top of page

Mwandishi:

Imeboreshwa:

ULY CLINIC

30 Machi 2025, 15:07:56

Multiple sclerosis

Multiple sclerosis

Ni neno tiba lenye jina la kiswahili la "Ugonjwa wa shambulio la mayelini" au "Sklerosisi sambavu"



Ugonjwa wa ni ugonjwa wa mfumo wa neva unaoshambulia mayelin, ambayo ni kizuizi cha mafuta kinachozunguka na kulinda nyuzi za neva (akson). Mayelin ina jukumu muhimu la kusaidia uhamaji wa haraka wa taarifa za umeme kati ya ubongo, uti wa mgongo, na sehemu zingine za mwili.


Katika ugonjwa huu, mfumo wa kinga ya mwili unaanza kushambulia mayelin, na hii husababisha uvimbe na uharibifu kwa mayelin na nyuzi za neva. Matokeo yake ni kwamba taarifa za umeme kutoka kwa ubongo hazipiti vizuri kwenye maeneo yaliyoshambuliwa, na hii inaweza kusababisha matatizo mbalimbali ya kimwili, hisia, na kimawazo.


Ugonjwa huu wa shambulio la mayelini unaweza kusababisha vipindi vya kizunguzungu mzunguko mapema zaidi, ambavyo vinaweza kuwa vya muda mfupi au kuendelea kwa muda mrefu.


Dalili zingine za awali za ugonjwa wa shambulio la mayelini

  • Kizunguzungu mzunguko cha vipindi ambacho kinaweza kuwa endelevu

  • Kuona vitu viwili badala ya kimoja

  • Kuona ukungu

  • Kuwashwa au kufa ganzi


Dalili nyingine zinazoweza kutokea


  • Mjongeo macho usio hiari

  • Kukosa haja kubwa

  • Udhaifu wa misuli

  • Kupooza kwa viungo

  • Misuli kukakamaa

  • Ongezeko la msisimko wa refleksi

  • Mtetemo wa misuli wakati wa kufanya mjongo

  • Ataksia (kutembea kusiko imara kutokana na matatizo ya uratibu wa mjongeo)


Ugonjwa wa shambulio la mayelini ni ugonjwa unaoweza kuja kwa vipindi na kutulia kwa muda au kuendelea polepole.

Imeandikwa:

25 Machi 2025, 11:00:09

bottom of page