top of page

Mwandishi:

Dkt. Sospeter M, MD

Mhariri:

Dkt. Lugonda B, MD

26 Oktoba 2020 13:00:51

Dawa ya Omoconazole

Dawa ya Omoconazole

Omoconazole ni dawa mojawapo ya kutibu magonjwa ya fangasi iliyo katika kundi la dawa linaloitwa Imidazole. Dawa hii huwa maarufu pia kwa jina la Mikogal.


Fomu na uzito wa dawa Omoconazole


Omoconaze hupatikana pia katika fomu ya Kidonge aina ya pessary vyenye miligramu

150

300

900

Omoconazole hupatikana pia katika mfumo wa krimu wenye ujazo mbalimbali na asilimia 1 ya kiini cha dawa


Namna Omoconazole inavyofanya kazi


Dawa ya Omoconazole ni aina ya dawa kutoka kundi la Imidazole, Dawa hii hufanya kazi kwa kuzuia utengenezaji wa homoni muhimu ya egosteroli ambayo hufanya kazi ya kutengeneza vijenzi vya ukuta wa seli.


Dawa zilizo kundi moja na Omoconazole


Dawa hii ipo katika kundi sawa na dawa zifuatazo;


  • Butoconazole

  • Clotrimazole

  • Econazole

  • Fenticonazole

  • Isoconazole

  • Ketoconazole

  • Luliconazole

  • Oxiconazole

  • Sertaconazole

  • Sulconazole

  • Tioconazole


Kazi ya Omoconazole


Hutumika kwenye matibabu ya fangasi kwenye ngozi

Wagonjwa wasiopaswa kutumia Omoconazole

Wagonjwa wenye aleji na dawa hii au jamii ya dawa za Antifangasi


Tahadhari kwa watumiaji wa Omoconazole


Wagonjwa wasiopaswa kutumia dawa ni ni pamoja na wagonjwa wenye aleji na dawa nyingine za antifangasi


Matumizi ya Omoconazole kwa mama mjamzito


Dawa hii ipo kwenye kundi C ya usalama wa dawa kipindi cha ujauzito


Dawa hii hushauriwa kutumika kwa uangalifu wakati wa kipindi cha ujauzito


Matumizi ya Omoconazole kwa mama nayenyonyesha


Takwimu hazijaonyesha kuwa kuna uwezekano wa hii dawa kuingia au kuwa kwenye maziwa ya mtoto ila aishauriwi itumike kwa wamama wajawazito


Maudhi ya Omoconazole


  • Baadhi ya maudhi madogo ya kutumia dawa hii ni pamoja na :

  • Kupata vipele

  • Kuhisi kuungua

  • Maumivu ya tumbo

  • Kuwashwa mwili


Endapo umesahau dozi ya Omoconazole


Je endapo utasahau dozi yako ufanyaje?


Endapo ukisahau kutumia dozi yako, tumia mara pale utakapokumbuka, na endapo muda umekaribia wa dozi nyingine acha dozi uliyosahau na endelea na dozi yako inayofuata kama ulivyopangiwa na daktari wako

ONYO: Usitumie dawa yoyote bila ushauri wa daktari. Dawa zinaweza kuleta madhara mwilini na pia matumizi ya baadhi ya dawa pasipo ushauri na vipimo husababisha  vimelea kuwa sugu dhidi ya dawa hiyo.
ULY clinic inakushauri kuwasiliana na daktari wako unapotaka kuchukua maamuzi yoyote yanayohusu afya yako.
Wasiliana na daktari/Mfamasia wa ULY clinic kwa ushauri na Tiba au kuandikiwa dawa kwa kupiga simu au Kubonyeza Pata tiba chini ya tovuti hii.

Imeboreshwa,

23 Julai 2023 16:54:56

Rejea za mada hii:-

1.Drugs.Omoconazole.https://www.drugs.com/international/omoconazole.html. Imechukuliwa 09/10/2020

2.Pubchem.Omoconazole.https://pubchem.ncbi.nlm.nih.gov/compound/Omoconazole. Imechukuliwa 09/10/2020

3.Drugbank.Omoconazole.https://www.drugbank.ca/drugs/DB13684.Imechukuliwa 09/10/2020
bottom of page