top of page
Mwandishi:
Imeboreshwa:
ULY CLINIC
29 Machi 2025, 23:50:32
Trichomoniasis
Ni neno tiba lenye jina la kiswahili la "Trikomoniasisi"
Trikomoniasisi kwa wanawake
Inaweza kusababisha ute wenye harufu mbaya ya uozo, ambao unaweza kuwa wa povu, wa kijani-manjano na mwingi, au mwembamba, mweupe, na kidogo. Dalili nyingine ni pamoja na muwasho, uke mwekundu na uliojaa alama ndogondogo za mvio wa damu , maumivu wakati wa kukojoa na kukojoa mara kwa mara, maumivu wakati wa tendo la ndoa , kutokwa matone ya damu baada ya kujamiiana, hedhi nzito isiyo ya kawaida, au maumivu wakati wa hedhi. Takribani asilimia 70 ya wagonjwa huwa hawaonyeshi dalili za ugonjwa.
Imeandikwa:
29 Machi 2025, 23:50:32
bottom of page
