Maelezo ya majibu ya maswali mbalimbali ya kiafya

Imarisha kinga ya mwili wako kwa chakula
Uwezo wa mwili kupambana na maradhi hutegemea kile unachokula. Kuuongezea mwili wako uwezo wa kukukinga na kuponya maradhi ya virusi, bakteria na fangasi, tumia mara kwa mara vyakula kama vile matunda yenye uchachu, pilipili hoho, tangawizi, vitunguu swaumu, spinachi n.k. Kula vema ujiepushe na maradhi.

Zuia kusafirisha vimelea vya maradhi unapokohoa
Magonjwa mengi ya mfumo wa hewa kama Kifua kikuu, mafua ya virusi, nimonia na mengine husafirishwa kwa njia ya matone ya maji maji yanayotoka wakati mtu anakohoa au kupiga chafya. Zuia magonjwa haya kwa kufunika kinywa chako na kitambaa, tishu au kiwiko cha mkono.

Kuongezewa damu
Ni tendo la kitiba la kuongeza ujazo wa damu iliyotolewa kwa mtu mwenye afya kwenda kwa muhitaji kupitia mishipa ya damu. Sababu zinazopelekea kuongezewa damu mara nyingi hutokana na ajali, upasuaji na magonjwa yanayomaliza damu. Kuna njia zingine za kuongeza damu, hata hivyo si rahisi kutumika kama mbadala wa kuongezewa damu.



