top of page

Mwandishi:

Dkt. Sospeter M, MD

Mhariri:

Dkt. Lugonda B, MD

8 Aprili 2020 06:27:11

Amoxicillin

Amoxicillin

Ni antibiotiki inayotibu maambukizi yanayosababishwa na bakteria. Kazi yake kuu kwa bakteria hawa ni kuua ama kuzuia ukuaji wao. Dawa hii huweza kutibu bakteria wa gramu hasina Gram chanya.

Kundi la dawa

Amoxicillin ni antibayotiki mojawapo iliyo kwenye kundi la Penicillin lijulikanalo kama aminopenicillin. Kundi hili ni la kwanza kujulikana kuwa na uwezo wa kupambana na bakteria wa Gramu hasi ambao hawatoi vomeng’enya vya Beta Lactam.

Sifa za dawa


  • Hustahimili asidi iliyo tumboni hivyo inaweza kutolewa kama kidonge cha kumeza

  • Dawa inapatikana kwenye mfumo wa kidonge, kidonge cha kutafuna, tembe na maji maji ya kunywa.

  • Rangi ya dawa inaweza kuwa nyeupe na kahawia isiyokolea, hata hivyo rangi ya dawa hutegemea kiwanda kinachotengeneza dawa

  • Hufyonzwa vizuri inapotumika pamoja na chakula


Fomu ya dawa wa Amoxicillin


Dawa hii hupatikana kwenye mfumo wa;


  • Kidonge milligramu 250-500

  • Tembe milligramu 250-500

  • Mfumo wa unga milligramu 250/kwa vayo


Utoaji taka mwilini wa Amoxicillin


Umetaboli wa amoxicillin hufanyika kwenye Ini. Utoaji wa sumu mwilini hufanywa na Figo na matumbo.


Amoxicillin hutibu magonjwa gani?


Dawa ya amoxicillin hutumika kutibu magonjwa yafuatayo yanayosababishwa na bakteria;


  • Kutibu maambukizi ya bacteria katika njia ya mkojo (UTI)

  • Kutibu maambukizi ya bacteria katika njia ya upumuaji mfano Neumonia

  • Kutibu maradhi ya sikio, Jicho na Pia

  • Kutibu maambukizi katika mfumo wa chakula au tumbo

  • Kutibu maambukizi ya ngozi na tishu laini

  • Kutibu maambukizi ya Bacteria H.Pyroli anayesababisha vidonda vya tumbo( hutumika na dawa zinine sio peke yake)


Amoxicillin huua bateria gani?


Baadhi ya Bakteria ambao wanadhuriwa na dawa hii ni:


  • Escherichia Coli

  • Haemophilus influenza

  • Streptococci

  • Neisseria Gonorrhoea

  • baadhi ya straini za Staphylococcus

  • Helicobacter pylori


Angalizo kwa watumiaji wa Amoxicillin


Tumia Dawa hii kwa Umakini kwa wagonjwa hawa


  • Wenye shida ya aleji au mzio wa Dawa hii na jamii ya Dawa ya penicillin mfano ampicillin, oxacillin

  • Wenye shida ya Ini

  • Wenye shida ya Figo

  • Wenye historia ya Pumu(asthma)

  • Wenye Aleji au mzio wa kundi la Dawa aina ya cephalosporin


Dawa zisizopaswa kutumika pamoja na Amoxicillin


Dawa hii Hairuhusiwi kutumika pamoja na Dawa zifuatazo kutokana na madhara makubwa yanaoweza kujitokeza

  • Chanjo hai ya BCG

  • Chanjo hai ya kipindupindu

  • Chanjo hai ya taifodi

  • Demeclocycline

  • Doxycycline

  • Eravacycline

  • Minocycline

  • Mycophenolate

  • Omadacycline

  • Pexidartinib

  • Pretomanid

  • Sarecycline

  • Tetracycline

  • Usitumie Dawa hii pamoja na Dawa ya probenecid sababu huongeza sumu ya amoxicillin mwilini.

  • Dawa hii inaongeza ufanyaji kazi wa dawa zinazozuia damu kuganga mfano warfarin, heparin.

  • Usitumie Dawa hii pamoja na Dawa aina Allopurinol sababu hupelekea Aleji Kali katika ngozi na Kuwashwa kwa ngozi.


Dawa kundi moja na Amoxicillin


Dawa zingine ambazo zipo kwenye kundi moja na Amoxicillin ni zifuatazo :


  • Ampicillin

  • Bacampicillin


Amoxicillin haipaswi kutumika kwa wagonjwa gani?


Amoxicillin haipaswi kutumika kwa wagonjwa hawa

  • Wagonjwa wenye mzio na Penicillin

  • Wagonjwa wenye mzioa na Cephalosporins

  • Dawa hii haipaswi kutumika kwa watu ambao hawana Maambukizi ya bakteria ili kuepusha dawa kuishiwa nguvu au bakteria kuwa sugu.


Matumizi ya Amoxicillin kwa wajawazito


Inaweza kutumika kwa mama mjamzito endapo faida ni kubwa kuliko madhara.


Matumizi ya Amoxicillin kwa wanaonyonyesha


Tafiti zinaonyesha kuwa kuna kiwango cha Amoxicillin hupita na kuingia kwenye maziwa ya mama na kumsababishia mtoto maudhi kama kuharisha, lakini hakuna madhara yanayoathiri kiwango cha uzalishaji wa maziwa.


Maudhi ya dawa Amoxicillin


Baadhi ya maudhi madogo ya dawa hi ni pamoja na :


  • Kuharisha

  • Kizunguzungu

  • Kiungulia

  • Kukosa usingizi

  • Kichefuchefu

  • Kuwashwa mwili

  • Kutapika

  • Maumivu ya tumbo

  • Mzio

  • Maumivu ya kichwa

  • Kuishiwa damu


Ufanye nini kama umesahau dozi yako?


Endapo umesahau kutumia dozi yako, tumia mara tu unapokumbuka, isipokua endapo muda wa dozi nyingine umefika unatakiwa kuruka hiyo dozi uliyosahau na kuendelea na dozi yako kwa muda kama ulivyopangiwa na daktari wako

ONYO: Usitumie dawa yoyote bila ushauri wa daktari. Dawa zinaweza kuleta madhara mwilini na pia matumizi ya baadhi ya dawa pasipo ushauri na vipimo husababisha  vimelea kuwa sugu dhidi ya dawa hiyo.
ULY clinic inakushauri kuwasiliana na daktari wako unapotaka kuchukua maamuzi yoyote yanayohusu afya yako.
Wasiliana na daktari/Mfamasia wa ULY clinic kwa ushauri na Tiba au kuandikiwa dawa kwa kupiga simu au Kubonyeza Pata tiba chini ya tovuti hii.

Imeboreshwa,

3 Novemba 2021 11:49:13

Rejea za mada hii:-

1.Amoxicillin Uses, side effects, interactions at https://www.webmd.com/drugs/2/drug-1531-3295/amoxicillin-oral/amoxicillin-oral/details. 7.4.2020

2.Amoxicillin Uses, Side effect and dosage guide at https://www.drugs.com/amoxicillin.html. 7.4.2020

3.Amoxicillin Uses, dosage and side effects at https://www.rxlist.com/amoxicillin-drug.htm. 7.4.2020

4.Amoxicillin what is it and does work at https://www.medicalnewstoday.com/articles/158481.7.4.2020
bottom of page