
Bei ya Spironolactone
Spironolactone ni dawa ya kundi la dawa za kuongeza kukukoa pasipo kupoteza potassium inayotumika kwa:
Kupunguza maji mwilini (idima) kutokana na moyo kushindwa kufanya kazi, magonjwa ya ini au figo.
Kudhibiti presha ya damu kama sehemu ya mchanganyiko wa dawa.
Kupunguza dalili za homoni za androjeni kwa baadhi ya hali kama chunusi au kupoteza nywele(kuota upara) (kwenye ushauri maalum wa daktari).
Spironolactone huondoa maji mwilini bila kuondoa potassium nyingi, tofauti na dawa za kupunguza maji mwilini kwa kuongeza kukojoa (diuretiki) zingine.
Fomu ya kawaida za Spironolactone
Spironolactone vidonge (25 mg / 50 mg / 100 mg)
Hutumika kwa watu wazima na vijana kulingana na hali ya kiafya. Dozi ya kawaida: mara 1–2 kwa siku (kulingana na ushauri wa daktari).
Bei:
MSD / Bohari ya dawa: takriban TZS 300–800 kwa pakiti ya vidonge
Famasi binafsi: takriban TZS 800–2,000 kwa pakiti ya vidonge (kulingana na nguvu na chapa)
Kumbuka muhimu
Spironolactone hupunguza maji bila kusababisha upungufu mkubwa wa potassium, lakini bado inahitaji ufuatiliaji wa damu (kama mgonjwa ana matatizo ya figo au anatumia dawa zingine za presha).
Inaweza kusababisha maumivu ya tumbo, kichwa, au mabadiliko ya mzunguko wa damu mwanzoni mwa matibabu.
Si dawa ya lazima kwa wajawazito bila ushauri wa daktari.
Usitumie bila ushauri wa mtaalamu wa afya; kutumia vibaya kunaweza kusababisha hyperkalemia (potassium juu sana).
Imeboreshwa:
15 Januari 2026, 09:15:06
