top of page

Mwandishi:

Dkt. Sospeter M, MD

Mhariri:

Dkt. Lugonda B, MD

4 Aprili 2020 17:45:07

Abacavir (ABC)

Abacavir (ABC)

Abacavir ni dawa mojawapo ya kudhoofisha makali ya Virusi vya UKIMWI(ART) na ipo kwenye kundi la dawa zinazoitwa NRTIs. Dawa hii haitumiki kama yenyewe, huchanganywa na dawa zingine za ART kudhibiti makali ya VVU. Kundi la dawa za NRTIs hufanya kazi ya kupunguza makali ya VVU kwa kuzuia RNA ya kirusi kujitengenezea DNA. Ili RNA itengeneze DNA inahitaji kimeng’enya kinachoitwa Reverse Transcriptase, abacavir huzuia kimeng’enya hiki na hivyo kirusi kushindwa kujuzalia.


Rangi na Fomu ya Abacavir (ABC)


Dawa hii hupatikana katika fomu ya kidonge na kimiminika

Rangi ya kidonge hutofautina kulingana na kampuni, inaweza kuwa nyeupe, njano mpauko, n.k Huweza kutumika hata pasipo chakula na kidonge huwa chenye miligramu 300, dawa ya maji huwa na miligramu 20 kwa kila mililita moja


Dawa kundi moja na Abacavir


  • Lamivudine (3TC)

  • Emtricitabine (FTC)

  • Zidovudine (AZT)


Abacavir hutibu nini?


Hutumika pamoja na dawa zingine katika kuthibiti virusi vya UKIMWI. Abacavir itatumika endapo imeungana na dawa zifuatazo ikiwemo yenyewe.

  • Abacavir (ABC) +Lamivudine (3TC) +Dolutegravir (DTG) kwa kifupi TRIUMEQ

  • Abacavir/Lamivudine

  • Abacavir, Lamivudine, Tenofovir

  • Abacavir hufahamika kwa jina jingine la Ziagen


Dozi ya Abacavir (ABC)


Mgonjwa anapaswa kutumia dawa hii kama ambavyo atakavyoelekezwa na Daktari.


Dawa zisizopaswa kutumika na Abacavir (ABC)


  • Emtricitabine

  • Ganciclovir

  • Ribavirin

  • Tipranavir

  • Zidovudine

  • Atanazavir

  • Didanosine

  • Methadone

  • Orlistat

  • Ethanol

  • Elvitegravir/cobicistat/emtricitabine/tenofovir


Abacavir ikitumiwa na dawa zifuatazo, mgonjwa anatakiwa kuwa chini ya uangalizi:

  • Fosamprenavir

  • Indinavir

  • Lamivudine

  • Methadone

  • Nelfinavir

  • Nevirapine

  • Atazanavir

  • Cabozantinib

  • Saquinavir

  • Stavudine

  • Tenofovir df

  • Tipranavir

  • Zidovudine

  • Didanosine

  • Efavirenz

  • Emtricitabine

  • Enfuvirtide

  • Orlistat

  • Ritonavir


Wagonjwa wasiopaswa kutumia abacavir


  • Mwenye historia ya mzio wa dawa hii

  • Wenye matatizo ya ini


Tahadhari kwa mtumiaji


Tahadhari inapaswa kuchukuliwa kwa;


  • Waliovimba ini

  • Wenye magonjwa mengine yanayoharibu kinga ya mwili kama ugonjwa wa Graves


Matumizi kwa mama mjamzito


Tafiti hazijathibitishwa kwamba ni kwa kiasi gani madhara kwa mtoto yanaweza kutokea ikiwa pamoja na matatizo katika uumbaji wa mtoto akiwa tumboni mwa mama.


Matumizi kwa mama anayenyonyesha


Mama mwenye Maambukizi ya HIV hapaswi kunyonyesha wakati wa miezi 6 yote hata hivyo haina madhara endapo itapita katika maziwa


Maudhi ya abacavir


Baadhi ya maudhi madogo ya dawa hi ni pamoja na:


  • Uchovu wa mwili

  • Homa

  • Maumivu ya misuli

  • Maumivu ya kichwa

  • Vipele

  • Kichefuchefu

  • Kutapika

  • Mzio

  • Kuwa na woga na hofu

  • kushuka kwa shinikizo la damu

  • Konstipesheni

  • Kukosa usingizi(insomnia)

  • Upungufu wa damu

  • Maumivu ya tumbo

  • Kukohoa

  • Anoreksia


Je kama umesahau dozi yako ya Abacavir (ABC) ufanyaje ?


Dawa hii hutumika kwa mchanganyiko pamoja na dawa zingine za kuthibiti VVU, endapo utasahau kunywa dozi yako, unapaswa kunywa na Kuendelea na muda huo siku inayofuata.


Lakini ukikumbuka kunywa baada ya masaa 24 kupita, kunywa dozi inayofuata kama ulivyopangiwa na daktari na achana na dozi uliyosahau.


ONYO: Usitumie dawa yoyote bila ushauri wa daktari. Dawa zinaweza kuleta madhara mwilini na pia matumizi ya baadhi ya dawa pasipo ushauri na vipimo husababisha  vimelea kuwa sugu dhidi ya dawa hiyo.
ULY clinic inakushauri kuwasiliana na daktari wako unapotaka kuchukua maamuzi yoyote yanayohusu afya yako.
Wasiliana na daktari/Mfamasia wa ULY clinic kwa ushauri na Tiba au kuandikiwa dawa kwa kupiga simu au Kubonyeza Pata tiba chini ya tovuti hii.

Imeboreshwa,

3 Novemba 2021 11:50:37

Rejea za mada hii:-

1.National Guidelines for the management of HIV&AIDS 7thEdition April 2019 ukurasa wa 71 na 206

2.Goodman and Gilman’s The pharmacological Basis of therapeutic ISBN 978-0-07-1624428 ukurasa wa 1636

3.Modern pharmacology with Clinical applications written by Charles R. Craig and Robert E. Stitizel Ukurasa wa 588

4.Clinical pharmacology and Therapeutics Written by James M Ritter ISBN 978-0-340-90046-8 ukurasa wa 353

5.MedScape.Abacavir. https://reference.medscape.com/drug/ziagen-abacavir-342600 Imechukuliwa 4/4/2020

6.Drugbank. Abacavir. https://www.drugbank.ca/drugs/DB01048. Imechukuliwa 4/4/2020

7.AIDS info. Drugs.abacavir. https://aidsinfo.nih.gov/drugs/257/abacavir/20/professional. Imechukuliwa 4/4/2020
bottom of page