top of page

Mwandishi:

Mhhariri

Dkt. Sospeter B, MD

Dkt. Peter A, MD

Alhamisi, 21 Julai 2022

Ugonjwa Leptospirosis

Ugonjwa Leptospirosis

Leptospirosis ni ugonjwa unaoweza kumpaka binadamu na mnyama. Kwa miaka mingi ugonjwa huu umekuwa hautokei sana kwa wanyama hata hivyo hivi karibuni kumekuwa na visa vingi. Kumekuwa na visa mbalimbali vimeripotiwa nchini Tanzania kuhusu Leptospirosis kati ya mwezi wa 6 na 7/2022.


Bakteria wanaosababisha Leptospirosis huenezwa kupitia mkojo wa wanyama walioambukizwa, na wanaweza kuingia ndani ya maji au udongo kisha kuishi huko kwa wiki hadi miezi. Aina mbalimbali za wanyamapori na wa nyumbani hubeba bakteria hao.


Wanyama hao hujumuisha, licha ya kutokuwa wao tu:


  • Ng'ombe

  • Nguruwe

  • Farasi

  • Mbwa

  • Panya

  • Wanyama wa mwituni


Wakati wanyama hawa wanaambukizwa, wanaweza wasionyeshe dalili za ugonjwa. Wanyama alioambukizwa wanaweza kuweka bakteria katika mazingira kupitia kinyesi au mkojo kila mara au kwa kipindi cha miezi michache hadi miaka kadhaa.


Uambukizaji wa bakteria wa Leptospirosis kwa binadamu


Binadamu wanaweza kuambukizwa bakteria wa Leptospirosis kupitia:


  • Kugusana na mkojo (au viowevu vingine vya mwili, isipokuwa mate) kutoka kwa wanyama walioambukizwa

  • Kugusana na maji, udongo, au chakula kilichochafuliwa na mkojo wa wanyama walioambukizwa


Namna bakteria wanavyoingia mwilini mwa binadamu


  • Bakteria wanaweza kuingia mwilini kupitia ngozi au utando wa laini wa ngozi (macho, pua, au mdomo), hasa ikiwa ngozi imepasuka kutokana na kujikata au mikraruzo. Unywaji wa maji machafu pia unaweza kusababisha maambukizi.

  • Mlipuko wa Leptospirosis kawaida husababishwa na utumiaji wa maji yaliyochafuliwa na vimelea, kama vile maji ya mafuriko. Maambukizi ya kutoka kwa mtu kwenda kwa mtu mwingine ni nadra sana kutokea.


Dalili za Leptospirosis


Kwa wanadamu, Leptospirosis inaweza kusababisha dalili mbalimbali, ikiwa ni pamoja na:

  • Homa kali

  • Kichwa

  • Baridi

  • Maumivu ya misuli

  • Kutapika

  • Ngozi ya manjano na macho

  • Macho mekundu

  • Maumivu ya tumbo

  • Kuhara

  • Harara kwenye ngozi


Nyingi ya dalili hizi zinaweza kuchanganywa na dalili za magonjwa mengine. Kwa kuongezea, baadhi ya watu walioambukizwa wanaweza wasionyeshe dalili yoyote ile.

Muda wa ugonjwa wa leptospirosis kuonekana


Mara baada ya kuambukizwa, huchukua siku 2 hadi wiki 4 kwa dalili kuonekana. Mara nyingi ugonjwa huanza ghafla kwa kusababisha homa na dalili zingine.


Awamu za ugonjwa wa leptospirosis


Leptospirosis huweza kutokea katika awamu mbili ambazo ni:


  • Baada ya awamu ya kwanza (na homa, baridi, maumivu ya kichwa, maumivu ya misuli, kutapika, au kuhara) mgonjwa anaweza kupona kwa muda lakini hugua tena.

  • Ikiwa awamu ya pili itatokea, ni kali zaidi; mtu anaweza kuwa na kushindwa kwa figo au ini au homa ya uti wa mgongo.

Muda wa ugonjwa wa leptospirosis kupotea


Ugonjwa huu hudumu kwa siku chache hadi wiki 3 au zaidi, na pasipo matibabu, inaweza kuchukuchua miezi kadhaa kupona.


Vihatarishi vya kupata leptospirosis


Leptospirosis hutokea duniani kote, lakini ni kawaida katika hali ya hewa ya joto au kitropiki. Watu wafuatao huwa na hatari kubwa zaidi ya kupata ugonjwa:


  • Wakulima

  • Wafanyakazi wa mgodi

  • Wazibua vyoo

  • Wafanyakazi wa machinjio

  • Wafugaji na walezi wa wanyama

  • Wafanyakazi wa samaki

  • Wakulima wa maziwa

  • Wafanyakazi wa jeshi


Ugonjwa huu pia unaonekana kuenezwa sana kwa watu wanaofanya kazi kwenye maji au kuogelea kwenye ziwani.


Matibabu ya leptospirosis


  • Leptospirosis hutibiwa kwa antibayotiki kama vile doxycycline au Penisilini, ambayo inapaswa kutolewa mapema wakati wa ugonjwa huo.

  • Antibiotiki za za mishipa zinaweza kuhitajika kwa watu wenye dalili kali zaidi. Watu walio na dalili zinazoashiria ugonjwa huu wanapaswa kuwasiliana na mtoa huduma ya afya mara moja kwa ushauri na tiba.


Kinga ya leptospirosis


Maambukizi ya Leptospirosis yanaweza kupunguzwa kwa kuacha kuogelea au kufanya kazi kwenye maeneo yenye maji yaliyochafuliwa na vimelea kwa mkojo au kinyesi chao.


Vifaa kinga kama viatu na glavu vinapaswa kuvaliwa kwa wale wanaofanya kazi kwenye maji yaliyochafuliwa na vimelea au wanaofanya michezo mbalimbali katika maji hayo yanayoguswa na wanyama.

ULY CLINIC inakushauri siku zote uwasiliane na daktari wako kwa ushauri na tiba kabla ya kuchukua hatua yoyote ya kitiba baada ya kusoma makala hii.

Wasiliana na daktari wa ulyclinic kwa ushauri zaidi na tiba kwa kubofya 'Pata Tiba,  au ''mawasiliano yetu' chini ya tovuti hii

Imeboreshwa,

21 Julai 2022, 18:50:03

Rejea za mada hii:

1. Surveillance for Waterborne Disease and Outbreaks Associated with Recreational Water Use and Other Aquatic Facility-Associated Health Events—United States, 2005–2006. MMWR September 12, 2008;57(SS09):1-29.
2. Surveillance for Waterborne Disease and Outbreaks Associated with Recreational Water—United States, 2003r–2004. MMWR December 22, 2006;55(SS12):1-24.
3. Surveillance for Waterborne-Disease Outbreaks—United States, 1999–2000. MMWR November 22, 2002; 51(SS08):1-28.
4. Update: Outbreak of Acute Febrile Illness Among Athletes Participating in Eco-Challenge-Sabah 2000—Borneo, Malaysia, 2000. MMWR January 19, 2002;50(02):21-24.
5. Public Health Dispatch: Outbreak of Acute Febrile Illness Among Participants in EcoChallenge Sabah 2000 Malaysia, 2000. MMWR September 15, 2000;49(36):816-817.
6. Update: Leptospirosis and Unexplained Acute Febrile Illness Among Athletes Participating in Triathlons—Illinois and Wisconsin, 1998. MMWR August 21, 1998;47(32):673-676.
7. Outbreak of Acute Febrile Illness Among Athletes Participating in Triathlons—Wisconsin and Illinois, 1998. MMWR July 24, 1998;47(28):585-588.
8. Outbreak of Leptospirosis Among White-Water Rafters—Costa Rica, 1996. MMWR June 27, 1997;46(25):577-579.
9. Guerra MA. Leptospirosis. J Am Vet Med Assoc. Feb 15 2009;234(4):472-478 (430).
10. Levett PN. Leptospira and Leptonema. In: Murray PR, Baron EJ, Pfaller MA, Tenover FC, Yolken H, eds. Manual of clinical microbiology. 8th ed. Washington, DC, ASM Press, 2003 (in press).
11. Levett PN. Leptospirosis. Clin Microbiol Rev 2001; 14: 296-326.
12. Tappero JW, Ashford DA, Perkins BA. Leptospirosis. In: Mandell GL, Bennet JE, Dolin R, eds. Principles and Practice of Infectious Diseases. Fifth Edition. New York: Churchill Livingstone, 2000: 2495-2501.

bottom of page