Mwandishi:
Dkt. Sospeter M, MD
Mhariri:
Dkt. Lugonda B, MD
22 Aprili 2020, 05:10:02

Fosinopril
Fosinopril ni dawa mojawapo ya kutibu shinikizo la juu la damu iliyo katika kundi la dawa linaloitwa angiotensini konventing enzaimu inhibita- ACEIs.
Fomu na uzito wa Fosinopril
Dawa hii huwa maarufu pia kwa jina la Monopril na inapatikana katika mfumo wa kidonge chenye uzito wa miligramu,
10mg
20mg na
40mg
Ufanyaji kazi wa Fosinopril
Namna dawa inavyofanya kazi kupunguza shinikizo la damu.
Dawa jamii ya ACEIs ikiwa pamoja na fosinopril hufanya kazi zifuatazo ili kupunguza shinikizo la damu
Kutanua kipenyo cha mishipa ya damu ya vena na ateri kwa kupinga utengenezaji wa homoni ya angiotensin II na uvunjwaji wa bradykinin. Kutanuka kwa mishipa husababisha mishipa kuwa na kipenyo kikubwa hivyo kushuka kwa shinikizo ndani ya mishipa na matokeo yake ni kupunguza mzigo wa damu unaoingia na kutoka kwenye moyo na kupunguza utendaji kazi wa moyo kupita kiasi.
Dawa zilizo kundi moja na Fosinopril
Dawa hii ipo katika kundi sawa na dawa zifuatazo:
Benazepril
Captopril
Enalaprili
Lisinopril
Moexipril
Perindopril
Quinapril
Fosinopril hutibu nini?
Hutumika kwenye matibabu ya wagonjwa wenye shinikizo la damu la juu
Hutumika kwenye matibabu ya moyo ulioferi
Usitumie Fosinopril na daw again?
Dawa hii haipaswi kutumika pamoja na dawa zifuatazo
Valsartan
Tolmetin
Telmisartan
Sulindac
Salsalate
Sacubitril/valsartan
Sacubitril/valsartan
Pregabalin
Piroxicam
Oxaprozin
Olmesartan
Naproxen
Nabumetone
Meloxicam
Mefenamic acid
Meclofenamate
Losartan
Lofexidine
Ketorolac
ketoprofen
Irbesartan
Indomethacin
Ibuprofen
Flurbiprofen
Fenoprofen
Etodolac
Eprosartan
Diflunisal
Diclofenac
Celecoxib
Candesartan
Azilsartan
Aspirin
Aliskiren
Wagonjwa wasiopaswa kutumia Fosinopril
Dawa hii haipaswi kutumika kwa wagonjwa wafuatao:
Wagonjwa wenye mzio na dawa hii au dawa jamii ya ACEIs
Tahadhari ya Fosinopril
Dawa hii inapaswa kutumika kwa tahadhari kwa wagonjwa wafuatao;
Wagonjwa wenye shida ya ini
Wagonjwa wenye shida ya figo
Wagonjwa wenye hatari ya kupata haipakalemia
Matumizi ya Fosinopril kwa mama mjamzito
•Haipaswi kutumika kwa mama mjamzito kwa sababu husababisha athari kwa mtoto tumboni. Madhara hayo kwa mtoto ni haipotension, haipoplezia ya fuvu, anyuria, kuferi wa figo na kifo.
Matumizi ya Fosinopril kwa mama anayenyonyesha
Haishauriwi kutumika kwa mama anayenyonyesha kwa sababu huingia kwenye maziwa ya mama.
Maudhi ya Fosinopril
Baadhi ya maudhi madogo ya dawa hi ni pamoja na;
Maumivu ya kichwa
Kutapika
Kizunguzungu
Haipakalemia
Othorstatik haipatesheni
Maumivu ya kifua
Kikohozi kikavu
Vipele kwenye ngozi
Kuharisha
Mwili kuishiwa damu
Mwili kuchoka
Je endapo utasahau dozi yako ufanyaje?
Endapo ukisahau kutumia Fosinopril, tumia mara pale utakapokumbuka, na endapo muda umekaribia wa dozi nyingine acha dozi uliyosahau na endelea na dozi yako kama ulivyopangiwa na daktari wako.
ONYO: Usitumie dawa yoyote bila ushauri wa daktari. Dawa zinaweza kuleta madhara mwilini na pia matumizi ya baadhi ya dawa pasipo ushauri na vipimo husababisha vimelea kuwa sugu dhidi ya dawa hiyo.
ULY clinic inakushauri kuwasiliana na daktari wako unapotaka kuchukua maamuzi yoyote yanayohusu afya yako.
Wasiliana na daktari/Mfamasia wa ULY clinic kwa ushauri na Tiba au kuandikiwa dawa kwa kupiga simu au Kubonyeza Pata tiba chini ya tovuti hii.
Imeboreshwa,
3 Novemba 2021, 11:33:23
Rejea za mada hii:-