top of page

Mwandishi:

Imeboreshwa:

ULY CLINIC

13 Julai 2026, 08:01:25

Vipele ni nini?

Vipele ni nini?

Vipele (hufahamika pia kama upele au kipele) ni aina ya tatizo la ngozi linalonekana kama uvimbe mdogo ulioinuka juu ya usawa wa ngozi.


Sifa kuu za vipele

  • Ukubwa: chini ya sentimita 1 (≤1 cm)

  • Umbo: inaweza kuwa duara au isiyo na umbo maalum

  • Rangi: vinaweza kuwa ya rangi ya ngozi, nyekundu, kahawia, au zambarau ikitegemea na rangi ya mtu

  • Muundo: mgumu, hauna usaha kwa ndani

  • Ni tatizo la msingi la ngozi katika matibabu ya ngozi

  • Havitoi majimaji (tofauti na malenge au jibu)

  • Huweza kutoka kama kipele kimoja au kuwa vingi

  • Wakati mwingine huweza kuungana na kutengeneza plagi.


Mifano ya hali zinazotoa vipele

  • Chunusi (vipele vya chunusi)

  • Mzio wa ngozi (vipele vya mzio)

  • Maambukizi ya virusi au bakteria

  • Magonjwa ya ngozi kama likeni planasi


Tofauti na madhaifu mengine ya ngozi

  • Baka(mabaka): Huwa tambarare, hauna mwinuko juu ya usawa wa ngozi

  • Nundu: Huwa kubwa na inaingia zaidi ndani ya ngozi, huzidi ukubwa wa sentimita 1

  • Lenge (malenge): huwa na maji ndani


Hitimisho

Upele ni uvimbe mdogo, mgumu, usio na maji, ulioinuka juu ya usawa wa ngozi, na ni mojawapo ya ishara muhimu katika uchunguzi wa magonjwa ya ngozi. Upele hufahamika na waswahili kwa majina mengine kama vipele, mapele, kipele, uvimbe chini ya sentimita 1 juu ya usawa wa ngozi n.k.

Imeandikwa:

7 Aprili 2026, 04:30:27

bottom of page