top of page

Dalili na viashiria vya magonjwa mbalimbali

ULY Clinic inakushauri kufuata ushauri wa daktari wako kabla ya kuchukua hatua yoyote ile baada ya kusoma makala. Bofya picha au neno soma zaidi ili kuingia kwenye makala kwa undani.

Maumivu ya tumbo la juu kulia

Maumivu ya tumbo la juu kulia

Miongoni mwa visabahishi ni vidonda vya tumbo, homa ya kongosho, homa ya ini na magonjwa ya mfumo wa damu na upumuaji. Baadhi ya visababishi huweza kupelekea mtu kupoteza maisha hivyo wasiliana na daktari upatapo dalili hii.

Maumivu ya tumbo la juu kushoto

Maumivu ya tumbo la juu kushoto

Visababishi huweza kuwa vidonda vya tumbo, homa ya tumbo na tezi kongosho. Baadhi ya visababishi huweza kupelekea mtu kupoteza maisha hivyo wasiliana na daktari upatapo dalili hii.

Maumivu ya tumbo la juu ya kitovu

Maumivu ya tumbo la juu ya kitovu

Maumivu ya tumbo la juu ya kitovu yanaweza kusababishwa na matatizo mbalimbali mwilini ambayo asili yake inaweza kuwa sehemu maumivu yalipo au sehemu nyingine mbali na maumivu hayo.

Maumivu ya kitovu

Maumivu ya kitovu

Maumivu ya kitovu asili yake inaweza kuwa karibu na kitovu au eneo lililo mbali na kitovu, baadhi ya visabaishi vinavyohitaji matibabu ya haraka ni homa ya kidole tumbo.

Maumivu ya tumbo chini ya kitovu

Maumivu ya tumbo chini ya kitovu

Husababishwa na madhaifu katika via vilivyo karibu au mbali na kitovu, baadhi yake ni maambukizi kwenye via vya mfumo wa chakula, mfumo wa mkojo kama kibofu n.k. Wasiliana na daktari kufahamu kisababishi kwako.

bottom of page