top of page

Jinsi Huduma za Matibabu Mtandaoni za ULY CLINIC zinavyofanya Kazi

Huduma za matibabu mtandaoni za ULY Clinic zimeundwa kukupa ushauri na mwongozo wa kitabibu kwa usalama, weledi na kwa kuzingatia kanuni za afya. Ili kupata utambuzi sahihi na mwongozo wa matibabu, tunafuata hatua maalumu zinazolinda usalama wako, faragha yako, na ubora wa huduma.

 

1️⃣ Hatua ya Kwanza: Kujaza Fomu ya Historia ya Tatizo

Mgonjwa anapaswa kwanza kujaza fomu ya tatizo lake la kiafya (historia ya ugonjwa).
Kupitia fomu hii daktari hupata taarifa muhimu kama:

  • Dalili ulizonazo

  • Muda tatizo lilipoanza

  • Sababu zinazoweza kuchochea tatizo

  • Historia ya magonjwa mengine

  • Dawa unazotumia

  • Taarifa nyingine muhimu kiafya

 

Kurasa ya fomu za matibabu inapatikana hapa

🔴 MUHIMU:

Daktari hawezi kutambua tatizo lako bila kujaza dodoso hili. Hii ni sehemu ya utekelezaji wa SERA YA MATIBABU MTANDAONI, inayolenga kulinda afya yako na kukupa utambuzi sahihi.

 

2️⃣ Hatua ya Pili: Kukubaliana na SERA YA MATIBABU MTANDAONI

Kabla ya kuanza tiba, unatakiwa:

Kukubaliana na Sera Yetu ya Matibabu Mtandaoni

Sera hii inasema kwamba:

  • Hutapewa majibu ya tatizo lako, kipimo cha kufanya, dawa au dozi kabla daktari hajafahamu hali yako ya kiafya.

  • Daktari lazima apate taarifa zako kupitia fomu au majibu ya vipimo atakavyokuandikia.

  • Usalama na ubora wa tiba hutegemea taarifa sahihi utakazojaza.

Ikiwa unakubaliana na sera hii, unatakiwa kujibu maswali unayoulizwa na daktari kwa usahihi na ufasaha.

 

3️⃣Hatua ya Tatu: Kuchangia Huduma

Baada ya kujaza fomu, utaelekezwa kwenda kwenye ukurasa wa kuchangia huduma.

👉 Link ya namna ya kuchangia huduma:

Hapa unachagua kiwango cha mchango kulingana na huduma unayohitaji.

 

4️⃣Hatua ya Nne: Kutuma Uthibitisho wa Malipo

Baada ya kuchangia huduma, unatakiwa kutuma uthibitisho wa malipo kupitia kurasa ya kuchangia huduma.
Hii inamwezesha daktari kuendelea na hatua inayofuata ya uchunguzi na ushauri wa kitabibu.

 

5️⃣Hatua ya Tano: Kupokea Huduma ya Matibabu

Baada ya daktari kupokea:

✔️ Fomu ya historia ya tatizo
✔️ Uthibitisho wa malipo

 

Atakuuliza maswali ya ziada au kukuandikia vipimo kama vinahitajika. Baada ya hapo, utapokea:

  • Utambuzi wa tatizo lako

  • Ushauri wa vipimo vinavyohitajika

  • Mwongozo wa matibabu (ikiwa inapobidi)

  • Ufuatiliaji (follow-up)

 

Huduma inatolewa kwa weledi na kwa kuzingatia viwango vya kitaalamu.

Huduma Maalumu: Siku ya Matibabu bila Malipo

ULY Clinic inaamini katika kusaidia jamii, hasa wale wasio na uwezo.
Kwa hiyo tumeanzisha huduma maalumu:

 

Matibabu bila malipo kwa wateja wasio na uwezo

Kwa wagonjwa waliopata huduma kwa mara ya kwanza na wenye baadhi ya matatizo ya afya, tunatoa matibabu bila gharama siku ya Jumamosi au siku nyingine kama itakayotangazwa kupitia kundi maalumu  la whatsapp la ULYCLINIC:

🕛 Kuanzia saa 12 jioni (6:00 PM) – saa 4 usiku (10:00 PM)

  • Kwa wagonjwa wasio na uwezo wa kifedha

  • Kwa baadhi ya magonjwa tu (kulingana na mwongozo wa daktari)

  • Kwa wateja wapya wanaotibiwa kwa mara ya kwanza kupitia mfumo huu

NB: Kama huduma pasipo tiba zitatolewa mbali na jumamosi, huduma hizo zitatangazwa kupitia kundi la whatsapp la ULY CLINIC. Unaweza kujiunga kwa kubofya hapa.

Kwa nini tunafuata utaratibu huu?

  • Kulinda afya yako kwa kutoa huduma sahihi na salama

  • Kuzuia makosa ya kitabibu

  • Kuhakikisha tunatoa huduma bora kwa taarifa kamili

  • Kufanya matibabu ya mtandaoni kuwa salama kama matibabu ya ana kwa ana

bottom of page