top of page

Mwandishi:

Dkt. Sospeter M, MD

Mhariri:

Dkt. Lugonda B, MD

10 Septemba 2021 17:30:44

Dawa Dapsone

Dawa Dapsone

Dapsone ni dawa iliyotengenezwa kutoka kwenye kemikali diamino-sulfone yenye uwezo wa kuzuia michomo kutokana na kinga za mwili pamoja na uwezo w akufanya kazi kama antibayotiki. Hutumika awali kwenye matibabu ya ukoma na leprosy ugonjwa wa ngozi wa dermatitis herpetiformis.


Majina mengine ya Dapsone


Majina mengine ya Dapsone ni;

  • Avlosulfon

  • Aczone


Namna Dapsone inavyoweza kufanya kazi


Hufanya kazi kwa kupunguza uvimbe kutokana mwitikio wa kinga za mwili na kuzuia ukuaji wa bakteria.


Kwenye tiba ya ukoma, dapson hufanya kazi kwa kuzuia uzalianaji wa bakteria Mycobacterium leprae. Hufanya hivi kwa kuzuia bakteria kutumia para-aminobenzoic acid (PABA) ili kuzalisha folic acid


Licha ya kutofahamika vema namna inavyofanya kazi kutibu magonjwa ya ngozi, dapson hufahamika kuweza kufanya kazi hiyo kwa kudhuru utendaji kazi wa chembe za ulinzi za neutrophil, eosinophils na monosait.


Dawa zilizo kundi moja na Dapsone


Dawa zilizo kundi moja na Dapsone ni ;

  • Clofazimine

  • Rifampicin


Fomu ya dawa ya Dapsone


Dawa hii ipo katika fomu ya vidonge vyenye uzito wa miligramu;

  • 25mg

  • 100mg


Dapsone hutibu nini?


Matumizi ambayo yameidhinishwa na FDA


  • Hutumika kutibu ukoma

  • Hutumika kutibu ugonjwa wa ngozi wa dermatitis herpetiformis

  • Hutumika kutibu ugonjwa wa Hansen's

  • Hutumika kutibu kifua kikuu ikiunganishwa na dawa nyingine kama Rifampicin na Ethambutol

  • Hutumika kama kinga na tiba ya nimonia ya jiroveci au Pneumocystis (carinii) jiroveci


Matumizi ambayo hayajahidhinishwa na FDA


  • Kutibu malenge ya makubwa ya dermatosis

  • Malenge makubwa ya lupus erythematosus,

  • Kutibu malenge makubwa ya erythema elevatum diutinum

  • Kutibu magonjwa ya malenge makubwa kutokana na shambulio binafsi la kinga za mwili mfano IgA pemphigus, pustular dermatosis ya kope za macho, pemphigus vulgaris, pemphigus foliaceous, na epidermolysis bullosa acquisita

  • Kutibu michomo kinga kwenye mishipa ya damu kama ugonjwa wa leukocytoclastic na urticarial

  • Kutibu magonjwa ya ngozi kutokana na ongezeko la neutrophil mfano sindromu ya Sweet, pyoderma gangrenosum na sindromu ya Behcet

  • Kutibu lupus erythematosus ya wastani, polychondritis ya kujirudia, granuloma annulare, loxoscelism, granuloma faciale, rosacea, panniculitis, pustular psoriasis, chunusi kubwa na rhinosporidiosis


Vimelea wanaodhuriwa na Dapsone


  • Mycobacterium Leprae


Ufozwaji wa dawa


Ufozwaji wa dawa hii hufanyika vizuri ikiingia kwenye mfumo wa chakula.


Wagonjwa wasiopaswa kutumia dapson


Wagonjwa wasiopaswa kutumia Dapsone ni wale


  • Wagonjwa wenye mzio na Dapsone.

  • Wagonjwa wenye mzio na dawa jamii ya Antileprosy.


Mwingiliano wa Dapsone na chakula


Dawa hii huweza kutumika kukiwa na chakula ama bila chakula.


Utoaji taka wa Dapsone mwilini


Dawa hii hutolewa mwilini kwa njia ya mkojo.


Matumizi ya Dapsone kwa mjamzito na anayenyonyesha


Matumizi ya Dapsone kwa mama mjamzito

Tafiti zinaonesha kuwa dawa hii inaweza kuleta madhara kwa mtoto. Hivyo haishauriwi kutumia dawa hii wakati wa ujauzito.


Matumizi ya Dapsone mama anayenyonyesha

Dawa hii inaingia kwenye maziwa ya mama anayenyosha na kusababisha madhara kwa mtoto hivyo haitakiwi kutumiwa na mama anayenyonyesha.


Dawa zenye muingiliano na Dapsone


Dawa zenye mwingiliano mkali na hivyo kutofaa kutumika pamoja na Dapsone;

  • Abametapir

  • Aluminum hydroxide

  • Apalutamide

  • Calcium carbonate

  • Chanjo hai ya BCG

  • Chanjo hai ya Typhoid

  • Dapsone topical

  • Famotidine

  • Fexinidazole

  • Ibuprofen/famotidine

  • Idelalisib

  • Ivosidenib

  • Lansoprazole

  • Lonafarnib

  • Mefloquine

  • Nefazodone

  • Saquinavir

  • Selinexor

  • Sodium bicarbonate

  • Sodium citrate/citric acid

  • Tucatinib

  • Voxelotor


Dawa zinazoweza kutumika na Dapsone chini ya uangalizi;

  • Carbamazepine

  • Cenobamate

  • Clarithromycin

  • Cobicistat

  • Digoxin

  • Efavirenz

  • Erythromycin base

  • Isoniazid

  • Ketoconazole

  • Methotrexate

  • Mifepristone

  • Rifabutin

  • Rifampin

  • Stiripentol

  • Tazemetostat

  • Tecovirimat

  • Teriflunomide

  • Tetracaine


Dawa zenye mwingiliano mdogo na Dapsone;

  • Artemether/lumefantrine

  • Atazanavir

  • Cortisone

  • Dexamethasone

  • Etravirine

  • Fluconazole

  • Griseofulvin

  • Hydrocortisone

  • Methylprednisolone

  • Metronidazole

  • Miconazole vaginal

  • Nifedipine

  • Phenobarbital

  • Phenytoin

  • Prednisone

  • Rifapentine

  • Ritonavir

  • Rufinamide

  • Secobarbital

  • Sulfamethoxazole

  • Verapamil

  • Voriconazole

  • Zafirlukast

  • Zidovudine


Maudhi ya dapsone


Kwenye damu

  • Upungufu wa damu kutokana na kuvunjwa kwa chembe nyekundu za damu

  • Methemoglobinemia

  • Leukopenia

  • Agranulocytosis


Ngozi

  • Mzio wa ngozi

  • Kubanduka kwa ngozi

  • Mebilliform eruption

  • Exfoliative erythroderma

  • Lupus erythematosus ya dawa

  • Epidermal necrolisis


Mfumo wa beva

  • Nyuropathi ya pembeni na kupoteza uwezo wa kimota


Kiakili

Kukosa usingizi na saikosis


Macho

  • Uono hafifu


Sikio, kinywa na pua

  • Kusikia masauti,

  • Hisia za vitu kuzunguka


Moyo

  • Mapigo ya moyo kwenda haraka


Mapafu

  • Eosinophilia ya mapafu


Ini

  • Hepatitis ya dawa

  • Sindromu ya dapsone

  • Manjano ya kutulia na kupungua kiwango cha albumin kwenye damu bila kuwa na kiwango kikubwa cha protini


Mfumo wa mmeng’enyo wa chakula


  • Kichefuchefu

  • Kutapika

  • Maumivu ya tumbo

  • Kukosa hamu ya kula

  • Kupungua uzito

  • Michomo kwenye kongosho


Figo

  • Sindromu ya Nephrotic,

  • Albuminuria,

  • Nekrosisi ya papilla za figo



Sindromu ya dapson

Hutokea wiki 2 hadi 6 toka mgonjwa ameanza kutumia dawa. Huwa na dalili za homa, harara kwenye ngozi, na hepataitis. Vipimo huonyesha ongezeko la vimeng’enya vya ini kwenye damu na eosinophilia. Huweza sababisha mgonjwa kupoteza maisha kama asipopata matibabu


Ufanye nini endapo utasahau kutumia dozi yako?


Kama umesahau kutumia dozi yako tumia mara pale utakapokumbuka, kama muda wa dozi inayofata umekaribia usimeze dozi uliyosahau endelea na dozi inayofuata kwa muda uliopangiwa na daktari. Usimeze dozi mbili kufidia uliyosahau.

ONYO: Usitumie dawa yoyote bila ushauri wa daktari. Dawa zinaweza kuleta madhara mwilini na pia matumizi ya baadhi ya dawa pasipo ushauri na vipimo husababisha  vimelea kuwa sugu dhidi ya dawa hiyo.
ULY clinic inakushauri kuwasiliana na daktari wako unapotaka kuchukua maamuzi yoyote yanayohusu afya yako.
Wasiliana na daktari/Mfamasia wa ULY clinic kwa ushauri na Tiba au kuandikiwa dawa kwa kupiga simu au Kubonyeza Pata tiba chini ya tovuti hii.

Imeboreshwa,

23 Julai 2023 16:54:25

Rejea za mada hii:-

Dapsone. https://reference.medscape.com/drug/dapsone-342559#91. Imechukuliwa 09/09/2021

WEBMD. Dapsone. https://www.webmd.com/drugs/2/drug-6744/dapsone-oral/details. Imechukuliwa 09/09/2021

WEBMD. Dapsone. https://www.ncbi.nlm.nih.gov/books/NBK470552/. Imechukuliwa 09/09/2021

NCBI. Dapsone. https://www.ncbi.nlm.nih.gov/books/NBK470552/. Imechukuliwa 09/09/2021
bottom of page