ushauri wa daktari).

  • Dalili za hatari ambazo zinahitaji uangalizi wa haraka wa daktari.

  • Mchoro wa ukuaji wa mtoto kuonyesha mabadiliko ya uzito wa mtoto kwa wiki.

  • Onyo la dharura likitokea ishara zinazoweza kuhatarisha maisha ya mama au mtoto.

Shinikizo la damu kwa mjamzito

Kikokotoo cha Shinikizo la Damu kwa Mama hukokotoa thamani ya shinikizo la damu kulingana na viwango vya juu (sistoliki) na vya chini (dayastoliki) vinavyoingizwa na mtumiaji.

Lini ushike mimba kujifungua siku yako

Kikokotoo cha Tarehe ya Kushika Mimba hukusaidia kujua ni lini unapaswa kushika mimba ili kujifungua tarehe unayotaka, kulingana na mzunguko wako wa hedhi.

Kikokotoo cha Utabiri wa jinsia ya mtoto

Hiki ni kikokotoo cha makadirio kinachotumia dalili za mama pamoja na kalenda ya jinsia ya Kichina kubashiri uwezekano wa jinsia ya mtoto.

B. Vikokotoo vya Vipimo & Uchunguzi

Vikokotoo hivi vinasaidia kuelewa muda sahihi wa kufanya vipimo na tafsiri za awali za matokeo.

Kipimo cha Mimba

Hukokotoa muda sahihi wa kupima ujauzito (mkojo au damu) kulingana na mzunguko wa hedhi.

Kipimo cha Hatari ya kisukari

Kikokotoo hiki hukusaidia kutathmini uwezekano wako wa kuwa na kisukari au kuwa kwenye hatari ya kupata ugonjwa huu. Hatari ya kisukari huongezeka kutokana na umri mkubwa, uzito kupita kiasi, shinikizo la damu, historia ya familia na kiwango cha mazoezi unayofanya.

Kipimo cha mimba kwa mkojo baada ya Mimba kutoka/kutoa

Kikokotoo hiki kimeandaliwa ili kukupa elimu na mwongozo wa jumla kuhusu muda unaohitajika kwa homoni ya ujauzito (hCG) kupungua baada ya kutoa mimba—iwe kwa dawa, kusafishwa, au mimba imetoka yenyewe. Kikokotoo hiki hakitoi jibu la moja kwa moja kama una mimba au huna mimba, bali kinaeleza kama muda uliopita unaweza kuathiri matokeo ya kipimo chako.

C. Vikokotoo vya Lishe & Mwili

Vikokotoo hivi vitahusiana na afya ya mwili, uzito na lishe.

Uwiano wa uzito kwa urefu(BMI)

Uzito Unaofaa

Kikokotoo cha Mahitaji ya Kalori kwa siku

​Kikokotoo cha kalori (nishati) ni zana rahisi na yenye manufaa inayokusaidia kujua takriban kiasi cha kalori unazohitaji kula kila siku kulingana na taarifa zako binafsi. Kipimo hiki kinazingatia umri, jinsia, uzito, urefu, kiwango cha shughuli za mwili, na lengo lako la afya kama kupunguza, kudumisha, au kuongeza uzito.

Uwiano wa uzito na urefu (BMI) na mlo wa wiki

Huhesabu BMI (Uwiano wa uzito kwa urefu) ya mtu na kutoa mapendekezo ya mpango wa mlo wa wiki kulingana na matokeo.

D. Vikokotoo vya Afya ya Mwili

Vikokotoo hivi vinahusiana na kazi za mwili kwa ujumla, maji, mkojo, na mapigo ya moyo.

 

Kiwango cha Mapigo ya Moyo

Hukokotoa mapigo ya moyo salama kulingana na umri na shughuli.
 

Kiasi cha Maji ya Kunywa kwa Siku

 Hukokotoa kiasi kinachopendekezwa cha maji kwa siku (uzito, jinsia, hali ya hewa, shughuli).
 

Idadi ya Kwenda Haja Ndogo kwa Siku

 Hutathmini idadi inayotarajiwa ya haja ndogo kulingana na unywaji wa maji na afya ya kibofu.

 

Shinikizo la damu na ushauri wa chakula na mazoezi

Kutathmini hali ya shinikizo la damu kulingana na vipimo vya systolic na diastolic, na kutoa miongozo ya lishe na mazoezi kusaidia kudhibiti BP.

E. Vikokotoo vya dawa kwa watoto

Vinafanya kazi ya kukokotoa viwango sahihi vinavyohusiana na watoto. 

 

Dozi ya dawa kwa watoto

Hukadiria dozi sahihi za dawa kulingana na uzito wa mtoto.

F. Uwezekano wa kushika mimba

Hivi nivi ni vikokotoo vinavyoku

Uwezekano wa kushika mimba baada ya mimba kutoka/Kutolewa

Kikokotoo hiki kinakadiria uwezekano wa kushika mimba baada ya kutoa mimba.

Uwezekano wa kushika mimba baada ya tendo la ndoa

Kikokotoo hiki kinaweza kusaidia kukadiria uwezekano wa kushika mimba kulingana na tarehe ya kuanza kwa hedhi ya mwanamke, tarehe ya tendo la ndoa bila kinga, na urefu wa mzunguko wa hedhi.

bottom of page