top of page
Kamusi Tiba ya ULY CLINIC
Idima
Ni hali ya mkusanyiko usio wa kawaida wa majimaji kwenye tishu za mwili, hasa katika nafasi zilizopo kati ya seli. Hali hii husababisha sehemu ya mwili kuvimba na inaweza kutokea eneo moja au sehemu mbalimbali za mwili. Huonekana mara nyingi kwenye vifundo vya miguu, miguu, mikono na uso, lakini inaweza pia kutokea ndani ya mwili, kama vile kwenye mapafu au tumboni.
bottom of page



