Mwandishi:
Imeboreshwa:
ULY CLINIC
3 Februari 2026, 06:53:15
Anafailaksis
Anafailaksis (kwa Kiingereza anaphylaxis) ni mzio mkali na wa haraka unaoweza kutokea dakika chache baada ya mtu kutumia dawa, kula chakula, au kugusana na kitu kinachosababisha mzio kwake. Ni hali hatari ambayo huhitaji huduma ya haraka ya kitabibu kwa sababu inaweza kuathiri kupumua na mzunguko wa damu.
Dalili za anafailaksis
Dalili zake hujitokeza ghafla na zinaweza kuchanganyika, zikiwemo:
Dalili za jumla
Kupoteza fahamu
Kujisikia joto kali ghafla
Dalili za ngozi
Kuvimba kwa ngozi
Kutokwa jasho jingi au kupauka
Ngozi kupasuka au kuonekana malengelenge makubwa
Dalili za njia ya hewa
Kuhisi unakabwa au kubanwa shingoni
Kuvimba kwa ulimi na midomo
Kutokwa na kamasi
Kupiga chafya au kupumua kwa shida
Dalili za tumbo
Kichefuchefu
Kutapika
Kuharisha
Maumivu ya tumbo
Dalili za mzunguko wa damu
Mapigo ya moyo kwenda haraka
Mapigo ya mishipa kuwa ya kasi
Imeandikwa:
21 Julai 2021, 19:12:31
