top of page

Mwandishi:

Dkt. Sospeter M, MD

Mhariri:

Dkt. Lugonda B, MD

Imeboreshwa:

28 Mei 2025, 10:15:48

Dawa Mifepristone

Dawa Mifepristone

Mifepristone ni dawa ya kuzuia homoni ya projesteroni ambayo hutumika kwa ajili ya kutoa mimba salama (medical abortion), kusababisha uchungu wa uzazi na kutibu hali nyingine zinazohusiana na homoni.


Rangi na Fomu ya Mifepristone

Mifepristone hupatikana katika fomu ya kidonge (tablet).Kidonge mara nyingi huwa na miligramu 200 za mifepristone.Rangi ya kidonge hutofautiana na kampuni lakini huwa nyeupe au kijivu hafifu.


Dawa kundi moja na Mifepristone

Mifepristone haipo kwenye kundi la dawa nyingi, lakini mara nyingi hutumika pamoja na:

  • Misoprostol – kwa ajili ya kutoa mimba au kusababisha uchungu

  • Methotrexate – katika baadhi ya taratibu mbadala kwa uavyaji mimba wa mapema


Mifepristone hutibu nini?

  1. Utoaji wa mimba salama (medical abortion) hadi wiki 10 za ujauzito

  2. Kutibu mimba iliyofia tumboni (missed abortion)

  3. Kusababisha uchungu wa uzazi kabla ya upasuaji au kujifungua

  4. Kutibu fibroids au hali ya homoni inayojulikana kama Cushing’s syndrome (katika baadhi ya nchi)


Dozi ya Mifepristone

  • Kwa kutoa mimba salama: 200 mg kwa mdomo, ikifuatiwa na misoprostol 800 mcg baada ya saa 24–48.

  • Dozi maalum hutolewa na mtoa huduma wa afya kulingana na hali ya ujauzito na afya ya mgonjwa.


Dawa zisizopaswa kutumika na Mifepristone

  • Corticosteroids (kama dexamethasone) – hupingana na mifepristone

  • Anticoagulants (kama warfarin) – huongeza hatari ya kutokwa damu

  • Erythromycin

  • Ketoconazole

  • Rifampin

  • Phenytoin

  • St. John’s Wort (dawa ya mitishamba)


Wagonjwa wasiopaswa kutumia Mifepristone

  • Mama mjamzito asiye na nia ya kutoa mimba

  • Wenye historia ya mzigo wa mimba nje ya mji wa mimba (ectopic pregnancy)

  • Wagonjwa wa pumu kali

  • Wagonjwa wenye matatizo ya tezi, ini au figo

  • Wenye matatizo ya damu kuganda (bleeding disorders)


Tahadhari kwa mtumiaji

  • Dawa itumiwe chini ya uangalizi wa mtoa huduma wa afya mwenye mafunzo maalum.

  • Tumia kwa tahadhari kwa wagonjwa wenye historia ya upasuaji mkubwa wa uterasi.

  • Hakikisha huna mimba nje ya uterasi kabla ya matumizi.


Matumizi kwa mama mjamzito

Hairuhusiwi, isipokuwa kwa madhumuni mahsusi ya kutoa mimba au kusababisha uchungu kwa sababu ya mimba iliyofia tumboni.


Matumizi kwa mama anayenyonyesha

Taarifa kuhusu usalama wake wakati wa kunyonyesha bado ni chache. Ushauri wa kitaalamu unahitajika kabla ya kutumia.


Maudhi ya Mifepristone

Baadhi ya maudhi ya kawaida ni:

  • Maumivu ya tumbo

  • Kutokwa na damu ukeni

  • Kichefuchefu

  • Kuharisha

  • Kizunguzungu

  • Homa ndogo

  • Uchovu

  • Maumivu ya kichwa

  • Kutapika


Je, ukisahau dozi ya Mifepristone ufanyaje?

Kwa kuwa dawa hutumika kwa tukio maalum (single use), ni muhimu kufuata ratiba ya dozi kama ilivyoelekezwa. Ikiwa dozi imecheleweshwa, wasiliana na mtoa huduma wa afya kabla ya kuendelea na misoprostol.

ONYO: Usitumie dawa yoyote bila ushauri wa daktari. Dawa zinaweza kuleta madhara mwilini na pia matumizi ya baadhi ya dawa pasipo ushauri na vipimo husababisha  vimelea kuwa sugu dhidi ya dawa hiyo.
ULY clinic inakushauri kuwasiliana na daktari wako unapotaka kuchukua maamuzi yoyote yanayohusu afya yako.
Wasiliana na daktari/Mfamasia wa ULY clinic kwa ushauri na Tiba au kuandikiwa dawa kwa kupiga simu au Kubonyeza Pata tiba chini ya tovuti hii.

Imeandikwa:

28 Mei 2025, 10:11:37

Rejea za mada hii:-

1. World Health Organization. Medical management of abortion. Geneva: WHO; 2018.

2. Kapp N, Ghosh N, Feldblum PJ. Medical abortion in primary care: review of clinical evidence. BMJ. 2018;360:k1382.

3. Raymond EG, Blanchard K, Blumenthal PD. Misoprostol alone for early medical abortion. Int J Gynaecol Obstet. 2006;92(3):281–3.

4. Gynuity Health Projects. Mifepristone information sheet [Internet]. 2020 [cited 2025 May 28]. Available from: https://gynuity.org
bottom of page