top of page

Mwandishi:

ULY CLINIC

Mhariri:

Dkt. Salome A, MD

Alhamisi, 4 Machi 2021

Kunyonyesha huku umekunja nne huweza kukufikasha kileleni

Kunyonyesha huku umekunja nne huweza kukufikasha kileleni

Inafahamika kisayansi kuwa, baadhi ya wanawake wanaonyonyesha , mtoto anaponyonya chuchu huamsha hisia kali za kingono zinazoweza kupelekea mama kufika kileleni wakati wa kunyonyesha huku amekunja nne. Hii ni kawaida kifiziolojia, mama anashauriwa kuacha kukunja nne wakati wa kunyonyesha endapo kupatwa na hisia hii inamfanya ajihukumu.


Hata hivyo baadhi ya wamama hujihukumu sana wanapopata hisia hizi, isitoshe wengine huamua acha kunyonyesha kabisa kuhofia kupata hisia hizo zinazoamshwa na mtoto anayenyonya. Baadhi ya wamama wanaporipoti hali hii kwa watu wasio wataalamu wa afya au wataalamu wa afya, watu hawa hushangaswa , humchukuliwa mama mkosaji na hata kumtilia shaka mama kuwa ana mahusiano ya kimapenzi na mtoto.


Kwanini mama anapata hisia za ngono na anafika kileleni ankinyonyesha huku amekunja nne?

Tafiti zinaonyesha kuwa, hali hii ya kufika kileleni inaweza kuashwa kwa kiasi kikubwa endapo mama atakunja nne wakati wa kunyonyesha. Hii ni kwa sababu, mama anapokunja nne, hukutanisha mashavu madogo ya uke na kufanya yasuguane na kusugua kinembe na kisha kufanya mama apate mshindo mkubwa kutokana na kugusana kwa kinembe na mashavu madogo pamoja na madhara ya homoni oxytocin inayosababisha ongezeko la mshindo.

ULY CLINIC inakushauri siku zote uwasiliane na daktari wako kabla ya kuchukua hatua yoyote ile kiafya baada ya kusoma vidokezo hivi

Wasiliana na daktari wa ULY CLINIC kwa elimu na ushauri zaidi kupitia namba za simu au kubonyeza 'Pata Tiba' Chini ya tovuti hii.

Imeboreshwa,

19 Julai 2023, 20:40:48

Rejea za mada hii:

Kwanini mama anaweza fika kileleni akinyonyesha huku amekunja nne?

bottom of page