top of page

Mwandishi:

Dkt. Sospeter M, MD

Mhariri:

Dkt. Lugonda B, MD

21 Aprili 2020, 20:32:49

Bumetanide

Bumetanide

Bumetadine ni dawa mojawapo ya kutibu kuvimba kwa mwili kutokana na magonjwa ya moyo na figo. Dawa hii ipo kwenye kundi la dawa zinazoitwa Loop Diuretics. Dawa hii huwa maarafu kwa majina ya Bumex na Burinex.

Rangi ya Bumetanide


Rangi ya Bumetanide huweza kuwa nyeupe,lakini mara nyingi hutegemea aina ya kiwanda kinachotengeneza

Dawa hii haina madhara inapotumika pamoja na chakula

Bumetadine hupatikana katika mfumo wa kidonge wenye uzito wa Milligram zifuatazo;


  • 0.5mg

  • 1mg

  • 2mg

  • Pia hupatikana katika mfumo wa maji kwa ajili ya sindano katika uzito wa 0.25mg/Ml


Dawa zingine zilizo kwenye kundi moja (Loop Diuretics) na dawa hii ni;


  • Ethacrynic Acid

  • Furosemide

  • Torsemide

Namna dawa inavyofanya kazi:


  • Hufanya kazi kwa kuzuia ufyozwaji wa Sodiamu Chloraidi na maji kwenye mirija ya figo na hii humpelekea mtu kukojoa mara kwa mara

  • Sodiamu inapopungua mwilini , mishipa ya damu huongezeka kipenyo na hivyo kushusha shinikizo la damu.

  • Ufyozwaji wa maji unapozuiwa, maji mengi hupotea kwa njia ya mkojo na hivyo uvimbe wa mwili hupunguza kwa wagonjwa wa moyo na figo.

Kazi ya dawa;


  • Hutumika kutibu hali ya kuvimba kwa sehemu za mwili kama miguu na uso ambayo hali hii huweza kuwatokea wagonjwa wa moyo ulioferi Ini na figo

  • Hutumika kutibu shinikizo la juu la damu

Dawa hii haipaswi kutumika pamoja na dawa zifuatazo:


  • Amikacin

  • Gentamicin

  • Lofexidine

  • Neomycin

  • Paromomycin

  • Squill

  • Streptomycin

  • Tobramycin

Matumizi ya Bumetanide


Dawa hii haipaswi kutumika kwa mgonjwa mwenye mzio na dawa hii na mgonjwa mwenye shida ya kukojoa pamoja na watoto chini ya siku 28


Tahadhari kwa dawa hii:


  • Huweza kupelekea hatari ya kupoteza elekrolaiti kwenye mwili na yapo madhara mengi ya kupoteza elekrolaiti kama Haipaglaisemia , haipotensheni, haipokalemia, haiponatremia na kuishiwa maji.

  • Endapo itatumika kwa mgonjwa mwenye shida ya kukojoa anapaswa kufuatiliwa kwa ukaribu

Kwa mama mjamzito na anayenyonyesha


Dawa hii ipo kwenye kundi C la usalama wa dawa kipindi cha ujauzito

Dawa hii inapaswa kutumika kwa tahadhari kwa mama mjamzito na mama anayenyonyesha.


Baadhi ya maudhi madogo ya dawa hi ni pamoja na ;


  • Upungufu wa madini ya Potasiamu

  • Upungufu wa madini ya Sodiamu

  • Sukari kuwa nyingi mwilini

  • Kuongeza kwa wingi wa creatinine kwenye damu

  • Kizunguzungu

  • Misuli kukaza

  • Sumu kwenye sikio


Je endapo utasahau dozi yako ufanyaje?


Endapo mgonjwa atasahau kutumia hii dawa anapaswa kutumia pindi anapokumbuka.

ONYO: Usitumie dawa yoyote bila ushauri wa daktari. Dawa zinaweza kuleta madhara mwilini na pia matumizi ya baadhi ya dawa pasipo ushauri na vipimo husababisha  vimelea kuwa sugu dhidi ya dawa hiyo.
ULY clinic inakushauri kuwasiliana na daktari wako unapotaka kuchukua maamuzi yoyote yanayohusu afya yako.
Wasiliana na daktari/Mfamasia wa ULY clinic kwa ushauri na Tiba au kuandikiwa dawa kwa kupiga simu au Kubonyeza Pata tiba chini ya tovuti hii.

Imeboreshwa,

3 Novemba 2021, 11:48:09

Rejea za mada hii:-

1.WebMd.Bumetanide.https://www.webmd.com/drugs/2/drug-14575/bumetanide-oral/details. Imechukuliwa 21/4/2020

2.Goodmannn and Gilman’s The pharmacological Basis of therapeutic ISBN 978-0-07-1624428 ukurasa wa 683

3.MedScape.Bumex.https://reference.medscape.com/drug/bumex-burinex-bumetanide-342421. Imechukuliwa 21/4/2020

4.DrugBank.Bumetanide.https://www.drugbank.ca/drugs/DB00887. Imechukuliwa 21/4/2020

5.RxWiki. https://www.rxwiki.com/bumetanide. Imechukuliwa 21/4/2020
bottom of page