top of page

Mwandishi:

Mhariri:

ULY CLINIC

Dkt. Benjamin L/ MD

5 Julai 2021 20:44:44

Maumivu ya tumbo baada ya kutoa mimba
shahawa-zenye-damu-ulyclinic-compressor.

Maumivu ya tumbo baada ya kutoa mimba

Maumivu ya tumbo baada ya kutoa mimba kwa kutumia dawa au kwa upasuaji ni hali ya kawaida kutokea haswa wiki chache baada ya kutoa mimba. Kwa kawaida, kwa waliotoa mimba kwa njia ya dawa, maumivu ya tumbo huwa makali masaa matatu hadi matano baada ya kutumia dawa na hufuatiwa na kutokwa na damu nyingi ukeni.


Mara baada ya damu kuanza kutoka maumivu ya tumbo huongezeka kiasi na kuanza kupungua kwa na hivyo damu inayotoka hupungua pia mpaka pale ukuta uliojipandikiza ndani ya kizazi uweze kutoka. Muda wa damu kutoka pia na kiasi cha maumivu ya tumbo kwa aliyetoa mimba kwa njia ya dawa, hutegemea umri wa ujauzito. Endapo ujauzito una wiki mbili hadi nne, damu inayotoka huzidi kidogo ile ya hedhi na huweza toka kwa siku 5 hadi 8 kisha kukata, baadhi ya wanawake wanaweza endelea ona damu mpaka wiki mbili lakini hutoka kidogo sana. Wakati huu ni muhimu kutumia dawa au vidonge vya kuongeza damu ili kuepuka upungufu wa damu.


Madhara makubwa yanayotishia uhai kutokana na kutoa mimba pasipo utaalamu, sehemu isiyofaa na mtoa huduma asiyefahamu huhatarisha afya na uhai wa anayetolewa mimba. Hata hivyo madhara yanaweza toke hata kama mimba inatolewa na mtaalamu mzoefu katika mazingira salama lakini huwa rahisi kurekebishwa haraka.


Makala hii imeelezea kuhusu maumivu ya tumbo baada ya kutoa mimba kwa dawa, kusoma kuhusu maumivu ya tumbo baada ya kutoa mimba kwa kusafishwa kizazi, soma Makala yake sehemu nyingine katika tovuti ya ULY CLINIC.


Ni kwa muda gani maumivu ya tumbo hudumu baada ya kutoa mimba kwa dawa?

Kwa kawaida maumivu ya tumbo baada ya kutoa mimba chini ya wiki nne kwa dawa hudumu kwa muda wa wiki moja, wiki la pili maumivu hubakia kidogo na huisha. Damu kutoka nyingi huisha wiki la kwanza na wiki linalofuatia hutoka kidogo kisha hukata


Nini husababisha maumivu ya tumbo baada ya kutoa mimba?


Endapo maumivu ya tumbo yanadumu kwa zaidi ya wiki 2 baada ya kutoa mimba kwa dawa, siku zote humaanisha, kuendelea kwa ujauzito, mimba kutoka nusu na maambukizi ndani ya mfuko wa uzazi.


Kuendelea kwa ujauzito baada ya kujaribu kutoa mimba kwa dawa

Ujauzito unaweza kuwa unaendelea kwa kwa sababu haujatoka, mimba imetungwa nje ya mfuko wa kizazi au kuwa na mimba zaidi ya moja. Endapo ujauzito unaendelea, yaani haujatoka vema, mara nyingi dalili zake huwa kuendelea kutoka kwa damu ukeni na maumivu ya tumbo zaidi ya siku 7 hadi 8. Ili kuweza kutibu mimba inayoendelea, inapaswa kufika hospitali ili kusafishwa kizazi.


Kubakia kwa mabaki ya mimba


Mimba iliyotoka nusu huambatana na dalili za maumivu ya tumbo na kutokwa na damu. mimba kutoka nusu kutokana na matumizi ya dawa hutibiwa kwa njia ya dawa au kusafisha kwa kufyonza mabaki endapo ujauzito upo chini ya wiki 13, na kwa njia ya kukwangua kizazi endapo ujauzito ni zaidi ya wiki 13. Uchaguzi wa matibabu hata hivyo hutegemea hali ya mama na uchaguzi wake pia baada ya kuelezewa aina za matibabu yaliyopo.


Maambukizi ndani ya uzazi


Maambukizi ndani ya kizazi baada ya kutoa mimba kwa dawa mara nyingi husababisha na bakteria wanaoishi ukeni pamoja na bakteria wa magonjwa ya zinaa endapo kabla ya kutoa mimba walikuwepo ukeni ambao ni;


  • Chlamydia trachomatis

  • Neisseria gonorrhea

  • Trichomonas vaginalis

  • Vajinosisi ya bakteria

  • Streptococcus kundi B

  • Escherichia coli

  • Staphylococcus aureus

  • Bacteroides fragilis na

  • Peptostreptococcus


Dalili


  • Maumivu ya tumbo ukiwa umetulia au likishikwa

  • Maumivu ya tumbo la chini ya kunyonga

  • Kutokwa na uchafu ukeni usio wa kawaida

  • Kichefuchefu

  • Kutapika

  • Kuharisha

  • Homa (inaweza kutokea mapema au kuchelewa tokea)

  • Kutetemeka mwili


Maambukizi kwenye kizazi baada ya kutoa mimba mara nyingi hutibiwa kwa dawa za mishipa kisha kuendelea na dawa za kunywa. Hatari ya kupata maambukizi huongezeka endapo mimba imetolewa kwa njia zisizo salama au matendo mbalimbali hatarishi. Soma Makala ya maambukizi ndani ya kizazi baada ya kutoa mimba kwenye Makala nyingine ndani ya tovuti hii ya ULYCLINIC.


Vipimo


Nini utafanyiwa utakapofika hospitali?


Utakapofika hospitali, daktari atachukua historia ya tatizo lako kwa kukuuliza maswali mbalimbali na kufanya uchuguzi wat umbo na uke kisha endapo atatambua tatizo utafnayiwa matibabu. Endapo hajaweza tambua au anataka kuthibitisha au kutofautisha matatizo aliyoyaona kucnagia au kutochangia. Mfano itamwezesha kufahamu kama bado una mimba na au ipo wapi. Vipimo ambavyo huagizwa sana kufanyika ni;


  • Kipimo cha utrosound ya via vya uzazi

  • Kipimo cha picha nzima ya damu ( FBP)

  • Kipimo cha beta- HCG

  • Vipimo vya magonjwa ya zinaa


Nini cha kufanya endapo unapata maumivu ya tumbo baada ya kutoa mimba kwa dawa?


Endapo unapata maumivu ya tumbo baada ya kutoa mimba kwa dawa, fanya mambo yafuatayo;


  • Tumia dawa za kupunguza maumivu jamii ya NSAIDS kama ibrupofen, au jamii ya Opioid kama Tramadol( dawa hizi husababisha kichefuchefu, kulewesha na maumivu ya tumbo)

  • Jikande tumbo la chini kwa muda wa dakika 15 hadi 20mara nyingi uwezavyo kwa maji ya moto kwenye chupa lakini tanguliza kitambaa kuepuka kuungua tumbo. Unaweza tumia chupa maalumu za kukanda tumbo la uzazi zinazopatikana madukani


Wakati gani wa kuonana na daktari?


Onana na daktari mara moja kwa ushauri na matibabu endapo una dalili zifuatazo;


  • Unapata maumivu makali yasiyozuilika kwa dawa za maumivu jamii ya NSAIDS

  • Unatokwa na damu nyingi inayolowanisha pedi kubwa zaidi ya mbili ndai ya masaa mawili

  • Unapata maumivu ya tumbo ambayo hayaishi kwa njia ya kupumzika, au kukanda tumbo na maji ya moto

  • Unapata homa zaidi ya nyuzijoto 38 za selishazi

  • Unatokwa na uchafu au ute ukeni wenye rangi isiyo ya kawaida ( mfano njano) na wenye harufu mbaya

  • Hutokwi na damu zaidi ya masaa 24 toka umetumia dawa za kutoa mimba


Wapi unapata taarifa zaidi?


Pata taaria zaidi kuhusu ujauzito, njia za uzazi wa mpango na kwenye makala zingine za ULY CLINIC kupitia linki ya nyumbani.

ULY CLINIC inakushauri siku zote uwasiliane na daktari wako kwa ushauri na tiba zaidi kabla ya kuchukua hatua yoyote ile ya kiafya baada ya kusoma makala hii.

Wasiliana na daktari wa ulyclinic kwa ushauri zaidi na tiba kwa kutumia namba za simu au kubonyeza link ya Pata Tiba chini ya tovuti hii

Imeboreshwa, 

8 Oktoba 2021 04:53:19

Soma dalili zingine Zaidi kwa kubonyeza herufi ya mwanzo hapa chini

​

[A] [B] [C] [D] [E] [F] [G] [H] [I] [J] [K] [L] [M] [N] [O] [P] [Q] [R] [S] [T] [U] [V] [W] [X] [Y] [Z] [Z] [#]

Rejea za mada

1. Clinical Practice Handbook for Safe Abortion. https://www.ncbi.nlm.nih.gov/books/NBK190099/. Imechukuliwa 05.07.2021

2. Karima R. Sajadi-Ernazarova, et al. Abortion Complications. https://www.ncbi.nlm.nih.gov/books/NBK430793/. Imechukuliwa 05.07.2021

3. Isabelle Carlsson, et al. https://bmcwomenshealth.biomedcentral.com/articles/10.1186/s12905-018-0645-6. Imechukuliwa 05.07.2021

4. Michelle H. Orlowski, DO, et al. Management of Postabortion Complications for the Emergency Medicine Clinician. https://www.annemergmed.com/article/S0196-0644(20)30747-2/fulltext. Imechukuliwa 05.07.2021

bottom of page