top of page

Mwandishi:

Mhariri:

Imeboreshwa:

ULY CLINIC

Dkt. Helen L, M.D

2 Aprili 2026, 16:17:50

Muda unaotosha kulala

Muda wa kulala kiafya hutegemea umri wa mtu na hupungua kwa jinsi umri unavyoongezeka. Mfano kichanga anapaswa kulala angalau muda wa masaa 14 hadi 17, vijana wadogo, masaa 7 hadi 9, wazee wa miaka 65 na zaidi, ni masaa 7 hadi 8 wakati wa usiku. Lala muda wa kutosha kwa afya yako


Muda wa kulala kulingana na umri


Kwa vinaja wadogo na watu wazima, wanashauriwa kulala kulala angalau kwa muda wa masaa 8 hadi 9 mfululizo wakati wa usiku, wakati huo watoto wadogo wanatakiwa kulala masaa mengi zaidi kuliko watu wazima au wazee. Ukilala muda wa kutosha utaimarisha mwili wako kiakili na kifizikia, watoto wadogo pia wanapaswa kulala muda wa kutosha ili wakue vema. Usiwe na tabia ya kulala muda pungufu au zaidi ya masaa yanayoshauriwa kiafya.


Umri wa siku 0 hadi miezi 11


Watoto wenye siku 0 hadi umri wa miezi 3

Muda wa kulala ni angalau masaa 14 hadi 17 kwa siku


Watoto wenye umri wa miezi 4 hadi miezi 11

Muda wa kulala ni angalau masaa 12 hadi 15 kwa siku


Umri wa Mwaka 1 hadi miaka 5


Watoto wenye umri wa mwaka 1 hadi miaka 2

Muda wa kulala ni angalau masaa 11 hadi 14 kwa siku


Watoto wenye umri wa miaka 3 hadi miaka 5

Muda wa kulala ni angalau masaa 10 hadi 13 kwa siku


Umri wa miaka 6 hadi 17

Watoto wenye umri wa miaka 6 hadi miaka 13


Muda wa kulala ni angalau masaa 9 hadi 11 mfululizo kwa siku


Watoto wenye umri wa miaka 14 hadi miaka 17

Muda wa kulala ni angalau masaa 8 hadi 10 mfululizo kwa siku


Umri wa miaka 18 na zaidi


Vijana wadogo wenye umri wa miaka 18 hadi miaka 25

Muda wa kulala ni angalau masaa 7 hadi 9 mfululizo kwa siku


Watu wazima wenye umri wa miaka 26 hadi miaka 64

Muda wa kulala ni angalau masaa 7 hadi 9 mfululizo kwa siku


Wazee wenye umri wa miaka 65 au zaidi

Muda wa kulala ni angalau masaa 7 hadi 8 mfululizo kwa siku

Imeandikwa:

2 Aprili 2026, 16:17:50

ULY CLINIC inashauri usitegemee au kufuata ushauri wowote uliyoona kwenye makala hii bila kuwasiliana kwanza na daktari wako. Kabla ya kuchukua hatua yoyote ya matibabu, hakikisha umepata ushauri rasmi kutoka kwa daktari wako ili kuepuka madhara yoyote yanayoweza kutokea.

​

Makala hii ni ya kielimu tu na haitumiki kama mbadala wa matibabu ya daktari.

bottom of page