Mwandishi:
Mhariri:
Imeboreshwa:
Dr.Sospeter Mangwella, MD
ULY CLINIC
4 Agosti 2025, 12:51:47
Vipele sehemu za siri tiba yake ni nini?
Swali la mgonjwa
“Vipele sehemu za siri tiba yake ni nini?”
Majibu ya kitaalamu
Vipele sehemu za siri vinaweza kuwa dalili ya hali au ugonjwa fulani unaohitaji uchunguzi na tiba mahsusi. Kwa ujumla, tiba ya vipele hutegemea chanzo chake, kwa kuwa kuna sababu nyingi zinazoweza kuvisababisha.
Visababishi vya vipele sehemu za siri
Magonjwa ya zinaa
Herpes genitalis
Kisonono
Chlamydia
Syphilis
Molluscum contagiosum
Tiba: Dawa maalum kulingana na ugonjwa (antiviral, antibiotiki, au antifungal)
Mzio wa mafuta, sabuni, pedi au kondomu
Huambatana na kuwasha au upele mwekundu.
Tiba: Epuka kirika, tumia antihistamine au krimu ya hydrocortisone kwa ushauri wa daktari
Magonjwa ya ngozi
Eczema ya sehemu za siri
Psoriasis
Lichen planus/sclerosus
Tiba: Dawa ya kupunguza uvimbe na kuwasha kama vile krimu za steroid
Maambukizi ya fangasi
Upele unaowasha sana, hasa kwa wanawake
Tiba: Antifungal cream au dawa ya kunywa kama fluconazole
Kutokwa jasho sana na msuguano
Huchochea upele kwenye mapaja au korodani
Tiba: Vaa nguo za pamba zisizobana, tumia dawa za kukausha unyevu
Vipele vya kurithi au visivyo na sababu maalumu
Kama folliculitis (kuvimba kwa vinywele)
Tiba: Kusafisha kwa antiseptic, kriam ya antibiotiki
Mambo ya kuzingatia
Epuka kujitibu bila uchunguzi wa daktari
Usitumie dawa za wengine
Tumia sabuni laini zisizo na kemikali kali
Osha sehemu za siri kwa maji safi na kukausha vizuri
Wasiliana na daktari endapo upele unazidi, unauma, unatoka usaha, au haupotei baada ya siku chache
Makala zingine
Unaweza kupenda kusoma makala zingine pia zinazofuata;
Rejea za za mada
Workowski KA, Bolan GA. Sexually transmitted diseases treatment guidelines, 2015. MMWR Recomm Rep. 2015;64(RR-03):1-137.
Bolognia JL, Schaffer JV, Cerroni L. Dermatology. 4th ed. Elsevier; 2018.
Centers for Disease Control and Prevention (CDC). Fungal infections. 2020.
British Association of Dermatologists. Patient Information Leaflets. https://www.bad.org.uk
ULY CLINIC inakushauri uwasiliane na daktari wako kwa ushauri na tiba kabla ya kuchukua hatua yoyote ile baada ya kusoma majibu haya.
Kupata ushauri zaidi au tiba kutoka kwa daktari wa ULY CLINIC bofya hapa au tumia linki ya Pata tiba
