top of page

Kamusi Tiba ya ULY CLINIC

Kipimo cha kuotesha majimaji ya uti wa mgongo ni nini?

Kipimo cha kuotesha majimaji ya uti wa mgongo

Pia huitwa kipimo cha kuotesha vimelea kwenye majimaji ya uti wa mgongo, ni kipimo cha maabara kinachotumika kubaini bakteria wanaoweza kusababisha maambukizi kwenye mfumo mkuu wa fahamu, hasa meninjitisi ya bakteria. Sampuli ya majimaji ya uti wa mgongo huchukuliwa kwa utaratibu wa kitabibu unaoitwa lumbar puncture na kupelekwa maabara kwa ajili ya uchunguzi na kuotesha vimelea.

Kipimo cha kuotesha makohozi ni nini?

Kipimo cha kuotesha makohozi

Pia huitwa kipimo cha kuotesha vimelea kwenye makohozi, ni kipimo cha maabara kinachotumika kubaini bakteria au vimelea wengine wanaoweza kusababisha maambukizi kwenye njia ya upumuaji, hasa mapafu.

Kipimo cha kuotesha mkojo ni nini?

Kipimo cha kuotesha mkojo

Pia huitwa kipimo cha kuotesha vimelea kwenye mkojo, ni kipimo cha maabara kinachotumika kubaini kama kuna bakteria au vimelea wengine wanaosababisha maambukizi katika njia ya mkojo. Sampuli ya mkojo huwekwa kwenye mazingira maalum ya maabara yanayowezesha vimelea kukua na kutambuliwa.

Kipimo cha kuotesha shahawa ni nini?

Kipimo cha kuotesha shahawa

Pia huitwa kipimo cha kuotesha vimelea kwenye shahawa, ni kipimo cha maabara kinachotumika kutafuta na kutambua bakteria au vimelea wengine katika shahawa wanaoweza kuhusishwa na maambukizi ya mfumo wa uzazi wa mwanaume. Sampuli ya shahawa hukusanywa kwenye chombo maalum kisicho na vimelea na kupelekwa maabara kwa ajili ya kuotesha na kutambua vimelea vinavyopatikana

Kipimo cha kuotesha tishu ni nini?

Kipimo cha kuotesha tishu

Pia huitwa kipimo cha kuotesha vimelea kutoka kwenye tishu, ni kipimo cha maabara kinachotumika kutambua bakteria, fangasi au vimelea wengine wanaoweza kusababisha maambukizi kwenye tishu za mwili. Sampuli ya tishu huchukuliwa kutoka kwenye eneo linaloshukiwa kuwa na maambukizi, kwa mfano wakati wa upasuaji, kutoka kwenye jeraha, jipu au tishu iliyoathirika, kisha hupelekwa maabara kwa ajili ya kuotesha na kutambua vimelea

bottom of page