top of page
Kamusi Tiba ya ULY CLINIC
Upungufu wa protini mwilini
Ni hali ambapo kiwango cha protini, hasa alibumini, huwa chini kuliko kiwango kinachotarajiwa katika damu. Alibumini husaidia kushikilia majimaji ndani ya mishipa ya damu, hivyo kiwango chake kinapopungua, majimaji yanaweza kutoka kwenye mishipa na kujikusanya kwenye tishu na kusababisha idima.
Upungufu wa pumzi
Ni hali ya mtu kuhisi kuwa anapata hewa kidogo, anashindwa kuvuta pumzi vizuri, au anahitaji kutumia nguvu zaidi ili kupumua. Mtu anaweza kuhisi kama kifua kinabanwa, hawezi kuvuta pumzi ya kutosha au anahitaji kupumua kwa haraka kuliko kawaida. Kwa lugha nyingine ya kitabibu, hali hii huitwa disipnia.
bottom of page

