Mwandishi:
Dkt. Sospeter M, MD
Mhariri:
Dkt. Lugonda B, MD
9 Septemba 2021, 20:09:57
![Dawa Fluticasone](https://static.wixstatic.com/media/26af9c_4f575b6857604697a3b374dafa1d2ba9~mv2.jpg/v1/fill/w_81,h_50,al_c,q_80,usm_0.66_1.00_0.01,enc_avif,quality_auto/Image-empty-state.jpg)
Dawa Fluticasone
Ni dawa aina jamii ya corticosteroid maarufu kwa jina jingine la Clarispray au Flonase. Dawa hii ni moja ya dawa zinazotumika kunyunyiza ndani ya pua.
Uzito na fomu ya Fluticasone
Hupatikana katika fomu ya maji yanayotumika kwa kunyunyiza puani
Dawa huwa na uzito wa mikrogramu
27.5mcg/ kwa mnyunyizo mmoja
50mcg/kwa mnyunyizo mmoja
93 mcg/ kwa mnyunyizo mmoja
Namna Fluticasone inavyoweza kufanya kazi
Dawa hii hufanya kazi katika mfumo wa kinga ya mwili kwa kupunguza uvimbe, wekundu na kuwashwa kutokana na mwitikio wa kinga za mwili kwenye kiamsha mzio, kazi hii hufanikiwa kwa kusinyaza mishipa ya damu kwenye eneo lililonyunyiziwa dawa.
Matumizi ya Fluticasone
Hutumika kutibu mafua yanayochuruzika kutokana na mzio
Hutumika kwa kutibu wagonjwa wa nyama za pua
Hutibu eczema
Soriasis
Harara kwenye ngozi kutokana na mzio
Wagonjwa wasiopaswa kutumia Fluticasone
Wagonjwa wenye mzio na dawa jamii ya Fluticasone au dawa zingine jamii ya corticosteroid
Utoaji taka wa Fluticasone
Chini ya asilimia 2 ya dawa hutolewa kwa njia ya mkojo na asilimia zinazobaki hutolewa kwa njia ya kinyesi.
Namna ya kutumia dawa
Tikisa taratibu chupa ya dawa
Jaribu kunyunyiza kwanza kama ni chupa mpya au kama hunyanyunyiza kwa muda wa wiki au zadi
Unapotumia, elekeza mbali na macho
Peng'a pua kwanza kabla ya kunyunyiza dawa puani
Endapo utatumia dozi kubwa kuliko kawaida
Kutumia dozi kubw akuliko kawaida mara nyingi hakutokei kwa sababu dawa ni ya kunyunyiza puani. Hata hivyo ikitokea umekunywa kwa bahati mbaya, wasiliana na huduma za dharura kwa msaada zaidi
Tahadhari kwa matumizi ya fluticasone
Huweza kuficha maambukizi makali puani ikiwa pamoja na maambukizi ya fangasi Huweza kuongeza ukali wa maambukizi ya virusi kwenye pua Huchelewesha kupona kwa vidonda vya puani kutokana na maambukizi, upasuaji n.k
Mwingiliano wa Fluticasone na dawa zingine
Dawa zenye mwingiliano mkali za kuzuia dawa hii kutumika pamoja na dawa zingine; Atazanavir
Clarithromycin
Conivaptan
Darunavir
Fosamprenavir
Imatinib
Indinavir
Isoniazid
Itraconazole
Ketoconazole
Kopinavir
Nefazodone
Nelfinavir
Nicardipine
Posaconazole
Quinidine
Ritonavir
Saquinavir
Tipranavir
Voriconazole
Fluticasone ikitumika na dawa zifuatazo mgonjwa anapaswa kuwa chini ya ungalizi wa karibu na mtaalamu wa afya:
Fedratinib
Letermovir
Ribociclib
Ribociclib
Rucaparib
Stiripentol
Tazemetostat
Matumizi ya Fluticasone kwa mama mjamzito
Hakuna tafiti yeyote inayoonyesha kuwa kuna madhara endapo itatumika kwa mama mjamzito. Tafiti zinaonyesha dawa hii hupita kwenye kondo kwenda kwa mtoto kwa wanyama kama panya na paka.
Matumizi ya Fluticasone kwa mama anayenyonyesha
Hakuna tafiti zinazoonyesha kuwa dawa hii inapita kwenye maziwa ya mama, madhara yake kwa mtoto anayenyonya maziwa ya mama.
Maudhi madogo ya Fluticasone
Kuongezeka hali ya kutokwa damu puani
Kutokwa na damu puani
Kuchuruzika kw mafua
Hisia za
Wekundu na mabaka kwenye koo au puani
Homa
Kutetemeka
Maumivu ya mwili
Maumivu ya macho
Uono hafifu
Kutopana kwa kidonda
Ongezeko la uchovu
Udhaifu wa misuli
Maumivu ya kichwa
Kichefuchefu
Kutapika
Kikohozi
Koo chungu
Hisia za kuungua au kuwashwa ndani ya pua
Je endapo utasahau dozi yako ufanyaje ?
Kama umesahau kutumia dozi yako, tumia mara pale utakapokumbuka
ONYO: Usitumie dawa yoyote bila ushauri wa daktari. Dawa zinaweza kuleta madhara mwilini na pia matumizi ya baadhi ya dawa pasipo ushauri na vipimo husababisha vimelea kuwa sugu dhidi ya dawa hiyo.
ULY clinic inakushauri kuwasiliana na daktari wako unapotaka kuchukua maamuzi yoyote yanayohusu afya yako.
Wasiliana na daktari/Mfamasia wa ULY clinic kwa ushauri na Tiba au kuandikiwa dawa kwa kupiga simu au Kubonyeza Pata tiba chini ya tovuti hii.
Imeboreshwa,
23 Julai 2023, 16:54:25
Rejea za mada hii:-