top of page

Mwandishi:

Mhariri:

ULY CLINIC

Dkt. Peter A, MD

18 Aprili 2020 10:09:49

Kutapika
shahawa-zenye-damu-ulyclinic-compressor.

Kutapika

Kutapika ni kitendo cha kutoa nje ya mwili chakula au maji maji yaliyo tumboni kupitia mdomo, kitendo hiki hufanyika kwa haraka na huweza ambatana na maumivu katikati ya kifua.


Kutapika hufanyika kwa haraka na huambatana na maumivu makali au kiasi na hutanguliwa na kichefuchefu.


Kutapika ni moja kati ya njia za ulinzi wa tumbo na mwili dhidi ya sumu, hata hivyo huwa ni ishara ya hali au ugonjwa Fulani ulio mwilini. Wakati mwingine kutapika kunaweza kusiwe kunasababishwa na sababu ya hatari au kukawa na sababu ya hatari mwilini inayohitaji matibabu.


Matumizi ya dawa za kuzuia kutapika mara nyingi huwa haishauriwi kitaalmau, hii ni kwa sababu hupinga juhudi asili za kinga ya mwili kuondoa sumu mwilini. Hata hivyo baadhi ya hali na magonjwa husababisha kutapika kupita kiasi ambapo utahitaji uangalizi wa karibu wa daktari wako na matumizi ya dawa kuzuia kutapika. Usitumie dawa za kuzuia kutapika bila ushauri kutoka kwa daktari wako.


Dalili


Dalili ambazo huweza ambatana na kutapika


  • Maumivu ya tumbo

  • Kuharisha

  • Homa

  • Mapigo ya moyo kwenda kasi

  • Kutokwa na jasho

  • Kukauka kwa midomo

  • Kupungua kwa mkojo na kukojoa

  • Maumivu ya kifua

  • Kuzimia

  • Kuchanganyikiwa

  • Kulala sana

  • Kuishiwa nguvu

  • Kutapika damu


Visababishi


  • Hatua za awali za ujauzito

  • Msongo wa mawazo na hofu

  • Magonjwa ya figo

  • Kula sumu kwenye chakula

  • Maambukizi ya bakteria tumboni

  • Kula kupita kiasi

  • Mzio kutokana na harufu ya chakula au kitu chenye harufu

  • Shambulio la moyo

  • Jeraha kwenye ubongo

  • Uvimbe kwenye ubongo

  • Baadhi ya saratani

  • Kula sumu au pombe kupita kiasi

  • Homa ya safari

  • Matumizi ya baadhi ya dawa zenye maudhi ya kutapika

  • Matibabu ya kikemikali au mionzi mikali


Visabaishi vingine

  • Mzio wa anafailaksisi

  • Anoreksia nevosa

  • Ugonjwa wa apendeksi

  • Vetaigo

  • Bulimia nevosa

  • Sindromu ya kutapika

  • Msoongo wa mawazo

  • Kizunguzungu

  • Dayabekiti ketoasidosisi

  • Maambukizi ya sikio

  • Kukua kwa bandama(splenomegali)

  • Homa

  • Mawe kwenye kibofu cha nyongo

  • Kunywa sumu

  • Kucheua kwa tindikali za tumboni- GERD

  • Kuferi kwa moyo

  • Henia ya hayato

  • Kichwa maji(haidrosefalasi)

  • Haipathairoidizimu na haipothairoidizimu

  • Haipoparathairoidizimu

  • Isikemia ya utumbo

  • Kuziba kwa utumbo

  • Mvilio wa damu ndani ya fuvu la kichwa

  • Sindromu ya iritabo baweli

  • Intusasepsheni

  • Matumizi ya dawa za aspirini, NSAIDS, dawa za uzazi wa mpango, Digitalizi nakotiksi na antibayotiki

  • Ugonjwa wa menierezi

  • Meninjaitizi

  • Aleji kwenye maziwa

  • Saratani ya kongosho

  • Vidonda vya tumbo

  • Pancreataitisi

  • Stenosisi ya pairoriki

  • Saratani kwenye ubongo

  • Tiba mionzi

  • Sumu kwenye Ini


Wakati gani uonane na daktari haraka unapokuwa unatapika?

Unapaswa kumuona Daktari endapo utaona dalili zifuatazo;


  • Kutapika damu

  • Kuchanganyikiwa

  • Kichwa kuuma sana

  • Kupumua kwa kasi

  • Mapigo ya moyo kwenda mbio

  • Kuharisha sana


Matibabu


Matibabu ya kutapika hutegemea kisababishi, Mara nyingi kama dalili ya kutapika sababu yake haijulikani ni bora kutoitibu hii dalili ili kumsaidia daktarin kujua ni ugonjwa gani unapelekea dalili hii, kutumia dawa za kuzuia kutapika huficha ugonjwa.


Mgojwa anayetapika huweza kupatiwa matibabu ambayo ni;


  • Kuongezewa maji kupitia mishiopa ya damu

  • Kupewa dawa ya kuzuia kutapika kama kisababishi kinakulikana, Mfano kwa wa mama wajawazito.

  • Soma Zaidi kuhusu dawa za kuzuia kutapika katika Makala zetu hapa ULY CLINIC.

ULY CLINIC inakushauri siku zote uwasiliane na daktari wako kwa ushauri na tiba zaidi kabla ya kuchukua hatua yoyote ile ya kiafya baada ya kusoma makala hii.

Wasiliana na daktari wa ulyclinic kwa ushauri zaidi na tiba kwa kutumia namba za simu au kubonyeza link ya Pata Tiba chini ya tovuti hii

Imeboreshwa, 

19 Julai 2023 20:02:52

Soma dalili zingine Zaidi kwa kubonyeza herufi ya mwanzo hapa chini

​

[A] [B] [C] [D] [E] [F] [G] [H] [I] [J] [K] [L] [M] [N] [O] [P] [Q] [R] [S] [T] [U] [V] [W] [X] [Y] [Z] [Z] [#]

Rejea za mada

1.Di Lorenzo C. Approach to the infant or child with nausea and vomiting. http://www.uptodate.com/home. Imechukuliwa 17/4/2020

2.Longstreth GF. Approach to the adult with nausea and vomiting. http://www.uptodate.com/home. Imechukuliwa 17/4/2020

3.Nausea and vomiting. Merck Manual Professional Version. http://www.merckmanuals.com/professional/gastrointestinal-disorders/symptoms-of-gi-disorders/nausea-and-vomiting. Imechukuliwa 17/4/2020

4.Longo DL, et al., eds. Nausea, vomiting and indigestion. In: Harrison's Principles of Internal Medicine. 19th ed. New York, N.Y.: McGraw-Hill Education; 2015. http://accessmedicine.com. Imechukuliwa 17/4/2020

5.WebMd.Vomiting.https://www.webmd.com/digestive-disorders/digestive-diseases-nausea-vomiting. Imechukuliwa 17/4/2020

6.EveryDayHealth.Vomiting.https://www.everydayhealth.com/vomiting/guide/. Imechukuliwa 17/4/2020

7.HealthLine.Vomiting.https://www.healthline.com/health/nausea-and-vomiting. Imechukuliwa 17/4/2020

8.MedcineNet.Vomiting.https://www.medicinenet.com/vomiting/symptoms.htm. Imechukuliwa 17/4/2020

bottom of page