top of page

Mwandishi:

Mhariri:

Imeboreshwa:

WAMJW

ULY CLINIC

24 Agosti 2026, 03:43:15

Azuma na COVID-19

COVID-19 ni ugonjwa unaosababishwa na virusi vya Corona. AZUMA ni dawa ya kuua bakteria (antibiotiki) sio virusi. Hata hivyo, mpaka sasa hivi hakuna dawa iliothibitishwa kutibu COVID-19. Lakini hata hivyo, mapafu ya mgonjwa wa COVID-19 yanaweza pia kushambuliwa na bakteria na kusababisha madhara zaidi. Hivyo basi, ili kupunguza haya madhara, AZUMA nia mojawapo ya dawa ambazo mgonjwa wa COVID-19 hupewa na daktari hospitalini kulingana na hali ya mgonjwa ilivyo.


Kumbuka, matumizi holela ya dawa za antibiotiki kama AZUMA bila ushauri wa Daktari ni hatari kwani unaweza kupelekea kuibuka kwa usugu wa vimelea kwenye dawa.

Imeandikwa:

2 Aprili 2026, 19:07:10

ULY CLINIC inashauri usitegemee au kufuata ushauri wowote uliyoona kwenye makala hii bila kuwasiliana kwanza na daktari wako. Kabla ya kuchukua hatua yoyote ya matibabu, hakikisha umepata ushauri rasmi kutoka kwa daktari wako ili kuepuka madhara yoyote yanayoweza kutokea.

​

Makala hii ni ya kielimu tu na haitumiki kama mbadala wa matibabu ya daktari.

Rejea za mada hii:

bottom of page