top of page

Mwandishi:

Dkt. Sospeter M, MD

Mhariri:

Dkt. Lugonda B, MD

10 Septemba 2021 11:50:24

Dawa Piperacillin/tazobactam

Dawa Piperacillin/tazobactam

Piperacillin tazobactam ni dawa ya antibayotiki katika kundi la penicillin iliyounganishwa na tazobactam kwa ajili ya kuongeza uwezo wake wa kutibu magonjwa mbalimbali yanayosababishwa na bakteria haswa wa gramu hasi, na kiasi cha bakteria wa gramu chanya na anaerobiki. Tazobactam inayoongezwa kwenye dawa hii huwa na uwezo wa kuzuia kimeng’enya muhimu cha bakteria chenye jina la β-lactamase huongeza uwezo wa dawa hii zaidi na kufanya dawa ifanye kazi kwa vimelea wanaozalisha kimeng'enya hiki.


Uzito na fomu ya Piperacillin Tazobactam


Piperacillin Tazobactam hupatikana kama unga kwenye kichupa kwa ajili ya kuchanganywa na maji na kuchomwa kwa sindano. Kichupa kinaweza kuwa na


  • 2.25gm (2gm piperacillin na 0.25gm za Tazobactam)

  • 3.375 gm (3gm piperacillin na 0.375gm za Tazobactam)

  • 4.5 gm (4gm piperacillin na 0.5gm za Tazobactam)

  • 40.5gm ( 36gm piperacillin na 4.5gm za Tazobactam)


Dawa zilizo kundi moja na Piperacillin/tazobactam


Dawa zingine ambazo zipo kwenye kundi moja(penicillin) na Piperacillin/tazobactam ni zifuatazo :


  • Amoxicillin

  • Bacampicillin

  • Penicillin G

  • Penicillin V

  • Methicillin

  • Ampicillin

  • Procaine Penicillin

  • Dicloxacillin


Dawa ambazo zipo kundi moja na piperacillin/tazobactam kama kundi la dawa zilizoongezewa uwezo mpana wa matibabu


  • Piperacillin

  • Piperacillin/tazobactam

  • Pipracil

  • Ticarcillin/clavulanate

  • Timentin


Namna Piperacillin inavyoweza kufanya kazi


Piperacillin hufanya kazi kwa kujishikiza kwenye mlango wa penicillin, mlango huu hutumiwa na kimeng’enya cha peptidoglycan ili kuzalisha vijenzi muhimu vya ukuta wa bakteria. Kufanya kazi kwa dawa hii huzuia utengenezaji wa ukuta wa bakteria na hivyo pia kuzuia uzalianaji wake. Tazobactam inayoungwa na dawa hii, huzuia kimeng’enya beta lactamase ambacho huzalishwa na bakteria ili kuvunja dawa hii hivyo kufanya dawa iweze kufanya kazi vema na kuongeza upana wake wa matibabu ya bakteria gramu hasi, gramu chanya na wale jamii ya anaerobic.


Vimelea wanaodhuriwa na Piperacillin


  • Staphylococcus aureus

  • Escherichia Coli

  • Haemophilus influenza

  • Klebsiella Pneumoniae

  • Pseudomonas aeruginosa

  • Bacteroides fragilis

  • Bacteroides ovatus

  • Bacteroides thetaiotaomicron

  • Bacteroides vulgatus

  • Acinetobacter baumannii


Mwingiliano wa Piperacillin/tazobactam na chakula


Piperacillin Tazobactam haiathriwi na cha kula kwa kuwa hutumika kwa kuchoma ndani ya michipa ya damu.


Piperacillin/Tazobactam hutibu nini?


Matumizi ya Piperacillin/Tazobactam ni kama zifuatazo :


  • Kutibu maambukizi ya bakteria kwenye via vya tumbo

  • Kutibu maambukizi ndani ya via vya uzazi kwa wanawake (PID)

  • Kutibu nimonia ya jamii

  • Kutibu nimoni ya hospitali

  • Kutibu maambukizi ya bakteria kwenye ngozi

  • Michomo kwenye appendix (Appendisaitis)

  • Selilaitiz

  • Endometriosis baada ya kujifungua

Ili kuzuia usugu wa vimelea vya maradhi kwenye dawa hii, dawa hii inapaswa kutumika kutibu au kukinga shidi ya vimelea ambao wanadhuriwa na dawa hii tu.


Wagonjwa wasiopaswa kutumia Piperacillin/Tazobactam


  • Wagonjwa wenye mzio na dawa jamii ya Penicillin

  • Wagonjwa wenye mzio na dawa jamii ya cephalosporins

  • Wagonjwa wenye mzio na carbapenem


Tahadhari kwa watumiaji wa Piperacillin/Tazobactam


  • Huweza sababisha mzio makali wa anafailaksia au sindromu ya Stevens-Johnson

  • Kuvuja kwa damu kutokana na kuharibiwa kwa mchakato wa ugandishai damu , kama dalili zitatokea, dawa isitishwe haraka

  • Huweza sababisha upungufu wa chembe ulinzi za leucocyte na neutrophil inayoisha baada ya kuacha damu

  • Kuchokoza mfumo wa fahamu kiasi cha kupelekea degedege

  • Kudhuru figo kwa mgonjwa mwenye ugonjwa mkali

  • Huweza haribu kiwango cha madini kwenye damu kwamgonjwa anayedhibitiwa kiasi cha madini mwilini haswa madini sodiamu (Na+)

  • Kuhara kutokana na maambukizi ya Clostridium difficile

  • Ongezeko la usugu wa vimelea kwenye dawa hii endapo itatumika bila kuwa maambukizi


Utoaji taka wa Piperacillin/Tazobactam mwilini


Asilimia 80 ya dawa hutolewa kwa njia ya mkojo na asilimia zinazobaki hutolewa kwa njia ya haja kubwa

Mwingiliano wa Piperacillin/Tazobactam na dawa zingine


Mwingiliano mkali hazipaswi kutumika pamoja na;


  • Ampicillin

  • Antithrombin alfa

  • Antithrombin III

  • Argatroban

  • BCG vaccine live

  • Bivalirudin

  • Cholera vaccine

  • Dalteparin

  • Enoxaparin

  • Heparin

  • Omadacycline

  • Sarecycline

  • Warfarin


Piperacillin/Tazobactam ikitumika na dawa hizi mgonjwa anapaswa kuwa chini ya ungalizi wa karibu;


  • Azithromycin

  • Bazedoxifene

  • Chloramphenicol

  • Clarithromycin

  • Demeclocycline

  • Dichlorphenamide

  • Doxycycline

  • Erythromycin base

  • Erythromycin ethylsuccinate

  • Erythromycin lactobionate

  • Erythromycin stearate

  • Minocycline

  • Probenecid

  • Sodium picosulfate/magnesium oxide/Anhydrous citric acid

  • Tetracycline

  • Vancomycin


Dawa hizi zina mwingiliano mdogo na Piperacillin/Tazobactam;


  • Amikacin

  • Aspirin

  • Aspirin/citric acid/sodium bicarbonate

  • Chlorothiazide

  • Choline magnesium trisalicylate

  • Gentamicin

  • Hydrochlorothiazide

  • Ibuprofen IV

  • Meclofenamate

  • Neomycin PO

  • Rose hips

  • Streptomycin

  • Tobramycin

  • Willow bark


Matumizi ya Piperacillin/Tazobactam kwa mama mjamzito na anayenyonyesha


Matumizi ya Piperacillin/Tazobactam kwa mama mjamzito Tafiti za wanyama zinaonyesha hatari kwa vichanga kwa ksuababisha madhaifu ya kimaumbile. Taarifa za tafiti kwa binadamu hazipatikani au hazijafanyika. Matumizi ya Piperacillin/Tazobactam kwa mama anayenyonyesha Dawa hii inaweza kutumika kwa mama anayenyonyesha ,hakuna tafiti zinazoenyesha madhara yatakayompata mtoto


Maudhi madogo ya Piperacillin/Tazobactam


  • Kuhara

  • Haja kubwa ngumu

  • Kichefuchefu

  • Gesi tumboni

  • Maumivu ya tumbo

  • Homa

  • Maumivu sehemu dawa ilipochomwa

  • Kukakamaa kwa misuli

  • Anafailaksis

  • Maumivu ya kichwa

  • Maumivu ya misuli

  • Maambukizi ya fangasi ukeni

  • Maumivu ya maungio ya miguu na mikono

  • Kukosa usingizi

  • Harara kwenye ngozi

  • Vipele kwenye ngozi

  • Kuvimba kwa ngozi

  • Muwasho wa ngozi

  • Kuvia damu chini ya ngozi

  • Kushuka kwa sukari kwenye damu

  • Michomo kinga kwenye mshipa wa damu

  • Kushuka kwa shinikizo la damu

  • Kutokwa na jasho

  • Kutokwa na damu puani


Je endapo utasahau dozi yako ya Piperacillin/Tazobactam ufanyaje?


Kama umesahau kutumia dozi yako, tumia mara pale utakapokumbuka, isipokuwa kama muda wa dozi nyingine umeshafika unatakiwa kuruka hiyo dozi uliyosahau na kuendelea na dozi inayofuata kama muda uliopangiwa.

ONYO: Usitumie dawa yoyote bila ushauri wa daktari. Dawa zinaweza kuleta madhara mwilini na pia matumizi ya baadhi ya dawa pasipo ushauri na vipimo husababisha  vimelea kuwa sugu dhidi ya dawa hiyo.
ULY clinic inakushauri kuwasiliana na daktari wako unapotaka kuchukua maamuzi yoyote yanayohusu afya yako.
Wasiliana na daktari/Mfamasia wa ULY clinic kwa ushauri na Tiba au kuandikiwa dawa kwa kupiga simu au Kubonyeza Pata tiba chini ya tovuti hii.

Imeboreshwa,

23 Julai 2023 16:54:25

Rejea za mada hii:-

Medscape. Piperacillin Tazobactam. https://reference.medscape.com/drug/zosyn-piperacillin-tazobactam-342485 ,Imetolewa 19/8/2021

NCBI. Piperacillin Tazobactam. https://pubchem.ncbi.nlm.nih.gov/compound/Piperacillin , Imetolewa 19/8/2021

MayoClinic. Piperacillin Tazobactam. https://www.mayoclinic.org/drugs-supplements/piperacillin-and-tazobactam-intravenous-route/description/drg-20072716 , Imetolewa 19/8/2021

FDA. Piperacillin Tazobactam. https://www.accessdata.fda.gov/drugsatfda_docs/label/2017/050684s88s89s90_050750s37s38s39lbl.pdf. Imechukuliwa 19/8/2021

CDC. Piperacillin Tazobactam. https://stacks.cdc.gov/view/cdc/47210/cdc_47210_DS1.pdf. Imechukuliwa 19/8/2021

Piperacillin Tazobactam. https://www.medicinenet.com/piperacillintazobactam_sodium-injection/article.htm#. Imechukuliwa 19/8/2021
bottom of page