top of page

Mwandishi:

Mhhariri

ULY CLINIC

Dkt. Benjamin L, MD

Jumatano, 7 Julai 2021

Amibiasis kwa watoto

Amibiasis kwa watoto

Mara nyingi kimelea cha amiba anaweza kuingia kwenye mfumo wa umeng’enyaji chakula na kuishi bila kusababisha dalili yoyote ile, isipokuwa akivamia kuta za utumbo mpana. Uvamizi kwenye utumbo mpana husababisha dalili za kuharisha damu, maumivu na kunyonga kwa tumbo, kichefuchefu, kukosa hamu ya kula na homa. Amiba anaweza safari kwenda pia kwendaogani nyingine ndani ya mwili na kusababisha maambukizi kwenye Ini, mapafu moyo na ubongo.


Dalili za amibiasis kwa watoto


Watoto wenye maambukizi ya amiba huwa hawaonyesi dalili au kuwa na dalili kizsi tu. Baadhi ya watoto hupata dalili ndani ya siku au wiki chache, lakini wapo baadhi pia hupata baada ya miezi kadhaa kupita.


Endapo dalili zitatokea zinajumuisha;

  • Maumivu ya tumbo yanayoanza taratibu na kuambatana na choo kilaini au cha majimaji

  • Kunyonga kwa tumbo

  • Kichefuchefu

  • Kupoteza hamu ya kula

  • Haja kubwa yenye kamasi


Dalili zingine zinazoweza kutokea kwa baadhi ya watoto ni;

  • Homa

  • Haja kubwa yenye damu


Wakati gani uwasiliane na daktari haraka endapo mwanao ana dalili za amibiasis?


Wasiliana na daktari haraka kwa matibabu endapo mwanao ana dalili zifuatazo;


  • Kuharisha damu au kupata kinyesi chenye kamasi

  • Maumivu ya tumbo ( ataonekana kwa kukunja sura au kujikunja mwili seemu ya tumbo) kwa mtoto mkubwa atasema kuwa ana maumivu ya tumbo

  • Kuchemka

  • Kujaa kwa tumbo

  • Maumivu sehemu ya kulia chini ya mbavu


Vihatarishi vya maambukizi ya amiba kwa watoto

Maambukizi ya amiba hutokea mara nyingi kwenye maeneo yasiyo na mfumo mzuri wa utunzaji wa maji taka. Maeneo hayo hujumuisha maeneo yenye yenye mkusanyiko mkubwa wa watu na yasiyo na utunzaji mzuri wa kinyesi cha binadamu. Hii ndio maana ugonjwa huu hutokea katika nchi masikini au zile zinazoendelea duniani. Mfano endapo shimo la choo limechimbwa karibu na vyanzo vya maji, maji yenye vimela kutoka kwenye kinyesi hupenya kuingia kwenye vyanzo vya maji iwe kisima, mto au chanzo chochote kilicho karibu na makazi ya watu. kisima, Maji haya yakitumiwa bila kutibiwa, hupelekea kutokea kwa maambukizi ya kujirudia rudia.


Endapo mtu atajisaidia karibu na chanzo cha maji au kumwaga kinyesi kwenye maji au kutumia kinyesi cha binadamu kama mbolea, au kumwagilia maji yaliyo na kinyesi kwenye mazao, hupelekea kusambaza kwa maambukizi kwa kula vyakula hivyo.


Mtoto kula mchanga au udongo wenye mayai ya kimelea pia huwa chanzo kingine cha kupata maambukizi kwa watoto wanaoanza kutambaa.


Namna gani mtoto anapata maambukizi ya amiba?


Mtoto anaweza pata maambukizi ya amiba kwa kunywa maji au kula chakula kilichochanganyika na kinyesi chenye vimelea. Chakula kinaweza kuchanganyika na vimelea kwa njia mbalimbali kama vile;

  • Kuandaliwa chakula na mtu mwenye maambukizi pasipo kufanya usafi wa mikono kwa maji salama ( mtoto kula tunda lililoshikwa na mwenye maambukizi, au mtoto kula vidole vya mkono ulioshikwa na mtu mwenye maambukizi ambaye hajanawa mikono kwa maji safi baada ya kujisadia.

  • Kutumia vyombo vya mtu mwenye maambukizi, mfano kutumia bilauri moja ya kunywea maji, au vyombo vilivyoshikwa na mtu mwenye maambukizi ambaye hazingatii usafi wa mikono

  • Kutumia maji ya kunywa yasiyo salama, mfano yaliyochotwa mtoni au ambayo hayajachemshwa

  • Kula matunda yaliyosafishwa kwa maji yasiyo salama

  • Kunawa mikono kwa maji yasiyo salama

  • Kula udongo au mchanga wenye mayai ya kimelea cha amiba


Vipimo vya amiba kwa watoto

Baada ya kuchukuliwa historia ya dalili za mtoto na kufanyiwa vipimo vya awali vya mwili, daktari ataagiza mtoto afanyiwe vipimo mbalimbali. Kinyesi kitakusanywa kisha kupelekwa maabara kwa vipimo vya;


  • Kuchunguza uwepo wa amiba kwa hadubini

  • Kupima antijeni za amiba kwenye kinyesi


Matibabu ya amibiasis kwa watoto

Matibabu ya amibiasis hulenga katika kuondoa maambukizi na kuthibiti dalili zilizojitokeza. Dawa inayotumika sana kwa watoto ni metronidazole au Tinidazo (kwa watoto zaidi ya miaka 3) au dawa zingine zinazotumika kwa kuunganishwa zaidi ya moja kama;


  • Paromomycin (Humatin®)

  • Dehydroemetine

  • Tetracycline

  • Diloxanide Furoate

  • Diquinol


Matibabu mengine hutegemea hali ya mtoto, endapo mtoto anahara, utashauriwa kumpa maji ya kutosha au maji ya oral (ORS). Endapo mtoto ameharisha sana pia na ana hali mbaya anaweza kuongezewa maji hospitali.


Inachukua muda gani kupona amibiasis baada ya kuanza kutumia dawa?

Kwa kawaida inachukua kati ya wiki 1 hadi 3 kwa maambukizi kuisha kabisa mwilini bada ya kuanza kutumia dawa. Hata hivyo dalili zinaweza kupotea kabia kati ya wiki ya kwanza na pili tangia mtoto amenaz akutumia dawa. Amibiasis nje ya tumbo huweza kuchukua muda mrefu kupona.


Magonjwa yanayoweza kufanana dalili na amibiasis

Sio kila dalili za amiba humaanisha amibiasis, hii inafanya umuhimu wa kuonana na daktari kwa uchunguzi na vipimo kabla ya kuanza kutumia dawa. Magonjwa mengine yanayofanana sana dalili na maambukizi ya amiba kwa watoto ni;


  • Shigellosis

  • Salmonellosis

  • Campylobacteriosis

  • Homa ya enterohemorrhagic Escherichia coli,


Hata hivyo utofauti wa amibiasis na magonjwa haya ni dalili, dalili za magonjwa hayo huanza haraka zaidi ukiliganisha na amibiasis.


Madhara ya amibiasis kwa watoto

Madhara yafuatayo yanaweza kutokea endapo mtoto hatapata matibabu mapema. Inakadiliwa asilimi 7 hadi 30 ya wagonjwa wanawez akupta madhara haya wasipopata matibabu.


  • Intusasepsheni

  • Kutoboka kwa utumbo

  • Peritonaitiz

  • Kuoza kwa utumbo ( NEC)


Namna ya kumkinga mtoto kupata amibiasisi

Ili kumkinga mtoto na maaambukizi ya amiba, unaweza fanya mambo yafuatayo;


  • Tenge vyombo vya mtoto na watu wazima mfano vyombo vya kuogea, vya kunywea maji n.k

  • Nawa mikono wa maji safi baada ya kutoka chooni

  • Safisha mboga za majani na matunda kwa maji safi kabla ya kuliwa au kupika. Tumia maji salama yaliyotiwa iodine au chlorine

  • Jenga choo mbali na vyanzo vya maji

  • Mfundishe mtoto kutokula mchanga au vidole bila kunawa. Au tumia viziba mdomo ili asile mikono akishika chini


Matibabu ya dawa asilia

Kuna mambo na dawa asilia unaweza kutumia kwa matibabu ya amibiasisi kwa watoto, dawa hizo zinapatikana kwa madaktari wa tiba asilia na zingine zinauzwa internet. Matibabu hayo huweza kuwa;


  • Maji ya nazi

  • Maziwa yaliyotolewa siagi baada ya kuchacha

  • Vinega ya tufaa

  • Chai nyeusi

  • Vitunguu swaumu


Kusoma namna gani ya kutumia na vinavyofanya kazi, ingia kwenye makala zingine za dawa asilia ya amiba.


Majina mengine ya maambukizi ya amibiasis kwa watoto

Baadhi ya watu hutumia majina yafuatayo kumaanisha maambukizi ya amibiasisi kwa watoto


  • Amiba kwa watoto

  • Ugonjwa wa amoeba kwa watoto

  • Ugonjwa wa amoebiasis kwa watoto

  • Matibabu ya amiba kwa watoto

ULY CLINIC inakushauri siku zote uwasiliane na daktari wako kwa ushauri na tiba kabla ya kuchukua hatua yoyote ya kitiba baada ya kusoma makala hii.

Wasiliana na daktari wa ulyclinic kwa ushauri zaidi na tiba kwa kubofya 'Pata Tiba,  au ''mawasiliano yetu' chini ya tovuti hii

Imeboreshwa,

13 Julai 2023, 18:26:42

Rejea za mada hii:

1. Amebiasis. https://pedsinreview.aappublications.org/content/23/8/293. Imechukuliwa 07.07.2021

2. Rashidul Haque, et al. Entamoeba histolytica Infection in Children and Protection from Subsequent Amebiasis. https://www.ncbi.nlm.nih.gov/pmc/articles/PMC1360358/#. Imechukuliwa 07.07.2021

3. C. J. Rubidge, et al. Treatment of Children with Acute Amoebic Dysentery Comparative Trial of Metronidazole against a Combination of Dehydroemetine, Tetracycline, and Diloxanide Furoate. https://www.ncbi.nlm.nih.gov/pmc/articles/PMC2020286/. Imechukuliwa 07.07.2021

4. Antonio Peña Chavarria, M.D, et al. Treatment of Children with Intestinal Amebiasis Due to Entamoeba Histolyticawith a Single Dose of Paromomycin (Humatin®). https://academic.oup.com/milmed/article-abstract/131/4/379/4918789?redirectedFrom=PDF. Imechukuliwa 07.07.2021

5. Amoebiasis treatment. https://www.drugs.com/health-guide/gastrointestinal-amebiasis.html. Imechukuliwa 07.07.2021

bottom of page